Datasets:
Dataset Viewer
title
stringlengths 1
120
| text
stringlengths 257
48.7k
| source
stringclasses 2
values | url
stringlengths 31
150
| scraped_date
stringclasses 38
values | id
int64 0
58.4k
|
|---|---|---|---|---|---|
Mto Gakarazi
|
'''''' ni korongo linalopatikana magharibi mwa Burundi (mkoa wa Bubanza). Maji yake huelekea Ziwa Tanganyika, Mto Kongo na hatimaye bahari ya Atlantiki. * Orodha ya mito ya mkoa wa Bubanza * Orodha ya mito ya Burundi * Mito mirefu ya Afrika * [http://www.geonames.org Geonames.org] G Jamii:Mkoa wa Bubanza Jamii:Ziwa Tanganyika Jamii:Mto Kongo Jamii:Atlantiki
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mto_Gakarazi
| null | 32,069
|
Ellie Highwood
|
'''Ellie Highwood''' ni mshauri na mkufunzi kwa wasomi, watafiti na wanasayansi. Hapo awali alikuwa Profesa wa Fizikia ya Hali ya Hewa Chuo Kikuu cha Reading na alikuwa mkuu wa idara hiyo kuanzia mwaka [] hadi []. Pia alikuwa mwanachama wa Baraza la RmetS na Kamati ya Elimu. Mnamo tarehe 1 Oktoba [] alikua Raisi wa 81 wa Jumuiya ya Kifalme ya Hali ya Hewa (RMetS), akihudumu hadi mwaka []. Highwood alisomea fizikia Chuo Kikuu cha Manchester na kisha akasomea PhD Chuo Kikuu cha Reading . Utafiti wake unazingatia chembe za anga katika hali ya hewa, haswa athari za erosoli kwenye mabadiliko ya hali ya hewa na mifano ya hali ya hewa. Kuanzia mwaka []-[] pia alichukua nafasi ya Dean for Diversity and Inclusion kutoka Chuo Kikuu cha Reading, ambacho kilikuwa sehemu ya kazi na Profesa Simon Chandler-Wilde. Mnamo mwaka wa [] aliacha ulimwengu wa utafiti wa kitaaluma na kuanzisha biashara zake mwenyewe zinazozingatia kukuza mashirika ya umoja na kusaidia wasomi, watafiti na wanasayansi kupitia kufundisha mtu binafsi na timu. Kazi yake kuhusu erosoli na athari zake kwa hali ya hewa na mabadiliko ya hali ya hewa zimejadiliwa katika machapisho mashuhuri, kama vile ''The Independent'' na BBC . Amedai kuwa kupooza sayari kiholela kwa "kuingiza chembechembe ndogo za kuakisi kwenye angahewa" (kama ilivyopendekezwa na Paul Crutzen, kwa mfano) kunaweza "kusababisha ukame na machafuko ya hali ya hewa" katika nchi maskini, pia akisema kuwa "itakuwa busara kuchunguza njia mbadala ambazo zinaweza kutusaidia katika miongo ijayo". Jamii:Watu walio hai Jamii:Wanasayansi wa Uingereza Jamii:Wanawake wa Uingereza
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ellie_Highwood
| null | 38,743
|
Wa, Ghana
|
alt=Mwonekano wa Wa katika Mkoa wa Juu Magharibi mwa Ghana, uliochukuliwa kutoka mnara wa msikiti|thumb|Mwonekano wa Wa katika Mkoa wa Juu Magharibi mwa Ghana, uliochukuliwa kutoka mnara wa msikiti '''''' ni mji wa Jamhuri ya Ghana. Ndiyo makao makuu ni mkoa wa Magharibi ya Juu. Katika sensa ya mwaka [] kulikuwa na wakazi 105,821 * Orodha ya miji ya Ghana Jamii:Miji ya Ghana Jamii:Mkoa wa Mashariki ya Juu
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wa,_Ghana
| null | 37,884
|
Anne Brodsky
|
'''Anne Ellen Brodsky''' alizaliwa Juni 11, [], nchini Marekani. ni Profesa katika idara ya saikolojia na Gender and Women's Studies katika Chuo Kikuu cha Maryland, Baltimore County (UMBC). Pia, ni Mkurugenzi wa Programu ya Gender and Women's Studies, na Mwenyekiti wa Idara ya Saikolojia. Pia, ameandika kitabu kiitwacho, "With All Our Strength: The Revolutionary Association of the Women of Afghanistan." Brodsky ni binti wa Allan J. na Clementine Brodsky wa Shaler Township, Pennsylvania. Alihudhuria Shaler Area High School na alipata shahada yake ya kwanza (B.A.) kutoka Chuo Kikuu cha Vassar, Shahada ya Uzamifu (M.A.) kutoka Chuo Kikuu cha Maryland, na Shahada ya Uzamivu (Ph.D.) kutoka Chuo Kikuu cha Maryland, na aliendelea na masomo ya baada ya uzamivu kutoka Shule ya Afya ya Umma ya Johns Hopkins. Jamii:Waliozaliwa 1965 Jamii:Wanawake wa Marekani Jamii:Wanasaikolojia wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Anne_Brodsky
| null | 46,939
|
Katente
|
'''Katente''' ni kata ya Wilaya ya Bukombe, Tanzania yenye msimbo wa posta namba '''30514''' [https://tcra.go.tz/services/publication-of-postcode-list Tanzania Postcode List]. Katika sensa ya mwaka [] wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 32,323 https://www.nbs.go.tz, uk 228 . Wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka [], idadi ya wakazi wa kata ilikadiriwa kuwa watu 14,273.[https://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/majimbo/MAJIMBOApril_Kisw.pdf Makadirio ya Idadi ya Watu katika Majimbo ya Uchaguzi kwa Mwaka 2016, Tanzania Bara], Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dar es Salaam April 2016, iliangaliwa Mei 2021 Jamii:Wilaya ya Bukombe Jamii:kata za Mkoa wa Geita
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Katente
| null | 35,330
|
Lugha ya ishara ya Kituruki
|
'''Lugha ya ishara ya Kituruki''' ni lugha inayotumiwa na jamii ya viziwi nchini Uturuki. Kama ilivyo kwa lugha zingine za ishara, TİD ina sarufi ya kipekee ambayo ni tofauti na lugha zinazotumiwa katika eneo hilo. TİD inatumia alfabeta ya mikono miwili ambayo ni tofauti sana na alfabeti za mikono miwili zinazotumika katika lugha za alama za BANZSL. Pia, hutumia ulimi katika misemo fulani. Kuna taarifa chache zilizochapishwa kuhusu Lugha ya Alama ya Kituruki. Lugha ya alama ya Kituruki inaonyesha mpangilio wa kitenzi-kihitimisho (SOV). Pia, ina seti tajiri ya vitenzi vya modal ambavyo vinaonekana mwishoni mwa sentensi. Kulingana na Taasisi ya Takwimu ya Kituruki, kuna jumla ya watu 89,000 (wanaume 54,000, wanawake 35,000) wenye urema wa kusikia na watu 55,000 (wanaume 35,000, wanawake 21,000) wenye urema wa kuzungumza wanaoishi nchini Uturuki, kulingana na sensa ya mwaka [].[http://www.tuik.gov.tr/AltKategori.do?ust_id=11&ust_adi=N%FCfus%2C+Konut+ve+Demografi Türkiye İstatistik Kurumu, Nüfus, Konut ve Demografi Verileri 2000] TİD ni tofauti na lugha za alama za Ulaya. Kulikuwa na lugha ya alama ya korti ya Milki ya Ottoman, ambayo ilifika kilele chake karne ya 16 na 17 na ilidumu angalau hadi mwanzo wa karne ya 20. Hata hivyo, hakuna rekodi ya alama hizo wenyewe na hakuna ushahidi kwamba lugha hiyo ilikuwa asili ya Lugha ya Alama ya Kituruki ya kisasa.[http://turkisaretdili.ku.edu.tr/en/tid.aspx ''Turkish Sign Language (TİD) General Info''] , Dr. Aslı Özyürek, Koç University website, accessed 2011-10-06 Shule za viziwi zilianzishwa mwaka [], na hadi [] zilitumia TİD pamoja na lugha ya Kituruki ya kuzungumza na maandishi katika elimu.Deringil, S. (2002). İktidarın Sembolleri ve İdeoloji: II. Abdülhamid Dönemi (1876–1909), YKY, İstanbul, 249. Tangu mwaka 1953, Uturuki umeanzisha mbinu ya kuzungumza (oralism) katika elimu ya viziwi. jamii:WikiMonthly Edit-a-thon Kilimanjaro Jamii:Wiki4Inclusion Campaign in Tanzania
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha_ya_ishara_ya_Kituruki
| null | 47,975
|
Lana Chapel
|
'''Lana Chapel''' ni binti wa mtunzi wa nyimbo na mwimbaji wa muziki wa country na rock & roll Jean Chapel maarufu kama '''Mattie O'Neil''' na mume wake, msanii wa western swing, mtunzi wa nyimbo, mwanamuziki na mchekeshaji Salty Holmes wa kundi la '''Prairie Ramblers'''.[https://www.youtube.com/watch?v=6bIRTLO_yzU Lana Chapel Video: Bones]http://www.answers.com/topic/salty-holmes?cat=entertainment https://web.archive.org/web/20071113185047/http://cdbaby.com/cd/donlloydchapel https://web.archive.org/web/20070807143904/http://shs.starkville.k12.ms.us/mswm/MSWritersAndMusicians/musicians/Wynette.html Jamii:Waimbaji wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lana_Chapel
| null | 53,581
|
Ain't Nobody
|
"'''Ain't Nobody'''" ni kibao kikali cha mwaka wa 1983 ambacho kiliimbwa na kundi zima la Rufus & Chaka Khan. Kilitolewa kikiwa kama wimbo wa ziada katika albamu yao moja-kwa-moja ya bendi ''Stompin' at the Savoy''. Kibao hiki kilifikia nafasi ya kwanza katika chati za miondoko ya R&B huko nchini Marekani na kushika nafasi ya ishirini-na-mbili katika chati za ''Billboard'' Hot 100. Kibao hiki kimepata kuwa moja kati ya alama maarufu ya nyimbo za Khan. Mpiga kinanda wa Rufus David "Hawk" Wolinski ametunga kibao hiki kwa kutumia synthesizer inayojirudia yenyewe kwa mashine ya ngoma ya LinnDrum. Mtayarishaji mkongwe Quincy Jones (ambaye awali alifanyakazi na kina Rufus) alimtaka Wolinski autoe wimbo wa "Ain't Nobody" kwa Michael Jackson kwa ajili ya albamu iliyotingisha dunia, ''Thriller'', lakini kwa bahati mbaya Wolinski tayari alikuwa ameahidi kurekodi kibao hiki kwa Russ Titelman, ambaye hatimaye amekifanya kuwa kibao cha kundi kwa kuimbwa na Khan. Wimbo huu pia ulijumlishwa katika orodha ya vibwagizo vya filamu ya ''Breakin'''.[http://www.fast-rewind.com/break/findex.htm Breakin'] Jamii:Nyimbo za 1983 Jamii:Nyimbo za 1996 Jamii:Nyimbo za 1997 Jamii:Nyimbo za 2003 Jamii:Nyimbo za Chaka Khan Jamii:Nyimbo za LL Cool J
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ain't_Nobody
| null | 13,279
|
Antonio José de Sucre
|
thumb|right|Antonio José de Sucre '''Antonio José de Sucre''' (3 Februari [] - 4 Juni []) alikuwa mwanajeshi na mwanasiasa wa Amerika Kusini akipigania uhuru wa nchi mbalimbali pamoja na rafiki yake wa karibu Simon Bolivar. Alikuwa Rais wa sita wa Peru kuanzia tarehe 23 Juni hadi 17 Julai, mwaka wa []. Tena alimfuata Simon Bolivar kuwa Rais wa pili wa Bolivia kuanzia tarehe 29 Desemba [] hadi 18 Aprili []. Alijiuzulu na kuhamia mjini Quito. Aliuawa kwa kupigwa risasi aliposafiri karibu na mji wa Pasto nchini Colombia. Jamii:Marais wa Bolivia Jamii:Marais wa Peru
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Antonio_José_de_Sucre
| null | 9,001
|
Zeu
|
'''Zeu''' (pia '''Zeus''' kutoka Kigiriki: '''Ζεύς''' ''Zeus'') ni mkuu wa miungu katika dini ya Ugiriki ya Kale. Analingana na Jupiter katika dini ya Roma ya Kale. Katika imani ya Wagiriki alikalia kilele cha mlima Olimpos pamoja na miungu wenzake alkini alikuwa mkuu na mwenye nguvu kushinda wengine. Katika masimulizi ya Wagiriki alikuwa mtoto wa miungu Kronos na Rhea na mdogo wa Hestia, Demeter, Hera, Hades na Poseidon. Huyu baba-mungu Kronos alimeza watoto wake wote mara baada ya kuzaliwa akihofia ya kwamba watampindua sawa jini yeye mwenyewe aliwahi kumpindua babake mungu Uranos. Zeu alipoelekea kuzaliwa mamake Rhea alimficha pangoni akampa Kronos badale yake jiwe lililofunikwa na nguo akameza. Zeu alikua haraka akawa mkubwa na hapo alitumia mbinu wa dawa kumlazimisha baba kutapika watoto wote aliowahi kumeza. Baadaye aliungana na wakubwa zake na pamoja walimshambulia Kronos na kumshinda. Sasa miungu waliamua kugawana madaraka; Zeu alikuwa mungu mkuu wa mbinguni, Poseidon mkuu wa bahari na vilindi vyake na Hades mkuu wa dunia ya chini. Zeu alimwoa dadake Hera akazaa watoto naye lakini alitoroka mara kwa mara kufanya mapenzi na miungu wa kike wengine au na mabinti wa kibinadamu; mitholojia ya Wagiriki ilitaja zaidi ya majina 30 ya miungu au mabinti aliozaa nao. Aliheshimiwa na Wagiriki wote na kuabudiwa katika mahali pa pekee; pamoja na mahekalu kulikuwa na sehemu za misitu penye miti iliyotazamiwa kuwa miti mitakatifu yake. Kisiwani Kreta waliabudu kwenye mipango aliposemekana kufichwa na mamake. * Tinia - mungu wa kulingana na Zeu katika Mitholojia ya Kietruski. * Jupiter - mungu wa kulingana na Zeu katika Mitholojia ya Kirumi * Odin - mungu wa kulingana na Zeu katika Mitholojia ya Kinorsi. Jamii:Miungu wa Kigiriki
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Zeu
| null | 13,103
|
Amosi
|
thumb|[[Picha takatifu ya nabii Amosi, karne ya 18, monasteri ya Kizhi, Karelia, Russia).]] '''Amosi''' (kwa Kiebrania ''עָמוֹס'', Amos) ni mmojawapo kati ya manabii wa Israeli. Kitabu chake, kutokana na ufupi wake, ni kati ya vile 12 vya Manabii Wadogo. Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu. Sikukuu yake ni tarehe 15 JuniMartyrologium Romanum. Baada ya unabii wa Eliya na Elisha, Mungu aliendelea kukazania ufalme wa kaskazini kabla haujaangamizwa kabisa: tahadhari kabla ya hatari. Ndiyo sababu, ili kuthibitisha haki yake na utakatifu wake dhidi ya maovu ya Waisraeli, alimtuma huko Amosi kutoka Tekoa (ufalme wa kusini), alipokuwa mfugaji na mtunzaji wa mibuyu karibu na jangwahttps://www.santiebeati.it/dettaglio/47900. Amosi aliona maendeleo makubwa ya kaskazini chini ya mfalme Yeroboamu II, lakini hakudanganywa nayo, bali alitabiri yatakoma mapema. Aliona Waisraeli wanaoshika sabato na sikukuu, pamoja na ibada na sadaka mbalimbali, lakini wananyanyasa wenzao maskini: hapo akapiga kelele kudai kwanza haki itiririke kama maji ya mto ili ibada ziwe na maana. Hatimaye alikatazwa asiendelee kuhubiri, pia kwa sababu alikuwa mtu wa kusini, hivyo walifikiri anasema kwa kijicho tu. Habari zake zinapatikana katika Kitabu cha Amosi ndani ya Tanakh (Biblia ya Kiebrania), kwa hiyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo. Ni kwamba, tofauti na manabii Eliya na Elisha waliomtangulia wasiache maandishi, nabii Amos (786 - 746 hivi K.K.) ana kitabu chenye mafundisho yake aliyoyatoa katika ufalme wa Israeli (Kaskazini) ingawa alikuwa mtu wa ufalme wa Yuda (Kusini). Hakutarajia kutumwa na Mungu, ila ilimbidi akubali kutabiri kwa niaba yake (7:10-17), hasa kuwa Israeli itaangamizwa na kutekwa na Waashuru utumwani kwa makosa dhidi ya imani na ya haki pamoja na anasa (5-6). Waisraeli wakakataa maneno yake hata wakatendwa alivyowatabiria kwa ukali wote (2Fal 17:5-23). *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko *Anderson, Bernhard W. & Foster R. McCurley ''The Eighth Century Prophets: Amos, Hosea, Isaiah, Micah'' Wipf and Stock: 2003. ISBN 1592443540 *Rosenbaum, Stanley Ned ''Amos of Israel: A New Interpretation'' Georgia: Mercer University Press: 1990. ISBN 0865543550 *[http://ocafs.oca.org/FeastSaintsViewer.asp?SID=4&ID=1&FSID=101724 The Holy Prophet Amos] Orthodox icon and synaxarion *[http://hypertextbible.org/amos/amos/index.htm Hypertext bible commentary: Amos] Jamii:waliofariki karne ya 8 KK Category:Watu wa Biblia Jamii:Watakatifu wa Israeli Jamii:Manabii wa Agano la Kale Category:Manabii katika Uislamu
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Amosi
| null | 4,602
|
José Bernal
|
thumb|Jose Bernal Romero '''José Bernal Romero''' (8 Januari [] – 19 Aprili []) alikuwa msanii wa Kuba-Marekani, aliyezaliwa Santa Clara, Kuba, katika jimbo la zamani la Las Villas (sasa Villa Clara). Romero pia alipata kuwa raia wa Marekani kwa njia ya kawaida mwaka [].Dorothy Chaplik, "The Art of José Bernal," essay in [http://www.artnet.com/awc/jose-bernal.html artnet Monographs]. Bernal ana kazi zake za sanaa katika makusanyo kadhaa ya kudumu, ikiwemo: * ''San Antonio Museum of Art, San Antonio, Texas'' * ''Tucson Museum of Art na Historic Block, Tucson, Arizona'' * ''Asheville Art Museum, Asheville, North Carolina'' * ''Cameron Art Museum, Wilmington, North Carolina'' * ''McNay Art Museum, San Antonio, Texas'' * ''Mary and Leigh Block Museum of Art, Evanston, Illinois'' * ''The Art Institute of Chicago, Chicago, Illinois'' * ''Institute for Latino Studies/University of Notre Dame, Indiana'' * ''Art Museum of the Americas, OAS, Washington, D.C.'' * ''El Museo del Barrio, New York City'' * ''DePaul Art Museum, Chicago, Illinois'' * ''Loyola University Museum of Art, Chicago, Illinois'' * ''Museo Nacional Centro de Arte Reina Sofía, Madrid, Uhispania'' Matukio ya kurudisha macho (retrospectives) ya kazi za Bernal yamefanyika katika: * ''Cameron Art Museum'' * [https://www.askart.com/AskART/studio/studio.aspx?Studio=11139863 Bernal huko AskART] * [http://web.artprice.com/artist/434247/jose-bernal?l=en Bernal huko artprice] Jamii:wasanii wa Kuba Jamii:wasanii wa Marekani jamii:waliozaliwa 1925 jamii:waliofariki 2010 jamii:WikiMonthly Edit-a-thon Kilimanjaro
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/José_Bernal
| null | 57,547
|
Vita ya Kijerumani
|
400px|thumb|Ramani ya Ujerumani wakati wa vita ya 1866; ; ; ; '''Vita ya Kijerumani ya 1866''' (inaitwa pia '''Vita ya Austria dhidi ya Prussia''', au '''Vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Ujerumani'''; kwa Kijer.: ''Deutscher Krieg'') ilipiganwa mnamo [] kati ya Milki ya Austria kama kiongozi wa Shirikisho la Ujerumani na Ufalme wa Prussia. Prussia ilisaidiwa hasa na Italia pamoja na madola madogo ndani ya Ujerumani. Vita hiyo ilikuwa sehemu ya mwisho ya ushindani kati ya Austria na Prussia kuhusu kipaumbele katika Ujerumani kwa jumla. Tokeo lake lilikuwa ushindi wa Prussia, kuondoka kwa Austria katika siasa ya Ujerumani na ukuu wa Prussia juu ya madola mengine ya Ujerumani. Prussia ilifaulu kushinda majeshi ya Hannover na Bavaria pekepeke kabla hayajafaulu kuungana. Kwenye mapigano ya Koeniggraetz ilishinda pia jeshi kuu la Austria.[https://archive.org/details/campaigningerma00abthgoog The campaign of 1866 in Germany, by col. von Wright and capt. H.M. Hozier], uk 362 Vita ilimaliza Shirikisho la Ujerumani lililoondolewa. Prussia haikudai maeneo ya Austria lakini ilimeza madola ya Ufalme wa Hannover na temi za Hessen zilizoendelea kama mikoa ya PrussiaSchmitt, Hans A. (1975). "Prussia's Last Fling: The Annexation of Hanover, Hesse, Frankfurt, and Nassau, June 15 -October 8, 1866". Central European History. 8 (4): 316–347. doi:10.1017/S0008938900018008. S2CID 145525529. Sehemu za kaskazini za Ujerumani ziliungana katika Shirikisho la Ujerumani Kaskazini chini ya uongozi wa Prussia. Italia iliwahi kushambulia Milki ya Austria katika majimbo yake kaskazini mwa rasi ya Italia; inagawa jeshi lake halikufaulu katika mashambulio yake, baada ya vita Austria ilipaswa kukabidhi maeneo ya Venezia na Mantova kwa Ufalme wa Italia. jamii:Historia ya Ujerumani Jamii:Historia ya Austria Jamii:Historia ya Italia Jamii:1866
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita_ya_Kijerumani
| null | 44,010
|
Gabon
|
Kaimu Rais|majina_viongozi=Brice Oligui Nguema|serikali=Jamhuriyenye baraza la majeshi|fedha=Faranga ya CFA|majira_saa=+1(Afrika ya Magharibi)|tld=.ga|msimbo_simu=241|iso3166=GA|eneo_jumla=267 668|watu_kadirio=2 397 368|mwaka_kadirio=2023|pato= USD bilioni 19.319|mwaka_pato=2023|pato_kwa_mtu= USD 8 831|pato_halisi= USD bilioni 41.922|pato_halisi_kwa_mtu= USD 19 165|maendeleo= 0.706 - |mwaka_maendeleo=2021|ukubwa_bendera=120|ukubwa_nembo=90}} '''Gabon''', rasmi '''Jamhuri ya Gabon''' (Kifaransa: République gabonaise), ni nchi iliyo kwenye pwani ya Atlantiki ya Afrika ya Kati, kwenye ikweta, iliyopakana na Guinea ya Ikweta kaskazini-magharibi, Kamerun kaskazini, kusini Jamhuri ya Kongo, na Jamhuri ya Guinea-magharibi. Ina eneo la kilomita za mraba 270,000 (100,000 sq mi) na idadi ya watu milioni 2.3. Libreville ndio mji mkuu wa nchi na jiji kubwa zaidi. Nchi hii ina umma mdogo, madini na mali kwa wingi, na wafanyabiashara kutoka nchi za kigeni wameweza kufanya Gabon iwe nchi yenye maendeleo makubwa. Gabon imegawiwa katika mikoa 9 nayo ina jumla ya wilaya (''départements'') 37. Mikoa ni: *Estuaire, *Haut-Ogooué, *Moyen-Ogooué, *Ngounié, *Nyanga, *Ogooué-Ivindo, *Ogooué-Lolo, *Ogooué-Maritime, na *Woleu-Ntem. thumb|kushoto|Aliyekuwa Rais [[Omar Bongo Ondimba wa Gabon (kushoto) akiwa Washington, USA.]] Jamhuri ya Gabon, tangu kupata uhuru kutoka Ufaransa tarehe 17 Agosti [], imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa [] hadi kifo chake ([]: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali aliyepinduliwa na wanajeshi tarehe 30 Agosti []. thumb|Nyumba ya baraza, [[Libreville]] Mwaka wa [] Gabon ilianza demokrasia ya vyama vingi na katiba ya kidemokrasia ili ruhusu ukweli wa uchaguzi na uwajibikaji wa idara za serikali, lakini hali iliendelea kuwa karibu ileile. Gabon ni nchi yenye neema sana kuliko nchi jirani. Uchumi wake, hasa chumo cha umma, ni mara nne ya nchi za Afrika kusini kwa Sahara. Hii hasa ni kwa sababu ya uzalishaji wa mafuta ambao umeleta utajiri na mali, lakini usambazaji wa mali hii ya mafuta bado umedhoofika. Gabon ilikuwa mwanachama wa Muungano wa Nchi Zinazouza Mafuta (OPEC) kutoka mwaka wa 1975 mbaka 1995. Mwaka 1990, udhaifu wa pesa CFA frank uliacha Gabon katika shida ya kulipa deni za kimataifa; Ufaransa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) wameipa Gabon mkopo na usaidizi kwa uelewano kwamba Gabon itageuza uchumi wake barabara. Yasemekana mambo ya mazingira yalifanya umma wa Gabon kutopanda kwa sensa kati ya miaka [] na []. Ni nchi ambayo ina umma mdogo zaidi katika Afrika bara, na upungufu wa wafanyakazi ni mojawapo ya mambo yanayofanya hasa uchumi kutovuma zaidi. Umma hasa kwa ujumla ni kama watu milioni 2.4. Gabon hasa ina makabila zaidi ya 40 ambayo yana utamaduni na lugha tofauti lakini karibu wote (95%) ni wa jamii ya Bantu. Wafang ndio kabila kubwa zaidi nchini Gabon, wengine ni Wamyene, Wabandjabi, Waeshira, Wabapounou na Waokande. Lugha ya Kifaransa ndiyo lugha rasmi ya taifa ambayo hutumika kwa mawasiliano (wakazi wanaoimudu ni 80%). Wafaransa 10,000 wanaishi Gabon, na Ufaransa unaathiri mambo ya kigeni, utamaduni na biashara nchini Gabon. Upande wa dini, imekadiriwa kwamba 75.6% za wakazi ni Wakristo (hasa Wakatoliki), 12.2% ni Waislamu (hasa wageni), na 5.7% wanafuata dini asilia za Kiafrika (Bwiti). * Makabila ya Gabon * Muziki wa Gabon * Orodha ya lugha za Gabon * Mawasiliano nchini Gabon * Mambo ya kigeni ya Gabon * Orodha ya kampuni za Gabon * Jeshi la Gabon * Historia ya Gabon * Uchukuzi nchini Gabon * Orodha ya nchi kufuatana na wakazi * Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu * Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu * Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa * Demografia ya Afrika * David E. Gardinier, ''Kamusi ya Historia ya Gabon'', tolezi ya 2. (The Scarecrow Press, Inc., 1994) – kazi inayohusu maelezo biografia ya vifaa 1,453 * James F. Barnes, ''Gabon: Beyond the Colonial Legacy'' (Boulder: Westview, 1992) * [http://www.legabon.org Le Gabon : makala rasmi ya Jamhuri ya Gabon] * [http://www.assemblee.ga/ Assemblée nationale du Gabon] makala rasmi. * [http://gabon.embassyhomepage.com/ Gabonese Embassy in London] arithio za serikali * [http://www.senat.ga/ Le Sénat de la République Gabonaise] makala rasmi (kwa kifaransa) * [http://allafrica.com/gabon/ AllAfrica.com - ''Gabon''] viungo via taarifa ya habari * [http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/africa/country_profiles/1023203.stm BBC News Country Profile - ''Gabon''] * [http://www.cia.gov/cia/publications/factbook/geos/gb.html Kitabu cha wa dadisi wa Amerika - ''Gabon''] * [http://www.pygmies.info/ Baka watu wafupi wa Kamerun na Gabon] Utamaduni na wakazi wa kwanza Gabon * [http://dmoz.org/Regional/Africa/Gabon/ Open Directory Project - ''Gabon''] maelekezo * [http://www-sul.stanford.edu/depts/ssrg/africa/gabon.html Chuo kikuu cha Stanford – Afrika kusini mwa sahara: ''Gabon''] maelekezo * [http://www.sas.upenn.edu/African_Studies/Country_Specific/Gabon.html Chuo kikuu cha Pennsylvania – Ustadi wa-Afrika: ''Gabon''] maelekezo * [http://dir.yahoo.com/Regional/Countries/Gabon/ Yahoo! - ''Gabon''] directory category Jamii:Nchi za Afrika Jamii:Umoja wa Afrika Jamii:Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa Jamii:jumuiya ya Madola
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gabon
| null | 363
|
Carlos Rivas
|
'''Carlos Adan Rivas Godoy''' (alizaliwa Septemba 3, []) ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu kutoka Kanada aliyekuwa akicheza kama kiungo katika Ligi ya Chilean Primera División, Ligi ya Primera B de Chile na Ligi ya soka ya Kanada.[http://gotorontofc.com/index.php?name=PNphpBB2&file=viewtopic&p=38592 Canucks Abroad - Carlos Rivas Jr.] Jamii:Wachezaji mpira wa Kanada
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Carlos_Rivas
| null | 53,474
|
Kostabile
|
thumb|250px|[[Muujiza wa Mt. Kostabile.]] '''Kostabile, O.S.B.''' (Castellabate, Salerno, [] hivi - Cava de' Tirreni, Salerno, 17 Februari []) alijiunga na monasteri maarufu tangu utotoni akawa abati wake kuanzia mwaka [] hadi kifo chake. Aliishi na kuongoza kwa upole na upendo wa ajabu hata akaitwa "blanketi" la ndugu. Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu. Heshima hiyo ilithibitishwa na Papa Leo XIII tarehe 21 Desemba []. Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 17 FebruariMartyrologium Romanum. *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko * [http://www.santiebeati.it/dettaglio/91125 San Constabile (Costabile)] *[https://web.archive.org/web/20070224053421/http://www.catholic-forum.com/SAINTS/saintc2f.htm Constabilis of Cava] *[https://web.archive.org/web/20120212232210/http://www.saintpatrickdc.org/ss/0217.shtml Constabilis of Cava] Jamii:Waliozaliwa 1070 Jamii:Waliofariki 1124 Jamii:Wamonaki Jamii:Wabenedikto Jamii:Mapadri Jamii:Watakatifu wa Italia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kostabile
| null | 42,403
|
Ziwa Qinghai
|
|type=Ziwa la chumvi |inflow=|outflow=|catchment=|basin_countries=|length=|width= |area=km2 4186 (2004)km2 4489(2007)|depth=|max-depth= m 32.8|volume=|residence_time=|shore= |elevation=m 3260 |islands=Sand Island, Bird Islands|cities=Haiyan County|reference=}} '''Ziwa Qinghai''' ni ziwa kubwa zaidi nchini China. Iko katika Mkoa wa Qinghai uliopata jina lake kutoka kwa ziwa hili. Ziwa Qinghai ni ziwa la chumvi la magadi. "Qinghai" inamaanisha ziwa buluu. Ziwa hilo huwa na majina mbalimbali katika lugha za Kimongolia na Kitibeti yanayomaanisha "Ziwa la Buluu". Ziwa Qinghai liko karibu km 100 magharibi mwa Xining katika nyanda za juu za Tibet kwenye mita 3205 juu ya usawa wa bahari. Buffetrille 1994, p. 2; Gruschke 2001, pp. 90 ff. Lipo kati ya wilaya za Haibei na Hainan za Tibet kaskazini mashariki mwa jimbo la Qinghai katika kaskazini magharibi ya China. Eneo la ziwa limeonekana kubadilika; limepungua wakati wa karne ya 20 lakini limeongezeka tangu []. Mnamo mwaka [] ziwa lilikuwa na eneo la km2 4217. Kina cha wastani ni m 21. Mito 23 huingia ndani ya Ziwa Qinghai lakini hakuna njia ya maji kutoka, isipokuwa kwa uvukizaji. Kwa njia hiyo ziwa limezidi kuwa ziwa la chumvi lenye magadi mengi. Kwa sasa ziwa huwa na asilimia 14 za chumvi. Uso wa mji huganda na kuwa barafu wakati wa majira ya baridi. * |date=2001}}. * }}. * . * . * . * . * . * . * . * . * . * . * . * . * |date=2015|contribution-url=http://www.nature.com/articles/srep09780|contribution=Article 9780: ''Gymnocypris przewalskii'' (''Cyprinidae'') on the Tibetan Plateau|title=Scientific Reports|volume=Vol. 5}}. * }}. jamii:Maziwa ya China
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ziwa_Qinghai
| null | 29,697
|
Kasha Kropinski
|
thumb|Kasha Kropinski '''Kasha Kropinski''' (amezaliwa '''Katarzynka Kropiński''' mnamo 27 Agosti []) ni mwigizaji wa filamu na televisheni aliyezaliwa Afrika Kusini. Kasha alizaliwa Afrika Kusini, binti ya Jacek Kropiński na Debbie Cochrane. Jacek ni msanii wa filamu na Debbie > ni mwanamitindo wa zamani wa kimataifa. Kasha alianza akiwa na umri wa miaka 6, akicheza majukumu ya kuongoza jukwaani na kikundi cha ukumbi wa michezo cha Cape Town, Stagecraft. Majukumu yake ni pamoja na Christopher Robin, Peter Rabbit, Noddy, Mowgli, Frankie Fox katika Mbwa Mbwa wa ajabu, akipata sifa kubwa kutoka kwa wakosoaji wa ukumbi wa michezo. Kwa wakati huu, Kasha pia alipata sifa katika mitihani yake ya Uigizaji wa Chuo cha Utatu cha London. Wakati huo huo, Kasha pia aliigiza katika Ballet Eisteddfods na akapata tuzo 5 za medali za dhahabu. Alipokuwa na umri wa miaka 9, Kasha na wazazi wake walihamia Los Angeles ambapo alianza kufanya majukumu ya wageni kwenye Runinga: Angel, Bila ya Kufuatilia, Jimbo la Neema, Kuvuka Jordan, ER, The Shield, Uchafu, na Zoey 101. Yeye pia alifanya ADR (Uingizwaji wa Mazungumzo ya Maongezi, au Kurekodi Mazungumzo ya Ziada: aina ya utaftaji wa sauti) fanya kazi kwa Samaki Kubwa, Wawindaji, Kijiji na Bibi Harris. Alionesha mtoto wa mbwa Penny katika Disney's 101 Dalmatians II: Patch's London Adventure na Miss Holly katika Maandalizi ya Likizo ya Disney na Kutua. Pia aliendelea na majukumu yake ya ballet na kucheza katika uzalishaji wa 2003 na 2004 wa ballets za Nutcracker. Baada ya kuhitimu kutoka Shule ya Msingi ya Carpenter Avenue huko Studio City, alipokea Tuzo ya Rais ya Ustawi Bora wa Kielimu. Kwa sababu ya ratiba yake ya ballet na kaimu, aliendelea kusoma kupitia programu ya shule ya nyumbani ambapo alipewa kujiunga na Jumuiya ya Heshima ya Kitaifa. Katika umri wa miaka 11, Kasha alichaguliwa kuchukua jukumu la kuongoza katika muziki uliopendekezwa wa Andrew Lippa, Princess mdogo, na akashiriki katika uwasilishaji wa Broadway kwa wawekezaji huko New York. Aliporudi Los Angeles, alirushwa kwenye filamu ya Afrika Kusini ya ''The Story of a African Farm (iliyotolewa nchini Merika kama Bustin 'Bonaparte: The Story of a African Farm'', kama mmoja wa wahusika wakuu Lyndall , akicheza kinyume na Richard E. Grant na Armin Mueller-Stahl. Sinema hii ilitokana na kazi ya kawaida ya fasihi na Olive Schreiner na kuigizwa katika jangwa dogo la Karoo nje ya Cape Town, Afrika Kusini. Kasha amehudhuria shule ya majira ya joto ya Royal Ballet huko England, shule ya majira ya joto ya San Francisco Ballet na alikuwa wa mwisho katika Kesho ya Stars ambayo inaonyesha wasanii bora zaidi wa watu wazima kutoka Kusini mwa California katika muziki, densi na sauti. Alionekana katika umaarufu wa sinema ya 2009 katika jukumu la Ballerina. Katika msimu wa joto wa 2009, Kasha alihudhuria LAMDA (London Academy of Music and Dramatic Art) shule ya majira ya joto huko London, England, na aliporudi Los Angeles, alicheza majukumu mawili kwenye Cinderella ya ballet. Mnamo mwaka wa 2011 Kasha alitupwa kama Ruth Cole katika safu ya Televisheni ya AMC ya Hell on Wheels, onyesho kuhusu jamii ambayo ilifanya kazi katika kambi ya rununu iliyofuatia Reli ya Kwanza ya Transcontinental kote Amerika. Alionekana katika misimu ya kwanza hadi minne * ''MacGyver (2016 TV series)'' - Katarina Wagner (Episode 5: Toothpick) * ''Underwater Upside Down'' (2016) - Grace Conway * ''The Librarians'' TNT - Guest Star - Lucy Lyons * ''Hell on Wheels'' - Ruth (Series Regular) * ''Prep and Landing'' - Miss Holly * ''Fame'' - Ballerina * ''Dirt'' "Dirty, Slutty Whores" - Reagan * ''Zoey 101'' "Trading Places" - Tabitha * ''ER'' "White Guy, Dark Hair" - Mia * ''Crossing Jordan'' "Fire in the Sky" - Kimmy Moran * ''Oliver Beene'' "Oliver & the Otters" - Voice * ''The Story of an African Farm'' - Lyndall * ''Without a Trace'' "Wannabe" - Lisa Potter * ''The Shield'' "Carte Blanche" - Patty Ann Hinkle * ''101 Dalmatians II: Patch's London Adventure'' - (voice) Penny * ''State of Grace'' "A Taste of Money" - Annette Wheeler * ''Phantom Investigators'' "Were-Dog" - Melanie * ''Angel'' "Lullaby" & "Quickening" - Sarah Holtz * ''Mrs. Harris'' (ADR artist) * ''The Village'' (ADR artist) * ''Big Fish'' (ADR artist) * ''The Cat in the Hat'' (ADR artist) Jamii:Waigizaji filamu wa Afrika Kusini Jamii:Editathon 2021-06 Morogor
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kasha_Kropinski
| null | 36,215
|
Dahlia Duhaney
|
'''Dahlia Duhaney''' (alizaliwa 20 Julai []) ni mwanariadha mstaafu wa Jamaika ambaye alishindania nchi yake ya asili katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya joto ya mwaka [] huko Barcelona, Hispania. Alishinda taji la dunia katika mbio za kupokezana za wanawake za 4 × 100 m katika Mashindano ya Dunia ya IAAF mwaka [] huko Tokyo, Japani, pamoja na Juliet Cuthbert, Beverly McDonald na Merlene Ottey. Duhaney alikimbia kwa pamoja katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Louisiana. Jamii:Wanariadha wa Jamaika Jamii:Watu walio hai Jamii:Waliozaliwa 1970
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Dahlia_Duhaney
| null | 50,479
|
Dionysios Mantalos
|
'''Dionysios Mantalos''' (kwa Kigiriki: Διονύσιος Μάνταλος; 29 Oktoba [] – 7 Agosti []) alikuwa Askofu Mkuu wa Korintho. Aliteuliwa kuwa askofu wa Korintho mwaka [] akahudumu hadi alipofariki mwaka 2025. Alisomea masomo ya dini katika Shule ya Theolojia ya Athens. Mantalos alipewa daraja ya ushemasi mwaka [] na daraja ya upadri mwaka []. Alikuwa mchungaji ([]), kamishina ([]) na kansela ([]) wa Metropolis Mtakatifu wa Chalkis. Pia alihudumu kama naibu mkurugenzi wa Apostolic Diakonia ([]) na kansela wa Baraza la Kanisa la Kiorthodoksi la Ugiriki (2006). Huko Chalkis, Mantalos alihusika na masuala ya vijana na Shule za Jumapili, na alichangia kuanzishwa kwa vituo 25 vya utamaduni na kambi katika maeneo ya Ilia na Euboea. Pia alikuwa mkurugenzi wa shule ya Metropolis ya Chalkis na alifundisha masomo ya dini kwa mafunzo ya wafanyakazi. Vita vyake dhidi ya madawa ya kulevya vilikuwa na umuhimu mkubwa, ambapo alikuwa mwenyekiti wa bodi ya "Kituo cha Kuzuia Madawa ya Kulevya" cha Euboea. Alipewa daraja ya askofu wa Korintho tarehe 15 Oktoba [], aliendelea na kazi yake kwa kutilia mkazo masuala ya vijana. Alichapisha vitabu vingi na kutoa mihadhara, hotuba na mahojiano mengi katika vyombo vya habari. Mantalos alifariki dunia baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu. [https://orthodoxia.info/news/efyge-tin-zoi-o-mitropolitis-korin/ Έφυγε από την ζωή ο μητροπολίτης Κορίνθου Διονύσιος] Jamii:Waliozaliwa 1952 Jamii:Waliofariki 2025 Jamii:Maaskofu Jamii:Watu wa Ugiriki
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Dionysios_Mantalos
| null | 57,505
|
Jennifer Riria
|
'''Jennifer Riria''' ni mfanyabiashara, mtendaji wa shirika, muhudumu wa benki na msomi wa Kenya ambaye anahudumu kama Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa '''Kenya Women Holding Group''' ambayo ni taasisi ndogo ya fedha na bima inayohudumia karibu wanawake milioni moja wa Kenya wengi wao wakiwa vijijini.https://www.lionessesofafrica.com/blog/2015/1/11/dr-jennifer-riria-the-start-up-story-of-a-inspiring-entrepreneur-who-has-transformed-the-lives-of-hundreds-of-thousands-of-kenyan-womenhttps://nation.africa/lifestyle/mynetwork/Jennifer-Riria-Kenya-Women-Holding-CEO/3141096-4268122-mafojaz/index.htmlhttps://www.businessdailyafrica.com/news/Kenya-Women-Holding-empower-women-2022-elections/539546-4326312-132nguqz/index.html Jamii:Watu walio hai Jamii:wanawake wa Kenya
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jennifer_Riria
| null | 58,040
|
Zakayo wa Yerusalemu
|
thumb|[[Ramani ya Yerusalemu iliyotengenezwa kama mozaiki huko Madaba.]] '''Zakayo wa Yerusalemu''' (alifariki []/[]) kwa asili alikuwa Myahudi''Historia Ecclesiastica'', V, 12." akawa askofu wa nne wa Yerusalemu kuanzia mwaka [] hadi kifo chakehttp://www.santiebeati.it/dettaglio/92425. Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu[http://www.catholic.org/saints/saint.php?saint_id=2068 Catholic Online]. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 23 Agosti''Martyrologium Romanum'', 2004. *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko Jamii:Waliozaliwa karne ya 1 Category:Waliofariki 116 Category:Maaskofu Wakatoliki Category:Watakatifu wa Israeli
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Zakayo_wa_Yerusalemu
| null | 33,221
|
Senofonte, Maria na wanao
|
'''Senofonte, Maria na wanao''' Yohane na Arkadi (walifariki karne ya 6) walikuwa Wakristo wa Konstantinopoli ambao, kisha kujinyima hadhi ya kiseneta na mali nyingi, walishika maisha ya umonaki mjini Yerusalemuhttp://www.santiebeati.it/dettaglio/38720Great Synaxaristes: ''[http://www.synaxarion.gr/gr/sid/1899/sxsaintinfo.aspx Ὁ Ὅσιος Ξενοφῶν μετὰ τῆς συμβίου του Μαρίας καὶ τῶν τέκνων Ἀρκαδίου καὶ Ἰωάννου].'' 26 Ιανουαρίου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.''[http://oca.org/saints/lives/2013/01/26/100314-venerable-xenophon-of-constantinople Venerable Xenophon of Constantinople].'' OCA - Lives of the Saints. Συναξαριστής. ''[http://www.ecclesia.gr/greek/synaxaire/synaxari.asp?minas=1&id=146 26 Ιανουαρίου] .'' ECCLESIA.GR. (H ΕΚΚΛΗΣΙΑ ΤΗΣ ΕΛΛΑΔΟΣ). Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu. Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 26 JanuariMartyrologium Romanum. *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko Jamii:Waliofariki karne ya 6 Jamii:Wamonaki Jamii:Watakatifu wa Uturuki Jamii:Watakatifu wa Palestina
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Senofonte,_Maria_na_wanao
| null | 42,096
|
Chris Marshall
|
'''Chris Marshall''' (pia anajulikana kama '''Chris Marsh''' na '''Izes''', jina la kweli: '''Adrian Marshall''') ni mwimbaji wa reggae na dancehall, mtayarishaji na mwandishi wa nyimbo kutoka Jamaika. Anajulikana zaidi kwa kuandika pamoja nyimbo ya ''Temperature'' ya Sean Paul ambayo ilikua wimbo wa nambari moja kwenye ''Billboard Hot 100'' mwaka 2006 na pia kuonekana kwenye albamu ya Anitta ya ''Kisses'' kwenye wimbo - Tu Y Yo.https://www.youtube.com/watch?v=dW2MmuA1nI4 | Sean Paul - Temperature Jamii:Waimbaji wa Jamaika Jamii:Waliozaliwa 1982
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chris_Marshall
| null | 49,130
|
Jack Lerole
|
'''Aaron "Big Voice Jack" Lerole''' (c. [] - 12 Machi []) alikuwa mwimbaji na mpiga filimbi wa penny wa nchini Afrika Kusini. Lerole alikuwa mwimbaji mkuu katika muziki wa kwela wa [] Kusini Afrika. Lerole alikuwa kiongozi wa bendi ya Elias na Zig-Zag Jive Flutes yake, ambaye alikuwa na rekodi ya kimataifa mnamo 1958 na "Tom Hark". Alianzisha bendi ya mseto ya Mango Groove mwaka [], na baadaye akashirikiana na Dave Matthews Band, bendi ya roki kutoka Marekani. Jamii:Waliofariki 2003 Jamii:Waliozaliwa 1940 Jamii:Wanamuziki wa Afrika Kusini Jamii:Arusha Editathon Muziki
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jack_Lerole
| null | 39,884
|
George Mason
|
'''George Mason''' ni jina la uhusika wa kipindi cha televisheni cha Kimarekani maarufu kama ''24''. Uhusika ulichezwa na Xander Berkley. Yeye ni Mkurugenzi wa pili wa CTU. Kazi kubwa ilikuwa katika mambo ya utawala, lakini atekwa na Jack Bauer. Mason ndiye anayehusika kwa kukamatwa kwa Bauer na kugundua mwili wa Alan York. Mason ndiye anayehusika kwa kuongoza msako wa kuiokoa familia ya Bauer na kuzuia njama nzima dhidi ya David Palmer. Mason pia anahusika kwa kukamatwa kwa Nina Myers. Katika msimu wa 2, Mason dhahiri anajaribu kukimbia katika eneo ambalo linasemekana litafanyiwa uvamizi wa kigaidi, lakini akiwa njiani akapata simu iliyokuwa ikizungumzia kwamba kuna sehemu wanaunganisha mabomu ya nyuklia. Wakati wa mapigano ya risasi, Mason akapiga sehemu iliyokuwa imefunikwa sumu ya hewa. Hivyo ilimwathiri na akaambiwa atakufa baada ya siku moja toka alipopewa dawa za kupunguza makali. Mason baadaye akaoneka kujitolea mhanga maisha yake kwa kulibeba bomu la nyuklia na kwenda kulipuka nalo kwenye jangwa. Mason pia alikuwa mshabiki wa Jimi Hendrix. Jamii:Wahusika wa 24
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/George_Mason
| null | 7,778
|
Medamud
|
thumb|Hekalu la Montu Medamud (kutoka Madu ya Misri ya Kale) ilikuwa makazi katika Misri ya kale. Eneo lake la siku hizi liko karibu kilomita 8 mashariki-kaskazini kutoka Luxor. Hekalu la Montu lilichimbuliwa na Fernand Bisson de la Roque mwaka wa [], ambaye alitambua miundo kadhaa iliyowekwa wakfu kwa mungu-vita anayejulikana kama Montu. Hekalu sahili la Montu lilikuwepo hapa tayari kuelekea mwisho wa Ufalme wa Kale, au wakati wa Kipindi cha Kwanza cha Kati. Ilikuwa imezungukwa na ukuta. Sasa iko chini ya hekalu la sasa. Kulikuwa na pylon mbili, moja nyuma ya nyingine na, zaidi ya hizo, kulikuwa na pango lenye vyumba viwili, ambavyo vyumba vyake vya chini ya ardhi viliwekwa alama ya vilima juu ya uso. Milima hii ya ardhi labda ilifanya kazi kama malima ya kwanza. Wakati wa Ufalme wa Kati Enzi ya 12, hekalu la zamani lilijengwa upya kabisa kwa kiwango kikubwa zaidi. Ujenzi na ukarabati zaidi uliendelea hadi wakati wa Milki ya Kirumi. Jamii:Africa Wiki Challenge Arusha 2022 Jamii:Utalii wa Misri
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Medamud
| null | 41,452
|
Durham, North Carolina
|
thumbnail|right|200px|Mji wa Durham, North Carolina '''Durham''' ni mji wa Marekani katika jimbo la North Carolina. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2008, mji una wakazi wapatao 223,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 123 kutoka juu ya usawa wa bahari. * Chuo Kikuu cha Duke Jamii:Miji ya Marekani Jamii:North Carolina
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Durham,_North_Carolina
| null | 9,189
|
Okyeame Kwame
|
alt=Okyeame Kwame|thumb|Okyeame Kwame '''Kwame Nsiah-Apau''' (alizaliwa 17 Aprili []), ,pia anajulikana kwa jina la kisanii kama ''Okyeame Kwame'' na jina la utani la Rap Doctor, ni mwanamuziki wa Ghana, mtunzi wa nyimbo, mkurugenzi mbunifu na mjasiriamali . Jamii:Waliozaliwa 1976 Jamii:Watu walio hai Jamii:Wanamuziki wa Ghana Jamii:Arusha Editathon Muziki Jamii:1lib1ref 2023
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Okyeame_Kwame
| null | 40,720
|
Wilaya ya Luweero
|
|subdivision_type2 = mji mkuu |subdivision_name2 = Luweero |leader_title = |leader_name = |established_title = |established_date = |area_magnitude = |area_total_km2 = |area_land_km2 = |area_water_km2 = |idadi_ya_wakazi_kwa_mwaka_wa = 2010 Makadirio |population_note = |wakazi_kwa_ujumla = 433100 |latd=00|latm=50 |lats=|latNS=N |longd=32|longm=30 |longs=|longEW=E |elevation_m = |blank_name = |blank_info = |website = http://www.luweero.go.ug |footnotes = }} '''Wilaya ya Luweero''' ni wilaya moja ya Mkoa wa Kati, Uganda. Idadi ya wakazi wake ni takriban 433,100. * Orodha ya mito ya wilaya ya Luweero Jamii:Wilaya ya Luweero Jamii:Wilaya za Mkoa wa Kati (Uganda) Jamii:Wilaya za Uganda
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wilaya_ya_Luweero
| null | 12,131
|
David Applegate
|
'''David L. Applegate''' ni mwanasayansi wa kompyuta wa Marekani anayejulikana kwa utafiti wake juu ya tatizo la wauzaji wanaosafiri. ''Applegate'' alihitimu kutoka Chuo Kikuu cha ''Dayton'' mwaka wa [], na kumaliza udaktari wake mwaka wa [] kutoka Chuo Kikuu cha ''Carnegie Mellon'', na tasnifu kuhusu ukadiriaji wa ujazo wa mbonyeo uliosimamiwa na ''Ravindran Kannan''. Applegate alifanya kazi katika kitivo katika Chuo Kikuu cha ''Rice'' na AT&T Labs kabla ya kujiunga na Google katika Jiji la New York mnamo 2016. Kazi yake kwenye ''Concorde TSP Solver'', iliyofafanuliwa katika karatasi ya 1998, ilishinda Tuzo ya ''Beale-Orchard-Hays'' ya Jumuiya ya Uboreshaji wa Hisabati, [ICM] na kitabu chake The travelling salesman problem na waandishi hao hao ilishinda Frederick W. Lanchester Tuzo mwaka wa [].[TSP] Yeye na Edith Cohen walishinda Tuzo la IEEE Communications Society's William R. Bennett kwa karatasi ya utafiti ya 2006 kuhusu uelekezaji wa mtandao.[ToN] Nyingine ya karatasi zake, kuhusu hesabu bila kubeba, alishinda tuzo ya George Pólya ya 2013.[CMJ] Mnamo [], alitajwa kuwa Mshirika wa AT&T. Akiwa na Guy Jacobsen na ''Daniel Sleator'', Applegate alikuwa wa kwanza kufanya uchanganuzi wa mchezo wa penseli na karatasi, Sprouts kwa njia ya kompyuta. Jamii:Waliozaliwa 1958 Jamii:mabingwa wa kompyuta wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/David_Applegate
| null | 42,821
|
Makabila ya Madeira
|
Makabila ya Madeira, visiwa vya Ureno vilivyoko Bahari ya Atlantiki, yanawakilisha mchanganyiko wa tamaduni za Ulaya, Afrika, na Amerika kutokana na historia ya uhamiaji, biashara ya baharini, na ukoloni. Jamii kuu ni: * Wareno wa Madeira – jamii ya wenyeji wa asili ya Ureno, huzungumza Kireno cha Madeira, wanajulikana kwa tamaduni za Katoliki, sherehe za Festa da Flor, na muziki wa Bailinho da Madeira. * Wamestizo wa Atlantiki – jamii ya mchanganyiko wa Kiafrika, Ulaya, na Amerika ya Kusini, hasa kutoka Brazil, Cape Verde, na Venezuela, wanajulikana kwa tamaduni za mijini, lugha ya Kireno, na sherehe za kitamaduni. * Wakape Verde wa Madeira – jamii ya wahamiaji kutoka Cape Verde, huzungumza Kireno na Kikrioli, wanajulikana kwa muziki wa Morna, tamaduni za kifamilia, na mchango wao katika sekta ya ujenzi na huduma. * Wahindi wa Madeira – jamii ndogo ya wafanyabiashara wa asili ya Uhindi, hasa Goa, wanajulikana kwa tamaduni za Hindu na Katoliki, na biashara ya rejareja. * Wahamiaji wa kisasa – jamii kutoka Ujerumani, Uingereza, Afrika Magharibi, na Amerika ya Kusini, wanachangia katika utofauti wa lugha, dini, na tamaduni za kisasa. Lugha rasmi ni Kireno, lakini lahaja ya Madeira inaathiriwa na Kispanishi, Kikrioli, na Kiingereza. Tamaduni za visiwa hujumuisha vyakula vya baharini kama espetada, sherehe za kitamaduni, na urithi wa kihistoria wa meli za karne ya 15. Jamii:Makabila ya Ulaya Jamii:Makabila ya Madeira Jamii:Afrocrowd 2025
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Makabila_ya_Madeira
| null | 57,418
|
Laurenti wa Brindisi
|
200px|thumb|Laurenti wa Brindisi, "mwalimu wa kitume". '''Laurenti wa Brindisi''' ni jina la kitawa la '''Giulio Cesare Russo''' (Brindisi, leo nchini Italia, 22 Julai [] - Belém, Ureno, 22 Julai []), padri na mkuu wa shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini miaka []-[]. Alitoa huduma ya kuhubiri katika sehemu mbalimbali za Ulaya asikubali kuchoka; alitekeleza majukumu yake yote kwa usahili na unyenyekevu, yawe ya kulihami Kanisa dhidi ya wavamizi Waislamu, ama ya kupatanisha watawala waliopigana vita ama katika kuongoza shirika lakehttps://www.santiebeati.it/dettaglio/28350. Alitangazwa mwenye heri na Papa Pius VI mwaka [], mtakatifu na Papa Leo XIII mwaka [], hatimaye mwalimu wa Kanisa na Papa Yohane XXIII mwaka []. Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 22 JulaiMartyrologium Romanum. Laurenti alizaliwa Brindisi, Italia, tarehe 22 Julai 1559. Baada ya kufiwa baba yake utotoni, alipokuwa na miaka 7 tu, mama alimtuma aishi utawani, hivyo alisoma kwenye shule ya Wafransisko Wakonventuali hukohuko Brindisi, akavaa kanzu yao tangu mwaka [] hadi [] kama maandalizi ya kujiunga nao. Tangu hapo alivutiwa na karama ya Fransisko wa Asizi, hata akavaa kanzu yao tangu mwaka [] hadi [] kama maandalizi ya kujiunga nao. Wakati huo ndipo alipoanza kuhubiri, kadiri ya desturi yao. Kisha kupatwa na hali ngumu kiuchumi katika familia, alihamia kwa ndugu yake padri huko Venezia alipoendelea kusoma na kuzingatia wito wa Kifransisko hadi kujiunga na urekebisho wa Wakapuchini tarehe 18 Februari [] kwa kuvaa kanzu yao na kubadilishiwa jina. Wakati huo shirika hilo lilikuwa limekomaa, anavyoonyesha mwenyewe ambaye ni tunda lake kamili zaidi pande nyingi. Huko Padova aliendelea kusoma mantiki na falsafa, halafu akarudi Venezia kusomea teolojia. Kwa wakati huohuo alikuwa anafundisha pia, kutokana na ujuzi wake mkubwa ajabu, hasa wa Biblia katika lugha zote asili, uliomsaidia hata kuhubiria kwa mafanikio Wayahudi. Kuhusu umuhimu wa Neno la Mungu alisema, "Neno la Bwana ni mwanga wa akili na moto wa utashi, hivi kwamba binadamu aweze kumjua na kumpenda Mungu. Kwa mtu wa ndani, anayeishi kwa neema hai ya Roho wa Mungu, ni mkate na maji, lakini mkate mtamu kuliko asali na maji yanayopendeza kuliko divai au maziwa… Ni silaha dhidi ya moyo ulioshupaa katika vilema. Ni upanga dhidi ya mwili, ulimwengu na shetani ili kuangamiza kila dhambi". Tarehe 18 Desemba [] alipata upadrisho akaendelea kutumia utaalamu wake kwa ajili ya Urekebisho wa Kikatoliki baada ya Mtaguso wa Trento. Kwa kuwa alijua lugha mbalimbali, kama vile Kifaransa na Kijerumani, aliweza kufanya utume mpana sana akahubiri katika nchi nyingi za Ulaya. Kwa ujuzi wake wa Biblia na mababu wa Kanisa aliweza kufafanua kwa utulivu na uwazi mafundisho ya Kikatoliki kwa Waprotestanti hasa wa Ujerumani, akionyesha misingi ya yale yaliyopingwa na Martin Luther, kama vile nafasi ya kwanza ya Mtume Petro na ya askofu wa Roma kati ya wenzao, asili ya uaskofu, utakaso wa dhati wa binadamu na haja ya kutenda mema ili kuokoka milele. Hata waamini wa kawaida, wasio na elimu kubwa, walifaidika na maneno yake alipowaelekea ili kuwahimiza washike imani yao kimaisha. Ni ajabu alivyofululiza kuhubiri katika miji mingi ya Italia na ya nchi nyingine hata alipotwishwa majukumu mengine mazito, kama vile mwalimu wa teolojia na mlezi wa wanovisi. Mwaka [] alianza kupata vyeo vikubwa shirikani, kama vile mkuu wa kanda na mshauri wa mkuu wa shirika. Pamoja na hayo, alitumwa Ujerumani kuongoza wanashirika wanaokwenda kuishi na kufanya utume huko. Mnamo Oktoba [] aliomba kuwa mmojawapo wa mapadri wa kuhudumia kiroho wanajeshi wa Kikristo wakipambana na Waturuki wavamizi. Tarehe 24 Mei [] alichaguliwa kuwa mkuu wa shirika, mwenye jukumu la kutembelea kanda zake zote. Aliendelea na wadhifa huo hadi mwaka 1605. Kati ya majukumu mazito ndani ya shirika na ya Kanisa kwa jumla aliendelea kuwa mfuasi mnyenyekevu wa Fransisko wa Asizi, mbali ya kuandika vitabu vingi - vya ufafanuzi wa Biblia, vya maadili, vya hoja za kidini pamoja na hotuba nyingi, kama zile maarufu juu ya Bikira Maria - vilivyomstahilia jina la "Doctor Apostolicus", yaani "Mwalimu wa Kitume". Katika maandishi yake, alizungumzia mara nyingi liturujia. Anakumbukwa pia kwa ibada yake kwa ekaristi na kwa neema za pekee alizokuwa anazipata wakati wa kuiadhimisha, zilizomfanya achukue masaa kila siku kuadhimisha Misa, ambayo kwake ilikuwa hai. Alikuwa kama akitekwa na huo ukumbusho wa mateso, kifo na ufufuko wa Bwana. Pamoja na kutumia muda mwingi kusali, kwa ari yake ya pekee alikuwa akihimiza mapadri na waamini wengineo kuyapa kipaumbele maisha ya sala, kwa kuwa ndiyo njia ya kuongea na Mungu. "Lo, kama tungezingatia ukweli huu! Yaani kwamba Mungu yupo kweli na sisi tunaposema naye katika sala; kwamba yeye anasikiliza kweli sala zetu, hata tukisali kwa mioyo na akili yetu tu. Tena si tu kwamba yupo nasi na kutusikiliza, bali yuko radhi na kufurahi sana kutujalia tunachomuomba". Laurenti alionyesha kazi ya Roho Mtakatifu katika maisha ya waamini, akiwaangaza na kuwaimarisha kwa vipaji vyake waweze kuishi Injili kwa furaha. "Roho Mtakatifu anasaidia ubebaji wa nira ya sheria ya Mungu na kupunguza uzito wake, ili tuweze kushika amri za Mungu kwa urahisi mkubwa na hata kwa furaha". Vilevile aliangazia nafasi ya pekee ya Bikira Maria, akithibitisha kuwa alitungwa bila dhambi ya asili akashiriki kazi ya ukombozi iliyofanywa na Kristo. Heshima iliyomfuata kila mahali ilimfanya awe anatafutwa na kusikilizwa kama mshauri. Sifa yake nyingine ni juhudi kwa ajili ya amani. Mara nyingi Mapapa na watawala wa nchi Katoliki walimchagua kama balozi ili kutatua matatizo na kustawisha uelewano kati ya nchi za Ulaya ambazo wakati huo zilikuwa zinatishwa kuvamiwa na Dola la Waturuki Waosmani. Mwaka [] alitumwa na wananchi wa Napoli walionyanyaswa na makamu wa mfalme wa Hispania akawatetee kwa mfalme mwenyewe, Filipo III. Baada ya kukwepa njama mbalimbali, alitabiri kuwa mwenyewe atakufa mapema, na mfalme atamfuata kabla ya miaka miwili kwisha, kama ilivyotokea. Alifariki Belém, Ureno, tarehe 22 Julai [], labda kwa sumu, wakati wa usuluhishi huo. ''Opera omnia'', yaani maandishi yake yote katika magombo 15 yametolewa kitaalamu huko Quaracchi miaka []-[]. Kati yake kuna: *''Mariale'' *''Lutheranismi hypotyposis'' *''Explanatio in Genesim'' *''Quadragesimale primum'' *''Quadragesimale secundum'' *''Quadragesimale tertium'' *''Quadragesimale quartum'' *''Adventus'' *''Dominicalia'' *''Sanctorale'' *''Sermones de tempore'' *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko * Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 238-240 * Sala ya Kanisa ya Ki-fransisko - Benedictine Publications Ndanda - Peramiho, 1996, uk 213-229 * John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 251-252 * Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 496-499 * [http://www.newadvent.org/cathen/09359a.htm Catholic Encyclopedia article] (retrieved Aug 23, 2005) * [http://www.capuchinfriars.org.au/saints/laurence.shtml Capuchin Franciscan Friars of Australia biography] (retrieved Aug 23, 2005) * [http://www.catholic-forum.com/saints/saintl15.htm Patron Saints Index biography] (retrieved Aug 23, 2005) Jamii:Waliozaliwa 1559 Jamii:Waliofariki 1619 Jamii:Wafransisko Jamii:Mapadri Jamii:Watakatifu wa Italia Jamii:Walimu wa Kanisa
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Laurenti_wa_Brindisi
| null | 9,466
|
Makumbusho ya Kitaifa ya Utumwa
|
thumb|'''Makumbusho ya Kitaifa ya Utumwa''' '''Makumbusho ya Kitaifa ya Utumwa''' (kwa Kireno: Museu Nacional da Escravatura) yanapatikana Morro da Cruz, Luanda, Angola. Jumba hilo la makumbusho lilianzishwa mwaka wa [] na Taasisi ya Kitaifa ya Uzalendo wa Kitamaduni, kwa madhumuni ya kuonyesha historia ya utumwa nchini Angola. Jumba hilo la makumbusho linapakana na Capela da Casa Grande, lenye muundo wa karne ya 17 ambapo watumwa walibatizwa kabla ya kuwekwa kwenye meli za watumwa na kusafirishwa hadi Amerika. Jumba hilo la makumbusho linaonyesha mamia ya vitu vilivyotumika katika biashara ya utumwa na liko katika mali ya zamani ya Álvaro de Carvalho Matoso, nahodha wa ofisi kuu ya Forte de Ambaca, Fortaleza da Muxima, na Forte de Massangano nchini Angola, na wafanyabiashara wakubwa wa watumwa kwenye pwani ya Afrika katika nusu ya kwanza ya Karne ya 18. Matoso alifariki mwaka wa [], na familia yake na warithi waliendelea na biashara ya watumwa hadi [] wakati amri ya Maria II wa Ureno ilipiga marufuku usafirishaji wa watumwa kutoka milki ya Ureno. Jamii:Makumbusho ya Angola Jamii:Historia ya Angola Jamii:Historia ya Afrika Jamii:Utumwa Jamii:Sanaa ya Afrika Jamii:Luanda Jamii:Wiki4uni Jamii:Afrocuration Project 2022 Tanzania
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Makumbusho_ya_Kitaifa_ya_Utumwa
| null | 38,786
|
Bahari ya Japani
|
thumb|right|350px|Eneo la Bahari ya Japani '''Bahari ya Japani''' ni kando ya bahari ya magharibi mwa Bahari ya Pasifiki. Imepakana na Japani, Korea Kusini, Korea Kaskazini na Urusi. Bahari hii huko Korea Kaskazini hutajwa kama '''Bahari ya Mashariki mwa Korea''' na huko nchini Korea Kusini hutajwa kama '''Bahari ya Mashariki'''. Jamii:jiografia ya Japani Jamii:Bahari ya pembeni
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari_ya_Japani
| null | 9,109
|
Jean Bakomito Gambu
|
'''Jean Bakomito Gambu''' (alizaliwa Nebobongo, Mkoa wa Uele Juu, 14 Januari 1977) ni mwanasiasa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alichaguliwa kuwa seneta tarehe 31 Januari 2019 na kuwa rais wa Kamati ya Siasa, Utawala, Mahakama na Haki za Binadamu ya Seneti kutoka 26 Novemba 2020 hadi Januari 2024. Alijiuzulu nafasi yake kama seneta ili kuchagua kiti chake katika Bunge la Kitaifa. Pia amekuwa Rais wa Chama cha Bar cha Mkoa wa Haut-Uele tangu 2018; Alichaguliwa tena kwa miaka 3 mnamo 2022. Mnamo Aprili 28, 2024, alichaguliwa kuwa gavana wa jimbo la Haut-Uele akimrithi Christophe Baseane Nangaa,kwa kura 11 kati ya 20. Hata hivyo, uchaguzi wake unapingwa na mashirika ya haki za binadamu kutokana na kasoro kadhaa, ikiwa ni pamoja na wizi wa matokeo na vitisho. Jamii:wanasiasa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jean_Bakomito_Gambu
| null | 52,432
|
Kim Grant
|
'''Kim Grant''' (alizaliwa 25 Septemba []) ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Ghana. Aliwahi kucheza timu ya taifa ya Ghana. Grant ameichezea timu ya taifa ya Ghana tangu mwaka wa 1996. Grant alicheza Ghana katika mechi 7, akifunga mabao 1. {| class="wikitable" style="text-align:center;" !colspan="3"|Timu ya Taifa ya Ghana |- !Mwaka||Mechi||Magoli |- |1996||3||1 |- |1997||4||0 |- !Jumla||7||1 |} Jamii:Wachezaji mpira wa Ghana
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kim_Grant
| null | 31,723
|
Mase
|
Jacksonville, Florida View the Music Artists Biography Online VH1.com |accessdate=2009-12-15 |archivedate=2009-09-13 |archiveurl=https://web.archive.org/web/20090913124510/http://www.vh1.com/artists/az/mase/bio.jhtml }} |Origin = Harlem, New York |Genre = Hip hop |Years_active = 1995-present |Associated_acts = Harlem World, Raw-Talent DMX, Sean "Puffy" Combs, The Notorious B.I.G., Cam'ron, Lil' Cease, The LOX, Big L, Junior M.A.F.I.A. |Label = Bad Boy Records }} '''Mason Durell Betha''' (amezaliwa 27 Agosti []), ^ Gazeti la XXL Septemba 2002, page 101 anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii '''Mase''' (mara nyingi kama '''Ma $ e),''' awali inajulikana kama '''Murda Ma $ e,''' ni rapa wa Marekani, mtunzi, mwimbaji apendwaye kwenye runinga na msemaji. Yeye alikuwa msanii tarehe Sean "Diddy" Combs alikuwa na rekodi ya nyimbo za kisasa Bad Boy studio wakati wa miaka ya 1990. Yeye iliyotolewa albamu mbili katika Bad Boy,zinazojulikana mno ''Harlem World'' na jaribio , ''Double Up.'' Yeye alistaafu mwakani 1999, tu kurudi muziki mwaka 2004 na albamu ''Welcome Back.'' Mwakani 2005, alijaribu kutia mkataba na Rekodi ya G-Unit. Baada ya G-Unit kushughulikia usingeweza walikamilisha, Mase mara wanaohusishwa na Rekodi ya src. Mwanzilishi aw Src Steve Rifkind mara kazi Mase kusainiwa mwaka 2007, lakini, kama [], hakuweza kusikizana kisheria na Diddy juu ya kununua mkataba wa Mase. Rifkind imekuwa rekodi kuzungumza juu ya albamu ambayo Mase alitolea alipokuwa kwa src, ambayo ilikuwa kuwa aidha wenye jina "Suicide Note" au "The Revival." Katika mahojiano na gazeti la Hip-Hop XXL Rifkind alidai kuwa itakuwa imetolewa mwisho wa mwaka na kwamba alikuwa "ya kufurahisha." Albamu mara kamwe haikutolewa. Baada ya muda , Mase akarudi tena rapu Juni 2009. Oktoba ya mwaka huo, Diddy saini Mase's release kutoka Bad Boy Records. Katika Novemba, yeye imeshuka mixtape yake ya kwanza katika miaka mitatu, "I Do The Impossible". Ni kwa kushirikiana na zamani featured Watoto wa wanachama nafaka Cam'ron ( "Get It") na Mcgruff ( "Kama mimi Come Back For You"), na Remixes ya nyimbo kama hit Empire State of Mind. Yeye sasa ananunua rekodi mpya ya kushughulikia kazi ya albamu yake ya nne, "The Mason Betha Story". *''Harlem World'' (1997) *''Double Up'' (1999) *''Welcome Back'' (2004) *G-Unit Radio 16: Crucified 4 Da Hood 2006 *''I Do The Impossible'' 2009 * * Jamii:Waliozaliwa 1977 Jamii:Watu walio hai Jamii:Wanamuziki wa Marekani Jamii:Marapa wa Marekani Jamii:Watu kutoka Atlanta, Georgia Jamii:Watu kutoka Jacksonville, Florida Jamii:Watu kutoka Manhattan Jamii:Watu kutoka New York
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mase
| null | 9,682
|
Rasi ya Malay
|
right|Rasi ya Malay '''Rasi ya Malay''' (Kimalay: ''Semenanjung Tanah Melayu'') ni rasi kubwa katika Asia ya Kusini-Mashariki.The Physical Geography of Southeast Asia, Avijit Gupta Ina sehemu tatu zilizo chini ya nchi tofauti: * Kaskazini-magharibi yake ni eneo la kusini kabisa ya Myanmar (Burma) * Katikati yake ni eneo la Uthai * Kusini ni eneo la Malaysia ya magharibi Kusini kabisa kwake, karibu na ncha ya rasi, iko nchi ya Singapuri kwenye kisiwa Rasi ya Malay iko kati ya Bahari Hindi na Pasifiki. Upande wa Pasifiki ni Ghuba ya Uthai na Bahari ya Uchina. Mlango wa Malakka unatenganisha rasi na kisiwa cha Sumatra. Rasi inaanza kwenye latitudo ya +13 na kuelekea kusini hadi latitudo ya +1. Urefu wake ni km. 1,555. Sehemu nyembamba iko katika sehemu ya Kithai yenye km 60 pekee. Sura ya nchi ina tabia mbalimbali: milima, tambarare, maziwa, pwani na misitu minene. Milima ya juu ni Gunung Tahan (m 2,187) na Gunung Korbu (m 2,184) nchini Malaysia. Katika tambarare za Uthai iko Khao Luang (m 1,786). Sehemu ya Myanmar kuna Recho Taung (m 1,330). Jamii:jiografia ya Myanmar Jamii:jiografia ya Uthai Jamii:jiografia ya Malaysia Jamii:Rasi za Asia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rasi_ya_Malay
| null | 2,400
|
Augustine Ndeliakyama Shao
|
'''Augustine Ndeliakyama Shao''', CSSp (alizaliwa katika Wilaya ya Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania, 25 Septemba []) ni mchungaji wa Kanisa Katoliki la Tanzania na amekuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Zanzibar tangu mwaka 1997. Aliwekwa wakfu kuwa kasisi wa Shirika la Roho Mtakatifu (Holy Ghost Fathers) tarehe 4 Juni 1983. Papa Yohane Paulo II alimteua kuwa Askofu wa Zanzibar tarehe 30 Novemba 1996, na alipewa daraja ya uaskofu tarehe 27 Aprili 1997 kutoka kwa Polycarp Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Mbali na majukumu yake Zanzibar, Papa Benedikto XVI alimteua kuwa mshiriki wa Baraza la Kipapa la Majadiliano ya Kidini tarehe 20 Juni 2009. Askofu Shao amekuwa mtetezi wa ushirikiano wa Kanisa na tamaduni za Kiafrika, akisisitiza umuhimu wa kuelewa mila na desturi za mitindo za watu ili kuwezesha majadiliano ya kweli na ujumuishaji wa imani ya Kikatholiki. Pia ameizungumzia changamoto ya vurugu dhidi ya makasisi zinazotokana na magaidi wa Kiislamu, ambayo imekuwa tatizo kubwa katika dayosisi yake. Katika Mkutano Maalum wa Sinodi ya Maaskofu wa Afrika uliofanyika Oktoba 2009, alizungumzia haja ya kubadilisha mtazamo wa maaskofu wa Afrika kuhusu tamaduni na desturi zao, akisisitiza umuhimu wa kuleta usawa kati ya Ukristo na Dini asilia za Kiafrika. Jamii:Waliozaliwa 1951 Jamii:Waspiritani Jamii:Maaskofu Wakatoliki wa Tanzania Jamii:Watu walio hai
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Augustine_Ndeliakyama_Shao
| null | 53,383
|
João Mário
|
thumb|Joao Mario '''João Mário''' (amezaliwa tarehe 19 Januari []) ni mchezaji anayecheza katika klabu ya Internazionale ya Milano iliyopo katika ligi kuu ya Italia iitwayo Seria A na pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno. Alianza katika klabu ya Sporting CP ambaye mfumo wake wa vijana alikikuza kipaji chake, akiwa amekopwa kwa Vitória de Setúbal mwaka [] na kisha kurudi katika klabu yake na kuwa miongoni mwa wachezaji walisaidi timu kufanya vizuri katika mashindano hayo. João Mário alifanya mechi yake ya kwanza kwa Ureno mwaka 2014. Amechaguliwa kwa Kombe la Dunia la FIFA 2018 na alionekana katika Euro [], kushinda mashindano hayo ya mwisho. Jamii:waliozaliwa 1993 Jamii:watu walio hai Jamii:wachezaji mpira wa Ureno
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/João_Mário
| null | 26,521
|
Kitetela (lugha)
|
'''Kitetela''' ni lugha ya Kibantu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inayozungumzwa na Watetela. Mwaka wa [] idadi ya wasemaji wa Kitetela imehesabiwa kuwa watu 750,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kitetela iko katika kundi la C80. *[http://multitree.org/codes/tll lugha ya Kitetela kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/tll makala za OLAC kuhusu Kitetela] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/tete1250 lugha ya Kitetela katika Glottolog] *http://www.ethnologue.com/language/tll Jamii:Lugha za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jamii:Lugha za Kibantu
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kitetela_(lugha)
| null | 13,649
|
Kiwakilishi nafsi
|
'''Kiwakilishi nafsi''' (pia: '''Kiwakilishi cha nafsi''') ni aina ya neno/maneno yanayosimama badala ya majina yanayotaja nafsi za watu. Viwakilishi vya nafsi hugawanyika katika makundi mawili, nayo ni: *Viwakilishi vya nafsi huru *Viwakilishi vya nafsi kiambata Haya ni maneno mazima yanayoweza kusimama peke yake bila kuambatanishwa katika neno au mzizi wa neno jingine. {| class="wikitable" |- ! Nafsi !! Umoja !! Wingi |- | I || Mimi || Sisi |- | II || Wewe || Ninyi/nyinyi |- | III || Yeye || Wao |} ;Mifano zaidi: *''Mimi ni mwalimu'' *''Sisi ni walimu'' *''Wewe ni mwalimu'' *Nyinyi ni walimu'' *''Yeye ni mwalimu'' *''Wao ni walimu'' Hizi ni mofimu tegemezi/vipande vya maneno vinavyoambikwa/vinavyoambatanishwa katika neno au mzizi wa neno jingine ili kudokeza nafsi inayohusika. Mfano: ''Nikija nitawapeleka'', ''Tukisoma tutafaulu'', ''Ukija utakiona cha moto'', ''Mkija atawaona'', ''Asiyekujua hakuthamini'', ''Waliosafiri wamefika salama''. {| class="wikitable" |- ! Nafsi !! Umoja !! Wingi !! Mzizi |- | I || '''Ni''' || '''Tu''' || '''Ni'''kija/'''Tu'''kija |- | II || '''U''' || '''M''' || '''U'''kija/'''M'''kija |- | III || '''A''' || '''Wa''' || '''A'''kija/'''Wa'''kija |} *Lango:Lugha *Viwakilishi * Massamba, David. 2004. "Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Jamii:Isimu Jamii:Kiswahili
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiwakilishi_nafsi
| null | 12,839
|
Protoni
|
thumb|Muundo wa protoni '''Protoni''' ni chembe ndani ya atomi. Ni sehemu ya kiini cha atomi yenye chaji ya chanja pamoja na neutroni zisizo na chaji. Elementi zapangwa katika mfumo radidia kufuatana na idadi ya protoni. Masi ya protoni ni ndogo sana. Huaminiwa ya kwamba kila protoni inajengwa na quark tatu. Jamii:Fizikia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Protoni
| null | 3,492
|
Richard Smalley
|
thumb|200px|right|Richard Errett Smalley left|80px '''Richard Errett Smalley''' (6 Juni [] – 28 Oktoba []) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Marekani. Hasa amefahamika kwa kugundua na kuchunguza mfumo mpya wa kaboni. Mwaka wa [], pamoja na Robert Curl na Harold Kroto alikuwa mshindi wa '''Tuzo ya Nobel ya Kemia'''. Category:Waliozaliwa 1943 Category:Waliofariki 2005 Category:Wanasayansi wa Marekani Category:Tuzo ya Nobel ya Kemia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Richard_Smalley
| null | 11,939
|
Uwanja wa michezo wa Dr. Petrus Molemela
|
'''Uwanja wa michezo wa Dr. Petrus Molemela''' ni uwanja wa michezo ambao hapo zamani ulitambulika kama uwanja wa michezo wa '''Seisa Ramabodu'''. Ni uwanja wenye matumizi mengi na unapatikana Bloemfontein nchini Afrika Kusini. Kwa sasa unatumika kwa mchezo wa mpira wa miguu na ulitumika kama uwanja wa mazoezi kwa timu zilizoshiriki Kombe la Dunia la FIFA ya mwaka [] baada ya kuboreshwa mnamo mwaka [] na kufikia viwango vya FIFA.[https://web.archive.org/web/20090410184921/http://www.sa2010.gov.za/node/1936] Ni uwanja wa nyumbani kwa klabu ya Bloemfontein Celtic ambapo hutumia pia uwanja wa michezo wa Free state. Baada ya maboresho ya miaka mitatu(3) iliyokamilika mwaka [], uwezo wa uwanja kubeba washabiki uliongezeka kutoka ''18,000'' hadi ''22,000''. Jamii: Africa Wiki Challenge Arusha Jamii: Viwanja vya michezo Afrika Kusini
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uwanja_wa_michezo_wa_Dr._Petrus_Molemela
| null | 35,938
|
Wendy Brown
|
thumb|180px|right|Wendy Brown mwaka 2016 '''Wendy L. Brown''' (alizaliwa Novemba 28, []) ni mwananadharia wa siasa wa nchini Marekani. Ni profesa wa UPS katika shule ya sayansi ya jamii katika taasisi ya mafunzo ya juu huko Princeton, NJ. Hapo awali, alikuwa darasa la [] Profesa wa kwanza wa sayansi ya siasa na mshiriki mkuu katika mpango wa nadharia muhimu katika Chuo kikuu cha California, Berkeley. Jamii:Waliozaliwa 1955 Jamii:Watu walio hai Jamii:Wanawake wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wendy_Brown
| null | 38,624
|
South Plainfield, New Jersey
|
thumbnail|right|250px|CSX Treni Q410 kupitia njia ya kuvuka kwa barabara ya Metuchen huko South Plainfield, New Jersey mnamo 2005 thumb|right|260px|Mahali pa mji wa South Plainfield katika Middlesex County na [[New Jersey]] '''South Plainfield''' ni mji wa Marekani katika jimbo la New Jersey. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mnamo mwaka wa 2007, mji una wakazi wapatao 23,000 wanaoishi katika mji huu. Mji upo m 24 kutoka juu ya usawa wa bahari. Eneo lake ni 22 km². Jamii:Miji ya New Jersey Jamii:Middlesex County, New Jersey
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/South_Plainfield,_New_Jersey
| null | 11,686
|
Brunei
|
(translation) |national_anthem = ''Allah Peliharakan Sultan''"Mungu ambariki Sultani" |official_languages = Kimalay na Kiingereza |capital = Bandar Seri Begawan |latd=4 |latm=55 |latNS=N |longd=114 |longm=55 |longEW=E |largest_city = Bandar Seri Begawan |government_type = Ufalme |leader_titles = Sultani |leader_names = Hassanal Bolkiah |area_rank = ya 170 |area_magnitude = 1 E9 |area = 5,765 |areami² = 2,226 |percent_water = 8.6 |population_estimate = 442,400 |population_estimate_rank = ya 168 |population_estimate_year = 2018 |population_census = 332,844 |population_census_year = 2001 |population_density = 72.11 |population_densitymi² = 186.8 |population_density_rank = ya 134 |GDP_PPP = $9.009 billion |GDP_PPP_rank = ya 138 |GDP_PPP_year = 2005 |GDP_PPP_per_capita = $24,826 |GDP_PPP_per_capita_rank = ya 26 |sovereignty_type = Uhuru kutoka Uingereza |established_events = Mwisho wa hali ya nchi lindwa |established_dates = 1 Januari [] |HDI = 0.866 |HDI_rank = ya 35 |HDI_year = 2004 |HDI_category = high |currency = Brunei ringgit |currency_code = BND |country_code = |time_zone = |utc_offset = +8 |time_zone_DST = |utc_offset_DST = |cctld = .bn |calling_code = 6731 |footnotes = 1 Also 080 from Malaysia. }} '''Brunei''', rasmi '''Brunei Darussalaam''' (برني دار السلام , ''Negara Brunei Darussalaam'') ni usultani mdogo na nchi huru kaskazini mwa kisiwa cha Borneo huko Asia ya Kusini-Mashariki. Imepakana na majimbo ya Sarawak na Sabah ya Malaysia tu, ingawa sehemu kubwa ya kisiwa hicho inatawaliwa na Indonesia. Mji mkuu ni Bandar Seri Begawan. Mnamo 2024 ina idadi ya watu takriban 462,271. Lugha rasmi ni Kimalay huku Kiingereza kikitumiwa katika mandhari rasmi na shuleni. Mtawala wa nchi ni sultani Hassan al-Bolkiah. Anasemekana kuwa kati ya watu tajiri zaidi duniani kutokana na mapato ya mafuta ya petroli. Dola la Brunei lilistawi kuanzia mwaka [] hadi karne ya 17 likienea katika sehemu kubwa ya Borneo na hata visiwa vingine. Lilipokea Uislamu katika karne ya 15. Baada ya kunyang'anywa maeneo mengi na Wazungu (Wahispania, Waholanzi na Waingereza), mwaka [] sultani aliomba ulinzi wa Uingereza ambao uliendelea hadi uhuru wa mwaka []. Wakazi wengi (66%) ni wa jamii ya Wamalay, 10% ni Wachina, 3.4% ni Waborneo asili, 2.3% ni Wahindi, 16.8% wana asili tofauti. Lugha rasmi ni Kimalay, lakini Kiingereza pia kinatambuliwa na katiba ya nchi. Dini rasmi ni Uislamu wa madhehebu ya Sunni ambayo inafuatwa na thuluthi mbili za wakazi, lakini wakazi wengine wanafuata dini za Ubuddha (13%), Ukristo (10%) na dini za jadi (2%). Asilimia 7 hawana dini maalumu. * Orodha ya lugha za Brunei * Orodha ya nchi kufuatana na wakazi * * * * * * * * * * * * ; Serikali * [http://www.jpm.gov.bn/index.htm Prime Minister's Office of Brunei Darussalam] website ; Taarifa za jumla * * [http://ucblibraries.colorado.edu/govpubs/for/brunei.htm Brunei] from ''UCB Libraries GovPubs'' * * [http://www.bbc.co.uk/news/world-asia-pacific-12990058 Brunei profile] from the BBC News * [http://www.britannica.com/EBchecked/topic/82119/Brunei Brunei] at ''Encyclopædia Britannica'' * * [http://www.ifs.du.edu/ifs/frm_CountryProfile.aspx?Country=BN Key Development Forecasts for Brunei] from International Futures ; Biashara * [http://www.onebrunei.com/ Brunei Business Directory] ; Utalii * [http://www.tourismbrunei.com/ Brunei Tourism] website * [http://brulink.com/ Brunei Attractions] website * [https://web.archive.org/web/20090222020511/http://globaledge.msu.edu/countryInsights/country.asp?CountryID=15 Brunei information on globalEDGE] Jamii:Brunei Jamii:Nchi za visiwa Jamii:Nchi za Asia Jamii:Borneo Jamii:Jumuiya ya Madola
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Brunei
| null | 2,397
|
Gambamiti
|
'''Gambamiti''' ni spishi za nyoka wa jenasi ''Hemirhagerrhis'' katika familia Lamprophiidae. Mchana hupanda miti na vichaka ambapo huwinda mijusi na kula mayai yao. Juu ya gome la mti hawaonekani vizuri kwa ajili ya muungano wa rangi, madoa na milia (kamafleji, asili ya jina lao). Chonge zao ni meno ya nyuma kabisa na mdomo ni mdogo. Kwa hivyo gambamiti sio hatari kwa watu. Waama wakikaribishwa hawasogei na wanategemea majificho yao. * ''Hemirhagerrhis hildebrandtii'' Gambamiti Mashariki (Eastern bark snake) * ''Hemirhagerrhis kelleri'' Gambamiti Milia (Striped bark snake) * ''Hemirhagerrhis nototaenia'' Gambamiti wa Kawaida (Bark snake) * ''Hemirhagerrhis viperina'' Gambamiti wa Angola (Western bark snake) * Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) ''A field guide to the Reptiles of East Africa.'' Academic Press, San Diego, CA, USA. * [http://www.reptile-database.org/ Hazinadata ya watambaachi] Jamii:Nyoka
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gambamiti
| null | 25,412
|
Arialdo wa Milano
|
thumb|Mt. Arialdo alivyochorwa. '''Arialdo wa Milano''' (Italia Kaskazini, [] hivi - []) alikuwa shemasi wa Kanisa Katoliki aliyepinga kwa nguvu usimoni na maadili mengine mabovu ya wakleri [https://books.google.com/books?id=FGw_AAAAYAAJ&dq=St.+Arialdo&pg=PA227 Lea, Henry Charles. ''An Historical Sketch of Sacerdotal Celibacy in the Christian Church'', J.B. Lippincott, 1867]. Kutokana na juhudi hizo kwa ajili ya nyumba ya Mungu, hatimaye aliuawa kwa mateso makali na wakleri wawili http://www.santiebeati.it/dettaglio/59700. Mwaka mmoja baada ya kifo chake, Papa Aleksanda II alimtangaza mtakatifu mfiadini. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 27 JuniMartyrologium Romanum. *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko *[http://www.newadvent.org/cathen/10298a.htm Archdiocese of Milan] at the Catholic Encyclopedia *[http://www.santiebeati.it/dettaglio/59700 Sant' Arialdo di Milano] *[https://web.archive.org/web/20060821165839/http://www.eresie.it/id287.htm Sant' Arialdo da Carimate] Category:Mashemasi Jamii:Wafiadini Wakatoliki Category:Watakatifu wa Italia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Arialdo_wa_Milano
| null | 45,250
|
Kingston
|
'''Kingston''' ni jina la miji mbalimbali duniani. Asili ya jina hilo ni Kiingereza "King's Town" yaani "mji wa mfalme". Nchini Uingereza kuanzishwa kwa mji ulihitaji kibali cha mfalme wa nchi. Hivyo tamko la "mji wa mfalme" likawa sehemu ya jina la mji mara kadhaa. Waingereza kutoka miji mbalimbali iliyoitwa "Kingston" walipeleka jina hili kote duniani walipoanzisha miji katika koloni zao au kutoa majina mapya kwa miji ya koloni. * Kingston (kisiwa cha Norfolk makao makuu ya eneo * Kingston SE - Australia Kusini * Kingston-On-Murray - Australia Kusini * Kingston (Tasmania) * Kingston (Victoria) * Kingston (Jamaika) - mji mkuu * Kingston (New Brunswick) * Kingston (Nova Scotia) * Kingston (Ontario) * Kingston (Georgia) * Kingston, Massachusetts * Kingston (Michigan) * Kingston (New Hampshire) * Kingston (New Jersey) * Kingston (New York) * Kingston (Ohio) * Kingston (Oklahoma) * Kingston (Pennsylvania) * Kingston (Rhode Island) * Kingston (Tennessee) * Kingston (Utah) * Kingston (Washington) * Kingston (New Zealand) - mji mdogo kwenye kisiwa cha kusini * Kingston upon Hull * Kingston upon Thames karibu na London * Kingston, Cambridgeshire * Kingston, Devon * Kingston, Dorset * Kingston near Lewes - East Sussex * Kingston, Hampshire * Kingston, Portsmouth - Hampshire * Kingston, Isle of Wight * Kingston, Kent * Kingston Bagpuize - Oxfordshire * Kingston Blount - Oxfordshire * Kingston by Ferring - West Sussex * Kingston by Sea - West Sussex * Kingston Deverill - Somerset * Kingston Lisle - Oxfordshire * Kingston on Soar - Nottinghamshire * Kingston, East Lothian * Kingston, Moray * Kingston Bridge, Tradeston, Glasgow
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kingston
| null | 2,512
|
Mundu
|
thumb|Mundu thumb|Mundu na nyundo katika nembo la Austria '''Mundu''' ni kifaa kinachotumiwa katika kilimo kwa kukata nyasi na mavuno ya nafaka na mazao mengine. Mundu kama zana ya kilimo inajulikana tangu zama za mawe. Katika nchi nyingi za dunia haitumiwi tena sana kwa sababu nafasi yake imechukuliwa na mashine lakini pale ambako kazi ya kilimo inatekelezwa kwa mkono ni mahali pake hadi leo. Umbo la mundu ni kama kisu kirefu kilichopindwa kama kotama ndefu. Upande wa ndani ya bapa ni kali, upande wa nje ahuna ukali. Umbo la mundu lilitumiwa pia kama silaha kwa aina za pekee za upanga. Katika nembo la Austria na pia la Umoja wa Kisovyeti wa zamani mundu ni alama ya wakulima ikionyeshwa pamoja na nyundo kama alama ya wafanyakazi. Category:Zana za kilimo
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mundu
| null | 18,610
|
Makabila ya Zanzibar
|
'''Makabila ya Zanzibar''', visiwa vya Tanzania vilivyoko Bahari ya Hindi, yanawakilisha mchanganyiko wa tamaduni za Kiafrika, Kiarabu, Kishirazi, na Kiasia kutokana na historia ya biashara ya baharini, ukoloni, na uhamiaji wa karne nyingi. Zanzibar hakuna makabila ya moja kwa moja bali watu huitwa kimaeneo. Yaani, watu wa eneo fulani watwaita kwa jina la eneo hilo. Jamii kuu ni: * Wapemba – jamii ya wenyeji wa Kisiwa cha Pemba, huzungumza lahaja ya Kipemba, wanajulikana kwa tamaduni za kifamilia, kilimo cha karafuu, na mavazi ya kanzu na kofia. * Waunguja – jamii ya wenyeji wa Kisiwa cha Unguja, huzungumza Kiunguja, wanajulikana kwa tamaduni za Uislamu, muziki wa taarab, na sherehe za Maulidi na Eid. * Wamakunduchi – jamii ya kihistoria ya Kusini mwa Unguja, wanajulikana kwa tamaduni za Unyago, Ngoma ya Makunduchi, na mavazi ya jadi. * Wangazija – jamii yenye asili ya Komoro, huzungumza Kingazija, wanajulikana kwa tamaduni za Kiislamu, mapishi ya pilau, na sherehe za harusi za jadi. * Waarabu – jamii ya kihistoria kutoka Oman na Yemen, wanajulikana kwa tamaduni za kifalme, biashara ya karafuu, na urithi wa Usultani wa Zanzibar. * Washirazi – jamii ya kihistoria yenye asili ya Uajemi, wanajulikana kwa tamaduni za Uislamu, lugha ya Kiswahili yenye athari ya Kiajemi, na historia ya miji ya kale. * Wahindi – jamii ya wafanyabiashara wa asili ya Uhindi, hasa Gujarati, Goa, na Tamil, wanajulikana kwa tamaduni za Hindu, Sikh, na Uislamu, pamoja na biashara ya vito, nguo, na viungo. * Wachina – jamii ndogo ya kihistoria na kisasa, wanajulikana kwa tamaduni za Buddha, biashara ya rejareja, na vyakula vya jadi. * Wahamiaji wa kisasa – jamii kutoka Afrika Mashariki, Asia, na Ulaya, wanachangia katika utofauti wa lugha, dini, na tamaduni za kisasa. Lugha rasmi ni Kiswahili, lakini lahaja kama Kiunguja, Kipemba, Kimakunduchi, na Kingazija hutumika katika maisha ya kila siku. Tamaduni za Zanzibar hujumuisha muziki wa taarab, ngoma za unyago, vyakula vya pilau, urojo, na sherehe za Maulidi, Eid, na Siku ya Mapinduzi. Jamii:Makabila ya Afrika Jamii:Makabila ya Tanzania Jamii:Makabila ya Zanzibar Jamii:Afrocrowd 2025
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Makabila_ya_Zanzibar
| null | 57,422
|
Waovimbundu
|
'''Waovimbundu''', wanaojulikana pia kama Wambundu wa Kusini, ni kundi la kikabila la Kibantu linaloishi katika Uwanda wa Bié katikati mwa Angola na katika ukanda wa pwani magharibi ya milima hiyo. right|thumb|Pipa ya kuvutia ya Ovimbundu kutoka karne ya 19, iliyotengenezwa kwa mbao na metali. Inahifadhiwa katika Makumbusho ya Quai Branly, Paris. Wakiwa ndio kundi kubwa zaidi la kikabila nchini, wanawakilisha takriban asilimia 38 ya idadi ya watu wa nchi hiyo. Kwa kiasi kikubwa, Waovimbundu ni Wakristo, hasa wa Kanisa la Igreja Evangélica Congregacional de Angola (IECA) lililoanzishwa na wamisionari kutoka Marekani, na Kanisa Katoliki. Hata hivyo, baadhi yao bado wanashikilia imani na desturi za dini za jadi za Kiafrika. Waovimbundu asili yao ni kutoka jamii za Kibantu ambazo zilihama kaskazini katika kipindi cha karne nyingi zilizopita. Jamii hizo ziliunda makundi ya kijamii na kikanda ambayo hatimaye yakawa vitengo vya kisiasa na vyanzo vya utambulisho wa kijamii, kama vile M'Balundu, Sele, Wambo, Bieno na mengineyo. Walikuza kilimo cha hali ya juu, kilichokamilishwa na ufugaji wa wanyama wadogo kama kuku, mbuzi na nguruwe, pamoja na idadi ndogo ya ng'ombe waliowanunua kutoka kwa wakulima-wafugaji wa kusini (Nyaneka-Nkhumbi, Ovambo. Jamii:makabila ya Angola Jamii:Afrocrowd 2025
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Waovimbundu
| null | 57,244
|
Elizabeth Michael
|
'''Elizabeth Michael''' (maarufu kama '''Lulu'''; amezaliwa 16 Aprili []) ni mwigizaji wa filamu kutoka Tanzania. Mwaka wa [] alishinda tuzo ya Zanzibar International Film Festival kama msanii bora wa kike kupitia filamu "Foolish Age". Mwaka [] alitajwa na Tuzo za Vijana Afrika zifanyikazo nchini Ghana miongoni mwa vijana 100 wa Afrika wenye ushawishi mkubwa. Elizabeth alizaliwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar Es Salaam Tanzania. Ni mtoto wa Lucrecia Kalugira na Michael Kimemeta. Baadaye alijiunga katika shule ya Remnant Academy ambapo alimaliza elimu ya msingi. Alipata kusoma Perfect Vision High School, St Mary's High School kwa ajili ya Elimu ya sekondari. Baadaye alijiunga katika Chuo Cha Utumishi Wa Umma Tanzania (TPSC) akisomea kozi ya stashahada ya Rasilimali watu na Utawala (Diploma In Human Resources Management). Alianza kuigiza akiwa na umri wa miaka mitano mnamo mwaka 2000. Baadae alijiunga na kikundi cha Sanaa Kaole Group ambapo alikuwa pamoja na Steven Kanumba, Vincent Kigosi, Mwanaidi Suka na wengine wengi ambapo aliigiza tamthilia nyingi za runinga kama vile ''Gharika'', ''Taswira'', ''Zizimo '' na nyingine nyingi ambapo alikuwa akitumia jina la Lulu ambalo limekuwa maarufu mpaka leo. Baadae alianza kuigiza filamu akiwa bado na Umri mdogo,a mbapo filamu yake ya kwanza ilikuwa ''Misukosuko'' akishirikiana na Jimmy Mponda. Mnamo mwaka 2006 aliigiza filamu iitwayo ''wema'' iliyoandaliwa na Game 1st Quality na badae filamu nyingine nyingi kama Family Tears,Ripple Of Tears,Passion,Dangerous Girl na nyingine nyingi.Mpaka sasa amepata kuigiza filamu zaidi ya thelathini. Pia amepata kufanya Igizo la redioni lililoitwa ''Wahapahapa'' Akitumia jina la Mainda. lililoandaliwa na Media For Development International wakishirikiana na Ubalozi wa Marekani,Wizara Ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na chuo cha Johns Hopkins University Center For Communication Programs cha Marekani Igizo hilo liliongozwa na mmarekani afanyaye shughuli zake Afrika Bwana Jordan Riber. Pia Katika mradi huohuo wa Wahapahapa alipata kuigiza katika Video mbili za wasanii Lady Jay Dee iitwayo Shamba na Ya Enika iitwayo Changanya. Mradi wa Wahapahapa ulikuwa na lengo la kuelimisha jamii juu Ya malezi bora Ya mtoto katika kipindi cha ukuaji. Mnamo August 2013 Lulu alizindua filamu Yake Iitwayo Foolish Age ambayo Ni filamu Yake ya kwanza kuitaarisha mwenyewe.Ilizinduliwa katika ukumbi wa Mlimani City uliopo Dar Es Salaam Na kuhudhuriwa Na mamia ya Watu.Foolish Age ilifanya vizuri sokoni Na ilipata kuonyeshwa katika Tamasha Kubwa La Kimataifa La Filamu Zanzibar (Zanzibar International Film Festival), na baadae kuteuliwa kuwania Filamu Inayopendwa na Lulu alishinda Muigizaji wa Filamu Wa Kike Anaependwa kupitia filamu hio katika Tuzo za Watu 2014. Mnamo Mwaka 2015 Alizindua Filamu Yake ya pili Kama mtayarishaji iitwayo Mapenzi Ya Mungu. Filamu Hio ilionyeshwa katika Tamasha La Filamu La Kimataifa La Zanzibar (ZIFF) na mwaka 2016 ilishinda Filamu Bora Afrika Mashariki katika Tuzo Za Africa Magic Viewers Choice Awards zilizofanyika Lagos Nigeria. Amewahi Kuwa mtangazaji wa kipindi cha runinga kiitwacho watoto wetu Kinachorushwa na Runinga Ya ITV Tanzania Akiwa na umri mdogo mnamo mwaka 2004-2007. Pia mnamo mwaka 2014 na 2015 alikuwa mtangazaji wa mashindano Ya kutafuta vipaji vya uigizaji Tanzania yaitwayo Tanzania Movie Talents. *2013/14 alichaguliwa Kuwa balozi wa tamasha la filamu liitwalo Dar Film Festival lililofanyika Dar es Salaam. *2015 alifanya kazi na kampuni ya simu ya Airtel Tanzania kama mtangazaji wa kipindi cha Airtel Yatosha Tv Show. *Pia ni balozi wa kampuni ya Paisha Tanzania, ijushughulishayo na ufanyaji wa biashara mitandaoni *Pia aliteuliwa na kampuni ya Hengan Baby Products and Sanitary co ltd Kuwa balozi wa freestyle napkins bidhaa za wanawake kwa miaka miwili *Pia ni balozi wa Sinema Zetu International Film Festival tamasha la filamu linaloandaliwa Na chaneli ya Sinema Zetu ya kampuni ya Azam *Pia ni balozi wa Azania inajulikana kama pishi la Lulu, ni manager wa upcoming actor ajulikanae kama Suhelyht khan ambae jina lake halisi ni Suhely Tarmohammed. {| class="wikitable" ! style="background:#B0C4DE;" | Mwaka ! style="background:#B0C4DE;" | Jina ! style="background:#B0C4DE;" |Uhusika ! style="background:#B0C4DE;" |Maelezo |- | rowspan =10|2000's |''Zizimo'' | rowspan =10| Lulu | rowspan =9| Ilionyeshwa Na Independent Television Tanzania (ITV Tanzania) |- |''Dira'' |- |''Taswira'' |- |''Baragumu'' |- |''Gharika'' |- |''Sayari'' |- |''Tufani'' |- |''Tetemo'' |- |''Jahazi'' |- |''Demokrasia'' |Ilionyeshwa na Shirika la Utangazaji Tanzania/ Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) |- | 2017 | Sarafu |Jackline Sanga "Jack" |Inaonyeshwa na Maisha Magic Bongo (Dstv) |} {| class="wikitable" style="font-size:90%;" background: #f9f9f0; |- style="text-align:center;" ! style="background:#B0C4DE;" | Mwaka ! style="background:#B0C4DE;" | Jina ! style="background:#B0C4DE;" | Uhusika ! style="background:#B0C4DE;" | Maelezo |- |2009 |''Wahapahapa'' |Mainda |Ilirushwa na Radio One Tanzania |- |} {| class="wikitable" style="font-size:90%;" background: #f9f9f0; |- style="text-align:center;" ! style="background:#B0C4DE;" | Mwaka ! style="background:#B0C4DE;" | Filamu ! style="background:#B0C4DE;" | Uhusika ! style="background:#B0C4DE;" | Maelezo/Wahusika |- |2005 !Misukosuko Part 2 |Catherine | Jimmy Mponda,Seba and Salama Salmin(Sandrah) |- |2006 !Wema |Betty |Akishirikiana na Senga |- |2007 !Silent Killer | | Akishirikiana na Mohamed Nurdin(Chekibudi),Shumileta |- |rowspan=3|2008 !Family Tears |Lindah |Akiwa na Steven Kanumba,Wema Sepetu,Jacqueline Wolper and Richard Bezendhout |- !Mtoto wa Nyoka | | |- !Lost Twins | Anitha Mdogo |Akiwa na Steven Kanumba,Hashimu Kambi, Suzan Lewis. |- |rowspan=6|2009 !Taste of Love | |Akiwa na Aunty Ezekiel, Blandina Chagula,Mahsein Awadh. |- !Ripple of Tears |Lizy |Akiwa na Steven Kanumba |- !Passion | |Akiwa Jacqueline Wolper,Irene Uwoya,Yusuph Mlela,Hashim Kambi |- !Unfortunate Love | |Akiwa na Steven Kanumba,Lisa Jensen,Zamda |- !Too Late | |Akiwa na Mahsein Awadh(Dr Cheni),Tumaini Bigirimana(Fifi),Issa Mussa |- !Reason To Die |Nyina |Akiwa na Mahsein Awadh (Dr Cheni) |- |rowspan=3|2010 !Family Disaster |Julieth |Akiwa na Vincent Kigosi,Diana Kimaro |- !Crazy Love |Mwanafunzi |Akiwa na Steven Kanumba,Shamsa Ford,Hemed Suleiman |- !My dreams | |Akiwa Vincent Kigosi,Irene Uwoya,Shamsa Ford,Mahsein Awadh |- |rowspan=4|2011 !Birthday Party | |Akiwa na Salma Jabu(Nisha) |- !Ritazo | |Akiwa na Riyama Ally Na Baraka |- !Tattoo | | |- !Confusion |Besta |Akiwa na Diana Kimario,Hemedi Suleiman |- |rowspan=6|2012 !House Boy |Lulu |Akiwa na Wema Sepetu,Kajala Masanja,and Mr Blue |- !Woman Of Principles |Linah |Akiwa na Vincent Kigosi and Nargis Mohamed |- !Dangerous Girl |Hidaya | |- !Mtoto wa Mbwa |Nice |Akiwa na Simon Mwakapagata (Rado) |- ! Yatima Asiyestahili |Njwele |Akiwa Nice Mohamed(Mtunisy) and Jeniffer Kyaka |- !Oxygen | |Akiwa na Sydney, Hashim Kambi,Grace Mapunda |- |2013 !Foolish Age |Loveness |Akiwa na Diana Kimaro and Hashimu Kambi |- |2014 !Family Curse | |Akiwa na Hashimu Kambi, Yusuph Mlela, Cathy Rupia |- |2015 !Mapenzi Ya Mungu |Shikana |Akiwa na Flora Mtegoa, Linah Sanga |- |2016 !Ni Noma |Angela |Akiwa na Kulwa Kikumba and Isarito Mwakalikamo |- |} *Foolish Age *Mapenzi Ya Mungu *Ni Noma *2013 Zanzibar International Film Festival- Mwigizaji Bora wa Kike *2014 Tuzo za watu - Mwigizaji wa Kike Anayependwa *2016 Africa Magic Viewers Choice Awards- Filamu Bora Afrika Mashariki (Mapenzi Ya Mungu) *2016 Swahili Fashion Week Awards - Style Icon Of The Year Jamii:Waliozaliwa 1995 Jamii:Watu walio hai Jamii:Waigizaji filamu wa Tanzania Jamii:ACWP + film in Tanzania Jamii:Wasanii wanawake Tanzania
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Elizabeth_Michael
| null | 21,908
|
Kordofan Kusini
|
thumb|right|260px|Ramani ya Kurdufan Kusini '''Kordofan Kusini ''' ni mojawapo kati ya majimbo 18 ya Sudan. Eneo lake ni kilomita za mraba 158,355 na mwaka 2010 wakazi milioni 2.5 zilihesabiwa hapa. Mji mkuu ni Kadugli. Sehemu kubwa ya mashariki ya jimbo ni Milima ya Nuba ambayo ni nyumbani ya Wanuba. Jamii:Majimbo ya Sudan Jamii:Kordofan Kusini
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kordofan_Kusini
| null | 8,219
|
Kiwadjabangayi
|
'''Kiwadjabangayi''' kilikuwa lugha ya Kipama-Nyungan nchini Australia iliyozungumzwa na Wawadjabangayi katika jimbo la Queensland. Hakuna wasemaji ambao wamebaki kuongea lugha hii, yaani lugha ya Kiwadjabangayi ilitoweka. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiwadjabangayi kiko katika kundi la Kimariki. *[http://multitree.org/codes/wdy lugha ya Kiwadjabangayi kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/wdy makala za OLAC kuhusu Kiwadjabangayi] *[http://www.ethnologue.com/language/wdy lugha ya Kiwadjabangayi katika Ethnologue] Jamii:Lugha za Australia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiwadjabangayi
| null | 23,746
|
Kisama
|
'''Kisama''' ni lugha ya Kibantu nchini Angola inayozungumzwa na Wasama. Mwaka wa [] idadi ya wasemaji wa Kisama imehesabiwa kuwa watu 24,200. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kisama iko katika kundi la H20. *[http://multitree.org/codes/smd lugha ya Kisama kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/smd makala za OLAC kuhusu Kisama] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/sama1300 lugha ya Kisama katika Glottolog] *http://www.ethnologue.com/language/smd Jamii:Lugha za Angola Jamii:Lugha za Kibantu
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kisama
| null | 13,494
|
Ahmed Ammi
|
thumbnail|right|200px| Ahmed Ammi '''Ahmed Ammi''' (; alizaliwa 19 Januari []) ni mchezaji wa soka wa Kimoroko-Kiholanzi anayecheza kama beki wa kulia. Kwa sasa anacheza katika klabu ya Kiholanzi ya SC Irene ambayo ni ya kiwango cha wachezaji wasio wa kulipwa. Jamii:Wachezaji mpira wa Moroko Jamii:Wachezaji mpira wa Uholanzi Jamii:Waliozaliwa 1981 Jamii:Watu walio hai
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ahmed_Ammi
| null | 44,666
|
Umri wa kuacha shule
|
'''Umri wa kuacha shule''' ni umri wa chini ambao mtu anaruhusiwa kisheria kusitisha kuhudhuria katika taasisi ya elimu ya lazima. Nchi nyingi zina umri wa kuacha shule ambao umewekwa sawa na umri wao wa chini wa kuajiriwa wa wakati wote, na hivyo kuruhusu mpito mzuri kutoka kwa elimu hadi ajira, wakati chache zimeweka chini ya umri ambao mtu anaruhusiwa kuajiriwa. Jamii:Haki za watoto Jamii:Elimu Jamii:umri Jamii:sheria
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Umri_wa_kuacha_shule
| null | 43,216
|
Kiuda
|
'''Kiuda''' ni lugha ya Kiniger-Kongo nchini Nigeria inayozungumzwa na Wauda. Mwaka wa 1988 idadi ya wasemaji wa Kiuda imehesabiwa kuwa watu 10,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiuda iko katika kundi la Cross River. *[http://multitree.org/codes/uda lugha ya Kiuda kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/uda makala za OLAC kuhusu Kiuda] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/udaa1238 lugha ya Kiuda katika Glottolog] *http://www.ethnologue.com/language/uda Jamii:Lugha za Nigeria
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiuda
| null | 15,124
|
Don Cartagena (wimbo)
|
'''"Don Cartagena"''' ni wimbo kutoka katika albamu ya Fat Joe ya Don Cartagena. Wimbo umeshirikisha P. Diddy kwenye upande wa kiitikio, ambaye humu kaimba kiitikio tu (lakini pia hakuonekana ndani yake video yake). Wimbo umetayarishwa na mtayarishaji machachari - Younglord. Wimbo umebahatika kushika nafasi ya #21 kwenye chati za Hot Rap Singles na nafasi ya #40 kwenye chati za Hot R&B/Hip-Hop Singles & Tracks. Muziki wa video wa wimbo huu unaanza na watoto wengi wakiendesha baiskeli barabarani huku ikioneshwa matairi ya baiskeli yanageuka kuwa matairi ya gari. Wakati huohuo anasikika Fat Joe akizingumzia habari za utotoni mwake jinsi walivyoweza kuanzisha kijikikundi kidogo cha shule - pia akihadithia kwamba walikuwa na baba yao aliokuwa akisadia kwa kila walichokitaka, lakini pia kulikuwa na njemba moja aliyeitwa Santiago alikuwa akiogopeka sana. Kwani ukimuona huyo bwana, basi ujue maisha si mazuri tena. Baadaye Fat anaonekana kurudisha kisasi kwa yule bwana Santiago na kupewa heshima kubwa kwa marafiki zake waliokuwa wakihofia mtandao wa Santiago. Pichani, anaonekana mfuasi mmoja mmoja anauawa wa Santiago - na mwishowe yeye mwenyewe Santiago. {| class="wikitable" !align="left"|Chati !align="left"|Nafasi |- |align="left"|Hot Rap Singles |align="left"|# 21 |- |align="left"|Hot R&B/Hip-Hop Singles & Tracks |align="left"|# 40 |} * Jamii:Nyimbo za 1998 Jamii:Nyimbo za Fat Joe Jamii:Nyimbo zilizotayarishwa na Younglord
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Don_Cartagena_(wimbo)
| null | 11,986
|
Efate
|
'''Efate''' ni kisiwa cha Vanuatu. Kiko upande wa kusini wa kisiwa cha Epi. Eneo la kisiwa ni 899 km². Mji mkubwa kabisa kisiwani huitwa Port Vila ambayo pia ni mji mkuu wa Vanuatu. Mwaka wa 2009 idadi ya watu kisiwani imehesabiwa kuwa 65,829. Lugha za asili ambazo huzungumzwa kisiwani kwa Efate ni Kiefate-Kaskazini, Kiefate-Kusini na Kieton. Jamii:Visiwa vya Vanuatu
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Efate
| null | 18,154
|
Tyler Shaw
|
thumb|Tyler Shaw '''Tyler Shaw''' (alizaliwa 8 Aprili, []) ni mwimbaji na muigizaji kutoka Kanada. Baada ya kushinda "MuchMusic Coca-Cola Covers Contest 2012" iliyoandaliwa na chaneli ya muziki ya Kanada ya MuchMusic, alitoa wimbo wake wa kwanza, "Kiss Goodnight", kupitia Sony Music mnamo Desemba 2012. Wimbo huo ulithibitishwa Dhahabu na muziki wa Kanada mnamo Aprili 2013. Jamii:Waimbaji wa Kanada
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tyler_Shaw
| null | 51,502
|
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
|
thumb|Mahakama ya Kimataifa ya Jinai thumb|right|Rais wa Sudan Omar al-Bashir ambaye anatakiwa kufikishwa mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai kwa ukiukaji wa haki za kibinadamu katika eneo la Darfur '''Mahakama ya Kimataifa ya Jinai''' (Kifaransa: ''Cour Pénale Internationale''; Kiing. '''International Criminal Court''' ambayo kawaida hujulikana kama '''ICC''' au '''ICCt''' ni mahakama ya kudumu ya kuwashtaki watu kwa mauaji ya kimbari, hatia dhidi ya ubinadamu, hatia za kivita na hatia ya ushambulizi (ingawa kwa sasa haiwezi kuwashtaki watu kwa hatia ya ushambulizi). Makao makuu yako Den Haag (Uholanzi). Ni tofauti na Mahakama Kuu ya Kimataifa inayoamua ugomvi kati ya nchi kama pande zote zinakubali kupeleka kesi huko. Mahakama haya yaliundwa mnamo tarehe Mosi Julai, mwaka wa 2000 - tarehe ambapo Mkataba wa Roma wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ulipata nguvu za kisheria. Kufikia mwaka wa 2010, nchi 110 ni wanachama wa mahakama hayo, na nchi zingine 38 zimetia sahini lakini hazijapitisha kisheria Mkataba wa Roma. Hata hivyo, mataifa mengi, ikiwemo Uchina, Uhindi, Urusi na Marekani zinazidi kuyakosoa mahakama hayo na hazijajiunga nayo. Hadi 2011 mahakama imepokea malalamiko kuhusu kesi katika nchi 139; hadi Machi 2011 utafiti rasmi umefungulia kwa kesi 6, zote katika Afrika: Uganda Kaskazini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Darfur (Sudan), Kenya na Libya. Kesi tatu zilipelekwa na nchi ambazo ni wanachama wa ICC (Uganda, Kongo na Jamhuri ya Afrika ya Kati), mbili na Baraza la Usalama la UM (Darfur na Libya) na moja kufuatana na azimio la mshtaki mkuu wa ICC (Kenya). Jamii:Sheria Jamii:Mashirika
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mahakama_ya_Kimataifa_ya_Jinai
| null | 10,415
|
Kibodo (Afrika ya Kati)
|
'''Kibodo''' ni lugha ya Kibantu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati inayozungumzwa na Wabodo. Mwaka wa 1996 idadi ya wasemaji wa Kibodo imehesabiwa kuwa watu 15 tu. Kwa hiyo lugha hiyo imekaribia kutoweka kabisa. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kibodo iko katika kundi la D30. *[http://multitree.org/codes/boy lugha ya Kibodo kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/boy makala za OLAC kuhusu Kibodo] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/bodo1272 lugha ya Kibodo katika Glottolog] *http://www.ethnologue.com/language/boy Jamii:Lugha za Jamhuri ya Afrika ya Kati
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kibodo_(Afrika_ya_Kati)
| null | 14,560
|
Kiwarlmanpa
|
'''Kiwarlmanpa''' ni lugha ya Kipama-Nyungan nchini Australia inayozungumzwa na Wawarlmanpa katika jimbo la Northern Territory. Katika sensa ya mwaka 2006, kulikuwa na wasemaji wa Kiwarlmanpa 47 tu, na lugha imekaribia kutoweka kabisa hivi karibuni. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiwarlmanpa kiko katika kundi la Kipama-Nyungan cha Kusini-Magharibi. *[http://multitree.org/codes/wrl lugha ya Kiwarlmanpa kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/wrl makala za OLAC kuhusu Kiwarlmanpa] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/warl1255 lugha ya Kiwarlmanpa katika Glottolog] *[http://www.ethnologue.com/language/wrl lugha ya Kiwarlmanpa katika Ethnologue] Jamii:Lugha za Australia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiwarlmanpa
| null | 23,907
|
Joel Okuyo Atiku
|
'''Okuyo Joel Atiku Prynce''' ni mwigizaji wa Uganda, , mpiga picha na mhadhiri katika Uganda Christian University ambapo alihitimu na shahada ya kazi ya jamii na utawala wa jamii (BSWSA) pamoja na Chuo Kikuu cha Makerer, Kampasi mbili bora nchini Uganda. Mafanikio yake ya uigizaji wa filamu yalikuja wakati alipigwa kama kuzaliwa kwa Ibilisi katika mkurugenzi wa Uganda Matt Bish wa Film, Battle of the Souls [], Sinema maarufu Ugawood. Ilitokana na hadithi ya kweli ya kaka wa mkurugenzi, Mtangazaji wa Redio ya KFM Roger Mugisha.Prynce pia ni Rais wa kampuni yake mwenyewe The Lhynnq-X, Inc. Ni Mzaliwa wa Arua, tarehe 4 Desemba 1983 kawa mwanandoa Wagugbara na Lugbara, marehemu Luteni Kanali Gabriel Francis Atiku na Yema Drakuru Atiku, jukumu lake la kwanza villain lilimshinda mara tano za kimataifa pamoja na mwigizaji bora wa kusaidia katika tamasha la filamu la Balafon huko Bari, Italia (2008) na mwigizaji bora wa [] katika kuunga jukumu la African Movie Academy Awards (AMAA) huko Lagos , Nigeria.Tuzo zingine ni pamoja na Mwigizaji Bora katika Kijiji cha Ubuntu, Colorado (USA) mnamo 2010 na 2011 Zanzibar International Film Festival [ZIFF] huko Tanzania. Gazeti la Uganda '' The Observer '' lilimtaja Brad Pitt wa Okuyo Africa. Mama yake anakumbuka kwamba Joel alianza kuigiza kwa mtindo wa baba yake wa kutembea akiwa na umri wa miaka 4 pamoja na vitu alivyoangalia kwenye Runinga au alivyoona shuleni. Kufikia darasa la Tano, alikuwa ameshinda tuzo yake ya kwanza na aliendelea kuigiza wakati wote wa uzoefu wake wa shule.Okuyo pia alijiunga na MITG (Music & Instrumental Training Group), Kikundi cha Maigizo cha Arua ambacho kilitetea Umoja wa Ulaya, Programu za kuingilia UKIMWI katika eneo la Magharibi mwa Nile.Joel ameigiza filamu na maigizo mengi, ya ndani na ya kimataifa pamoja na kufanya kazi na wakurugenzi wa kiwango cha ulimwengu kama Michael Landon, Jr., Gabriel Range, Adrian McFarlane, Ruman Kudwai, Yuval Shefferman na mwenzake Matt Bish (Jina kamili: Matthew Bishanga). Joel alicheza majukumu katika filamu kama "State Research Bureau (S.R.B)" pamoja na Mfululizo wa Runinga kama "Locked Up Abroad", "Raised Wild" na "Lost in Africa". Filamu Maisha za Filamu za Maisha alizocheza baada ya mafunzo katika chuo cha filamu cha Mira Nair ni pamoja na '' On Time (2008) '' iliyoongozwa na Patricia Olwoch, "Looserpool", "Live Joseph" na "Estranged" (ambapo alicheza jukumu la kuongoza) iliyoongozwa na Sandra Kosse. Kazi zingine ambazo ameangazia ni pamoja na "Fruits of Love", "Journey to Jamaa" as Lucky, "Haunted Souls" and "A Good Catholic Girl" iliyoongozwa na Matt Bish (ambayo ilijumuishwa katika "Africa First: Volume Two", hadithi ya filamu fupi tano kutoka kwa watengenezaji filamu mpya wa Afrika). Alikuwa uso wa BlackBerry Curve (MTN Uganda mwaka []. Halafu mnamo [], alikua modeli ya runway katika usiku wa mitindo wa V.I.P huko Lagos, Nigeria. Amefanya kazi kama mfano katika Vanity Models (Verona, Italia) na Uganda's Gorgeous Fashions. Uso wa Joel pia unaonekana katika SAB Miller, Runinga, Bango & Magazeti ya mtandaoni kwa bidhaa za bia kama vile Stone Lager huko Ghana, Safari Lager Tanzania na Nile Special Lager katika nchi ya nyumbani, yote iliyoongozwa na Mark Lawrie kwa The Videolounge. Matangazo mengine ya Runinga ni pamoja na Warid Telecom (Kongo Brazzaville) iliyoongozwa na Steve Jean; Warid (Uganda), Benki ya Stanbic na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins kilichoongozwa na Carolyn Kamya pamoja na Benki ya Uganda iliyoongozwa na Matt Bish. Alikuwa wa kiume wa kwanza kutokea katika sehemu ya "Taa za Wanawake wa Kiafrika" katika 'Taa Zote za' mnamo []. Joel alionekana kwenye promo ya "Upendo Makanika (safu ya Runinga)", moja wapo ya programu za kwanza zilizorushwa kwenye Pearl Magic ambazo zilipitia dijiti kwenye GOtv kuanzia Jumatatu 1 Oktoba []. Okuyo ametoa kipaji chake kama sauti inayounga mkono uzalishaji wa redio kama "Mako Meere" iliyoongozwa na Patricia Olwoch (kwa Mifumi) na "Rock Point" na Albert Mwesige (Audio Central). Aliwahi kufanya kazi kwa Bob FM pia. Amecheza katika maonyesho ya ukumbi wa michezo kama "Just You Me & the Silence" iliyoongozwa na Judith Adong kwa kushirikiana na Alfajiri Productions. Mnamo [], alishiriki kama Lokil kuandaa tamthilia ya jukwaa inayoitwa "Strings" ambayo itafanywa kwanza mnamo 22 Novemba. Okuyo alipata ukosoaji mbaya, hata kutoka kwa marafiki kwa kuigiza "The River and the Mountain", mchezo ambao sehemu yake Baraza la Vyombo vya Habari nchini Uganda lilisema "inakuza vitendo vya ushoga". Imeandikwa na mshairi aliyesomea Oxford Beau Hopkins akishirikiana na David Cecil, mtayarishaji wa Uingereza na meneja wa Tilapia (Kituo cha Utamaduni ambapo mchezo huo ulichezwa kwa wiki moja hadi 23 Agosti []), ilionekana kuwa kinyume na sheria, kanuni za kitamaduni na maadili. ya Uganda kwa hivyo kukamatwa kwa Cecil mnamo 6 Septemba []. Katika mchezo huo, Okuyo anacheza Samson, mmiliki wa kiwanda cha ushoga aliyeuawa na wafanyikazi wake baada ya kuchochewa na wachungaji wenye msimamo mkali. Okuyo alishtakiwa kwa "kufadhiliwa na vikundi vya kushawishi mashoga", lakini akajibu, "Siko katika utetezi wa mashoga. usihukumu, kutenga, madhara au kuua wengine." Joel anafurahiya kuchora (Sanaa), mitindo, uigizaji wa filamu, modeli, kukutana na marafiki wapya, misaada ya kibinadamu, kucheza mpira wa kikapu, gitaa, kuogelea, uvuvi, kusoma, kupika, kuandika na kusafiri. Mnamo Machi 2020, alijiingiza kwa msanii wa dancehall Cindy Sanyu ambaye alikuwa amewahi kufanya naye kazi filamu mbili November Tear na Bella (filamu ya 2017) | Bella. Video za muziki Vipindi vya Okuyo vilipatikana katika "Boo" ya Priscilla Kalibala, wimbo wa asili wa "Battle of the Souls" pamoja na "Watu Huru" iliyoandikwa na kutumbuizwa na Terry De Vos kama wimbo wa asili kwa "State Research Bureau". Anaangazia pia video ya muziki ya "Kibulamu" ya Winnie Nwagi kama mpenzi wake. Mwimbaji anamwambia kuwa uhusiano wao hauna vitu kadhaa vya kimapenzi, kwa hivyo wanahitaji kwenda kwa njia zao tofauti. Winnie hata anafunga begi lake kuondoka. Mwishowe, wanapatanishaw lakini wakiwa wamekaa mezani, pakiti mbili za kondomu zinaanguka kutoka kwenye kanzu ya Okuyo na video hiyo inafifia. Anaangazia pia "Ready To Leave" na Abasa. Prynce kupitia kampuni yake ya utengenezaji ametengeneza video za muziki kwa wasanii kama Cindy pamoja na "Whine Yo Waist", "Sunset" na "Kiki", n.k. Jamii: Waigizaji Filamu wa Uganda
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Joel_Okuyo_Atiku
| null | 33,708
|
Giovanni Romano
|
'''Giovanni Romano''' (alifariki []) alikuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki aliyewahi kuwa Askofu wa Terni ([]–[]). Romano alipewa daraja ya upadre katika Shirika la Wahubiri (Order of Preachers). Mnamo 1481, aliteuliwa na Papa Sixtus IV kuwa Askofu wa Terni, akihudumu hadi kifo chake mnamo []. ''(in Latin)'' Jamii:Watu wa Italia Jamii:Maaskofu Wakatoliki Jamii:Waliofariki 1485
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Giovanni_Romano
| null | 55,164
|
Pernilla Larsson
|
thumb|Pernilla Larsson mnamo 2012 '''Pernilla Larsson''' (alizaliwa 18 Septemba, []) ni mwamuzi wa mpira wa miguu kutoka nchini Uswidi. Amekuwa kwenye Orodha ya FIFA ya waamuzi wanawake wa kimataifa tangu mwaka 2010. Alichaguliwa na FIFA kuchezesha mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA la Wanawake mwaka 2015. Mnamo 2014, alikua mwamuzi bora mwanamke wa Shirikisho la Soka na Takwimu Duniani (IFFHS). Pia Larsson alitajwa kuwa mwamuzi mwanamke wa mwaka wa Uswidi katika Fotbollsgalan mwaka 2014. Mwaka huo huo, aliwahi kuwa mwamuzi katika Kombe la Dunia la FIFA la Wanawake chini ya miaka 17 mwaka 2014. {{Mbegu-mtu Jamii:Waliozaliwa 1976 Jamii:Watu walio hai Jamii:Wanamichezo wa Uswidi
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Pernilla_Larsson
| null | 43,857
|
William Luther Pierce
|
'''William Luther Pierce III''' (11 Septemba [] – 23 Julai []) alikuwa mfuasi wa itikadi za neo-Nazi, mpenda ubaguzi wa rangi wa kizungu, na mwanaharakati wa siasa za mrengo wa kulia wa Marekani. Kwa zaidi ya miaka 30, alikuwa mmoja wa watu wenye ushawishi mkubwa katika harakati za wazungu wenye siasa kali za utaifa. Kwa taaluma, alikuwa mwanafizikia na mwandishi wa riwaya The Turner Diaries na Hunter, akitumia jina la kalamu Andrew Macdonald. Riwaya yake ya kwanza ilihamasisha uhalifu kadhaa wa chuki, ikiwa ni pamoja na shambulio la bomu la Oklahoma City mwaka 1995. Pierce alianzisha shirika la kitaifa la wazungu wenye siasa kali, National Alliance, ambalo aliliongoza kwa takriban miaka 30. thumb|Pierce akiwa amevalia sare ya chuo cha kijeshi cha shule ya upili Alizaliwa Atlanta katika familia ya Kipresbiteri yenye asili ya Scotch-Irish na Kiingereza. Pierce alikuwa mzao wa Thomas H. Watts, gavana wa Alabama na Mwanasheria Mkuu wa Confederate States of America wakati wa Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Marekani. Alimaliza shule ya sekondari mwaka 1952, kisha akapata shahada ya fizikia kutoka Rice University mwaka 1955 na baadaye shahada ya uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Colorado Boulder mwaka 1962. Alianza kazi kama profesa msaidizi wa fizikia katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Oregon mwaka huo huo. Mwaka 1965, aliacha nafasi yake ya kufundisha katika chuo hicho na kuwa mtafiti mwandamizi katika kampuni ya anga ya Pratt & Whitney huko Connecticut. Mwaka 1966, alihamia eneo la Washington, D.C. na akawa mshirika wa George Lincoln Rockwell, mwanzilishi wa American Nazi Party, ambaye aliuawa mwaka 1967. Baadaye, Pierce alikua kiongozi mwenza wa National Youth Alliance, ambayo iligawanyika mwaka 1974, na kusababisha Pierce kuanzisha National Alliance. Riwaya yake ya The Turner Diaries (1978) inaelezea mapinduzi yenye ghasia nchini Marekani, yakifuatiwa na vita vya dunia na maangamizi ya jamii zisizo za kizungu. Riwaya yake nyingine, Hunter (1989), inasimulia hadithi ya muuaji wa kibaguzi anayefanya mauaji peke yake. Mwaka 1985, Pierce alihamishia makao makuu ya National Alliance huko Hillsboro, West Virginia, ambako alianzisha Cosmotheist Community Church ili kupata msamaha wa kodi kwa shirika lake. Aliendelea kuendesha kipindi cha kila wiki American Dissident Voices, kuchapisha jarida la ndani la National Alliance Bulletin (awali likiitwa Action), na kusimamia machapisho yake kama vile jarida National Vanguard (awali likiitwa Attack!), Free Speech, na Resistance. Aidha, alisimamia uchapishaji wa vitabu kupitia kampuni yake National Vanguard Books, Inc., pamoja na lebo ya muziki wa siasa kali za wazungu, Resistance Records. Wakati wa kifo chake mwaka 2002, National Alliance ilikuwa ikipata mapato ya zaidi ya dola milioni 1 kwa mwaka, ikiwa na zaidi ya wanachama 1,500 na wafanyakazi wa kitaifa 17 waliolipwa mshahara wa kudumu. Baada ya kifo chake, shirika hilo lilikumbwa na migogoro ya ndani na kuporomoka. '''Maisha ya Mapema na Elimu''' William Luther Pierce III alizaliwa Atlanta, Georgia. Alikuwa mtoto wa William Luther Pierce Jr. na Marguerite Farrell, na familia yake ya Kipresbiteri ilikuwa na asili ya Scotch-Irish na Kiingereza. Ndugu mdogo wa Pierce, Flournoy Sanders, ambaye alikuwa mhandisi, alisaidia Pierce katika shughuli zake za kisiasa. Baba yake Pierce alizaliwa huko Christiansburg, Virginia mwaka 1892. Mama yake alizaliwa huko Richland, Georgia mwaka 1910, na familia yake ilikuwa sehemu ya aristokrasi ya Old South, ikiwa ni wazao wa Thomas H. Watts, gavana wa Alabama na mwanasheria mkuu wa Confederate States of America. Baada ya Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Marekani, familia ilishi maisha ya tabaka la kati. Baba yake Pierce aliwahi kutumikia kama mwakilishi wa serikali kwenye meli za mizigo zinazosafiri baharini na alituma ripoti zake kwa Washington, D.C.; baadaye alikua meneja wa shirika la bima lakini aliuawa katika ajali ya gari mwaka 1943. Baada ya kifo cha baba yake, familia ilihamia Montgomery, Alabama, na baadaye kwenda Dallas, Texas. Pierce alifanya vizuri shuleni; miaka miwili ya mwisho ya shule ya sekondari alizihudhuria katika Allen Military Academy huko Bryan, Texas. Alikuwa na maslahi katika roketi za mfano, kemia, redio, umeme, na kusoma fasihi ya sayansi. Accessed on Vimeo. Accessed on Vimeo. Baada ya kumaliza shule ya kijeshi mwaka 1951, Pierce alifanya kazi kwa muda mfupi katika shamba la mafuta kama roustabout (mfanyakazi wa shambani). Aliumia wakati bomba lenye kipenyo cha inchi nne (10 cm) lilipanguka juu ya mkono wake, na alikamilisha majira ya kiangazi akifanya kazi kama muuzaji wa viatu. Pierce alipata ufadhili wa masomo kujiunga na Rice University huko Houston. Alimaliza masomo yake katika chuo hicho mwaka 1955 akiwa na shahada ya fizikia. Alifanya kazi katika Los Alamos National Laboratory kabla ya kujiunga na shule ya juu, awali katika Caltech mwaka 1955–56. Katika Chuo Kikuu cha Colorado huko Boulder, Colorado, alipata shahada ya uzamili na uzamivu mwaka 1962. Alifundisha fizikia kama profesa msaidizi katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Oregon kutoka 1962 hadi 1965. Jamii:Waliozaliwa 1933 Jamii:Waliofariki 2002 Jamii:Wanasiasa wa Marekani Jamii:Wanaharakati wa Marekani Jamii:Feminism and Folklore 2025 in Tanzania
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/William_Luther_Pierce
| null | 55,553
|
Angkor Wat
|
thumb|300px|Sura ya hekalu kuu 300px|thumbnail|Angkor Wat inavyoonekana kutoka hewani thumbnail|300px|[[Sanamu ya mchezaji wa hekaluni]] '''Angkor Wat''' ni hekalu kubwa katika mkoa wa Angkor, Kamboja. Hekalu hilo lilijengwa katika karne ya 12 kwa amri ya mfalme Suryavarman II kama kitovu cha mji mkuu wake. Ni hekalu la Kihindu kubwa zaidi duniani. Limetangazwa na Unesco kuwa sehemu ya urithi wa dunia. Ibada katika hekalu zilibadilihswa baadaye kuwa za Kibuddha na leo hii imekuwa ishara ya taifa la Kamboja na sehemu ya nembo lake. Hekalu la Angkor Wat ni sehemu ya jumla ya majengo mengine mengi ya kidini ya Angkor, iliyokuwa eneo la miji mikuu ya wafalme wa Khmer kama vile Angkor Wat, Angkor Tom na mengine katika karne ya 9 hadi karne ya 15. Hakuna mabaki ya majengo nje ya mahekalu kwa sababu Wakhmer walitumia mawe kwa majengo ya kidini pekee. Hekalu liko takriban km 240 upande wa kaskazini-magharibi wa mji mkuu Phnom Penh. Eneo lote la hekalu la Angkor Wat lina urefu wa km 1.5 na upana wa km 1.3. Lote limezungukwa na mfereji wa maji mwenye upana wa mita 190. Kwa hiyo hekalu liko kwenye kisiwa kilichotengenezwa na binadamu. Mawe makubwa ya ujenzi yalisafirishwa kwenye maji kwa njia ya boya. Mawe yamenyoshwa kwa umakini na kuunganishwa bila sementi na bila kuonyesha mapengo. Katikati ya kisiwa kuna hekalu kuu lenye minara 5 inayoitwa prasat. Mnara mkubwa una kimo cha mita 65. Kuta za hekalu zimejaa sanamu zilizochongwa katika jiwe. Zinaonyesha hasa wachezaji wa kike wakati wa kucheza katika ibada mbele ya miungu. Sanamu hizo zimechongwa kila moja kwa namna ya pekee, hakuna mbili zilizo sawa. Kwenye ghorofa la juu kuna kanda za picha za kuchongwa katika jiwe zinazoonyesha masimulizi ya mashairi matakatifu ya Wahindu yanayoitwa Ramayana na Mahabharata. Chanzo cha ujenzi wa miji na hekalu kilikuwa azimio la wafalme wa Khmer katika karne ya 9 la kutengeneza malambo na mifereji ya umwagiliaji katika eneo la Angkor. [[Miundombinu] hiyo iliweka msingi kwa kilimo cha mpunga chenye mazao kadhaa kila mwaka na kuleta idadi kubwa ya watu pamoja na utajiri kwa nchi. Kwa njia hiyo milki ya Khmer ilikuwa dola lenye uwezo mkubwa katika Asia Kusini Magharibi lililoweza kujenga miji mikubwa yenye mahekalu ya ajabu. Mwaka [] mfalme Suryavarman II alianza kuwa mtawala wa Khmer hadi []. Alishinda vita kadhaa na kupanua eneo la milki. Alitengeneza upya mahekalu yaliyokuwepo na kuanzisha makazi mapya ya kifalme pamoja na hekalu kubwa la Angkor Wat. Alikabidhi hekalu kwa ibada ya mungu wa kihindu Vishnu. Wataalamu wanaona dalili ya kwamba hekalu hili lilikusudiwa kuwa baadaye pia hekalu la kaburi la mfalme huyu. Katika miaka ya baadaye eneo la Angkor ilivamiwa na maadui wa Khmer, kurudishwa tena chini ya milki yao na tangu mwaka [] mfalme Jayavarman VII alianzisha mji mkuu mpya wa Angkor Tom. Mfalme huyo alikuwa mfuasi wa Buddha, si tena mfuasi wa miungu ya Uhindu. Kwa hiyo hekalu kuu la Angkor Tom likawa hekalu la Kibuddha. Miaka iliyofuata ibada za Kihindu katika Angkor Wat zilififia na kuwa mahali pa Wabuddha. Katika karne ya 15 Wathai walivamia na kutwaa Kamboja na eneo la Angkor halikuwa tena mji mkuu. Lakini Angkor Wat iliendelea kutumiwa na wamonaki Wabuddha. Wakati ule hapakuwa tena na pesa ya kukarabati mahekalu, hivyo majengo mengi yalifunikwa na misitu minene. Angkor Wat ilihifadhiwa kutokana na mfereji mpana wa maji uliozuia uenezaji wa misitu. Tangu karne ya 17 wasafiri wa kwanza kutoka ng'ambo walifika Kamboja na kutembelea Angkor Wat. Wazungu wa karne ya 19 waliandika juu ya hekalu wakishangaa jinsi gani majengo mazuri namna hii yalijengwa katika nchi iliyokuwa maskini na katika hali duni wakati wao. http://www.cambodianview.com/documents/articles/Brief_Presentation.pdf Maelezo kwa watalii katika Angkor Wat * [http://www.autoriteapsara.org/en/angkor/temples_sites/temples/angkor_vat.html Angkor Wat - APSARA Authority Official Description] Jamii:Kamboja Jamii:Urithi wa Dunia Jamii:Uhindu Jamii:Ubuddha
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Angkor_Wat
| null | 16,838
|
David Rovics
|
'''David Stefan Rovics''' ( / ˈroʊ vɪks / ROH -viks ; ROH amezaliwa Aprili 10, []) ni mwimbaji/ mtunzi wa nyimbo wa Marekani. Muziki wake unahusu mada kama vile vita vya Iraq vya [], kupinga utandawazi, machafuko, na masuala ya haki za kijamii . Rovics amekuwa mkosoaji mkubwa wa Rais wa zamani George W. Bush, Chama cha Republican, John Kerry, na Chama cha Democratic. Rovics anakosoa sera za serikali ya Marekani na anadai kuwa "sera ya mambo ya nje ya serikali ya Marekani inawakilisha maslahi ya makampuni ya Marekani" na kwamba "serikali ya Marekani haipendi demokrasia ya ndani ya nchi au nje." Ingawa baadhi ya kazi za Rovics hazichapishwi, na nyingi zinasambazwa kibiashara, Rovics amefanya muziki wake wote uliorekodiwa upatikane bure kama faili za mp3 zinazoweza kupakuliwa. Anahimiza usambazaji wa bure wa kazi yake kwa njia zote zisizo za faida ili kukuza kazi yake na kueneza ujumbe wa kisiasa, na anazungumza dhidi ya tovuti au programu kama iTunes ambazo hutoza pesa kwa kupakua nyimbo zake. Rovics pia ametetea uimbaji wa nyimbo zake kwenye maandamano na amefanya muziki wake na mashairi kupatikana kwa kupakuliwa mitandaoni. David Rovics alizaliwa huko New York City . Familia yake ilihamia Wilton, Connecticut alipokuwa mdogo. Rovics alitiwa msukumo wa kisiasa wakati wa ujana wake kutokana na uzoefu wake na watu wenye mwelekeo wa kihafidhina, mazingira ya Kikristo ya mji wake wa asili. Wazazi wake, wanamuziki wa classical na waelimishaji, walikuwa huru katika mtazamo wao. Labda kwa sababu hii, wakati katika ujana wake Rovics alipata ushwishi wa kufuatilia mambo ya nyuklia duniani . Amejielezea kuwa " Myahudi anayepinga Uzayuni kutoka New York". Mnamo 1985, Rovics alijiandikisha katika Chuo cha Earlham huko Richmond, Indiana, lakini aliacha shule na kuhamia Berkeley, California. Alifanya kazi i kama vile mpishi, barista, katibu na mpiga chapa, huku akifuatilia masilahi yake ya muziki kama mwigizaji wa barabarani na katika vilabu vidogo na baa. Alijizatiti katika mrengo wa kushoto na akawasiliana na watunzi wengine wa nyimbo na waigizaji na kufanya nao maongezi ya chini chini kulingana na masuala mazima ya itikadi zao kisiasa . Kufikia mapema miaka ya 1990 alikuwa akipendelea kusafiri katika njia za chini ya ardhi za Boston. Jamii:Watu walio hai Jamii:Waliozaliwa 1967 Jamii:Wanamuziki wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/David_Rovics
| null | 43,844
|
Val McDermid
|
'''Valarie McDermid''' (alizaliwa 4 Juni []) ni mwandishi wa uhalifu wa Kiskoti, anayejulikana zaidi kwa mfululizo wa riwaya zinazoshirikiana na daktari wa saikolojia ya kimatibabu Dr. Tony Hill na washirika wake katika idara ya polisi. Kazi yake inachukuliwa kuwa sehemu ya aina ndogo inayojulikana kama Tartan Noir. Mfululizo huu ulibadilishwa kwa televisheni, ukiendeshwa kutoka [] hadi [], na kujulikana kama "''Wire in the Blood''." Pia alikuwa na mfululizo wa pili, unaojulikana kama Karen Pirie, uliobadilishwa kutoka kwa vitabu vyake kadhaa vinavyomudu shirikiana na mhusika huyo. McDermid anatoka katika familia ya wafanyakazi huko Fife. Alisoma Kiingereza katika Chuo cha St Hilda, Oxford, ambapo alikuwa mwanafunzi wa kwanza kukubaliwa kutoka shule ya serikali ya Kiskoti. Baada ya kuhitimu, alikua mwandishi wa habari na akaanza kazi yake ya fasihi kama mwandishi wa tamthilia. Mafanikio yake ya kwanza kama mwandishi wa riwaya, "''Report for Murder: The First Lindsay Gordon Mystery,''" yalichapishwa mnamo []. McDermid aliingizwa katika Klabu ya Uchunguzi yenye heshima mnamo 2000. Mnamo 2010 alishinda CWA Diamond Dagger kwa mchango wake wa maisha yote katika uandishi wa uhalifu katika lugha ya Kiingereza. Alipewa udaktari wa heshima na Chuo Kikuu cha Sunderland mnamo []. Yeye ni mwanzilishi mwenza wa Tamasha la Uandishi wa Uhalifu la Harrogate na Tuzo ya Riwaya ya Uhalifu ya Theakston's Old Peculier ya Mwaka, sehemu ya Tamasha za Kimataifa za Harrogate. Mnamo [] aliongoza timu ya wanafunzi wa zamani wa St Hilda kushinda Changamoto ya Chuo Kikuu cha Krismasi. Mnamo [], McDermid alichaguliwa kuwa Mshirika wa Jumuiya ya Kifalme ya Edinburgh, pamoja na Mshirika wa Jumuiya ya Kifalme ya Fasihi. Kazi za McDermid zinaangukia katika mifululizo mitano: - Lindsay Gordon (mwandishi wa habari) - Kate Brannigan (mpelelezi wa kibinafsi) - Tony Hill (daktari wa saikolojia ya kimatibabu) na DCI Carol Jordan - DCI Karen Pirie - Allie Burns (ripota wa uchunguzi) "The Mermaids Singing," kitabu cha kwanza katika mfululizo wa Hill/Jordan na Val McDermid, kilishinda Tuzo ya Dhahabu ya Jumuiya ya Waandishi wa Uhalifu kwa Riwaya Bora ya Uhalifu ya Mwaka. Mfululizo wa Hill/Jordan umebadilishwa kwa televisheni chini ya jina "Wire in the Blood," ukiigizwa na Robson Green na ulioendeshwa kutoka [] hadi []. Mfululizo mwingine ulibadilishwa kutoka kwa vitabu vya Val McDermid vinavyomudu shirikiana na Karen Pirie; mfululizo huo unaitwa "Karen Pirie." McDermid amesema kwamba mhusika wake Jacko Vance, mtu mashuhuri wa TV mwenye tamaa ya siri ya mateso, mauaji na wasichana wa chini ya umri, ambaye alimudu shirikiana katika "Wire in the Blood" na vitabu viwili vya baadaye, anatokana na uzoefu wake wa moja kwa moja wa kumudu hoji Jimmy Savile. Mbali na kuandika riwaya, McDermid anachangia katika magazeti kadhaa ya Uingereza na mara nyingi hutangaza kwenye BBC Radio 4 na BBC Radio Scotland. Riwaya zake, hasa mfululizo wa Tony Hill, zinajulikana kwa maelezo yao ya wazi ya jeuri na mateso. Mnamo [], McDermid alipokea Cartier Diamond Dagger kutoka Jumuiya ya Waandishi wa Uhalifu kwa "''mafanikio bora katika uwanja wa uandishi wa uhalifu.''" McDermid anachukulia kazi yake kuwa sehemu ya aina ya "Tartan Noir" ya hadithi za uhalifu za Kiskoti. Mnamo Agosti [], McDermid aliripoti kwamba mali ya Agatha Christie ilikuwa imetishia wachapishaji wake kwa hatua za kisheria ikiwa wangeita McDermid kama "Malkia wa Uhalifu." Walisema kwamba neno hilo lilikuwa na hakimiliki ya mali ya Christie. Jamii:Waliozaliwa 1955 Jamii:Waandishi wa Uskoti Jamii:Feminism and Folklore 2025 in Tanzania
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Val_McDermid
| null | 55,816
|
Kigezo:Kata za Wilaya ya Singida Mjini
|
{| class="toccolours" |- | 50px| ! width="100%" bgcolor="lightsteelblue" style="text-align: center;" | Kata za Wilaya ya Singida Mjini - Mkoa wa Singida - Tanzania | 50px| |- | colspan="3" align="center" | Ipembe | Kindai | Kisaki | Majengo | Mandewa | Minga | Misuna | Mitunduruni | Mtamaa | Mtipa | Mughanga | Mungumaji | Mwankoko | Uhamaka | Unyambwa | Unyamikumbi | Unyianga | Utemini |} Jamii:Vigezo vya wilaya za Tanzania|
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kigezo:Kata_za_Wilaya_ya_Singida_Mjini
| null | 6,751
|
Papa Klementi V
|
thumb|right|Papa Klementi V. '''Papa Klementi V''' ([] – 20 Aprili []) alikuwa Papa kuanzia tarehe 5 Juni/14 Novemba [] hadi kifo chakehttps://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father. Alitokea Villandraut, Ufaransahttps://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa ''Bertrand de Got''. Alimfuata Papa Benedikto XI akafuatwa na Papa Yohane XXII. *Orodha ya Mapapa *[http://www.newadvent.org/cathen/04020a.htm Kuhusu Papa Klementi V katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki] Jamii:Waliozaliwa 1264 Jamii:Waliofariki 1314 Jamii:Papa Jamii:Watu wa Ufaransa
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Papa_Klementi_V
| null | 3,047
|
Mariana Ba
|
'''Mariama Bâ''' (17 Aprili [] - 17 Agosti []) alikuwa mwandishi na mtetezi wa haki za wanawake wa Senegal, ambaye riwaya zake mbili za lugha ya Kifaransa zote zilitafsiriwa katika lugha zaidi ya kumi na mbili. Mariama Bâ ni mzaliwa wa mkoa wa Dakar, alilelewa na Mwislamu. Hisia zake za kuchanganyikiwa kuhusu hatima ya wanawake wa Afrika zinaonyeshwa katika riwaya yake ya kwanza, ''Une si longue lettre'' ([]; iliyotafsiriwa kwa Kiswahili kama ''Barua Ndefu Kama Hii''). Katika kazi hii ya nusu ya wasifu,Mariama Bâ anaonyesha huzuni na kujiuzulu kwa mwanamke ambaye lazima ashiriki maombolezo ya marehemu mumewe na mke wake wa pili, mdogo. Kitabu hiki kifupi kilitunukiwa Tuzo la kwanza la noma la Uchapishaji Barani Afrika mnamo mwaka []. Jamii:waliozaliwa 1929 Jamii:Waliofariki 1981 Jamii:waandishi wa Senegal Jamii:AWC GWEI
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mariana_Ba
| null | 47,673
|
Benjamin Margate
|
|mahala_pa_kuzaliwa=London, UK|kazi_yake=Founder of Online Biology Tutors|utaifa=Waingereza}} '''Benjamin Margate''' (alizaliwa London, Uingereza, 19 Machi 1989) ni mwandishi wa biolojia wa Uingereza, mkufunzi na mshauri wa elimu, na mwanzilishi wa Wakufunzi wa Baiolojia ya Mtandaoni mwenye Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya Biolojia kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham. Benjamin Margate ni mwandishi wa biolojia wa Uingereza, mwalimu, na mshauri wa elimu, akitumia BSc katika Sayansi za Kibiolojia kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham na zaidi ya miaka 10 ya utaalamu katika kuunda na kuratibu maudhui ya kina ya biolojia. Kazi yake inalenga kutoa blogu za elimu na rasilimali kwa wanafunzi wa biolojia na kuwezesha uunganisho na walimu wa kitaaluma. Akitambuliwa kwa maarifa yake ya kina na kujitolea kwa elimu ya biolojia, mchango wa Benjamin umekuwa jiwe la msingi kwa wanafunzi wanaotafuta kuimarisha uelewa wao wa somo. Shauku ya Benjamin kwa biolojia iliwashwa katika Shule ya Oratory ya London, London. Hamasa yake kwa sayansi ya maisha ilistawi katika mazingira yaliyolea udadisi na ubora wa kitaaluma. Benjamin aliendelea na safari yake ya kielimu katika shule ya sita ya Westminster City School, akifanya vizuri katika Biolojia, Kemia, na Hisabati. Tamaa yake ya uelewa wa kina ilimpeleka katika Chuo Kikuu cha Birmingham, ambapo alipata shahada ya kwanza ya heshima katika Sayansi za Kibiolojia, ikiweka jukwaa kwa mchango wake wa baadaye katika uwanja wa biolojia. Kwa msingi uliojikita kwa kina katika ubora wa kielimu na shauku kwa elimu, Benjamin alianzisha Online Biology Tutors UK. Ameandika mamia ya makala katika vyanzo mbalimbali na yuko katika mchakato wa kuandika kitabu 'GCSE Biology Student Revision Guide for Exams in AQA, CCEA, OCR and Edexcel. Juhudi zake zinapanuka hadi podcast yenye mada ya biolojia, ikitajirisha mazingira ya elimu na maudhui yanayoziba pengo la uelewa na kukuza thamani kubwa kwa biolojia. Nje ya majukumu yake ya kitaaluma, Benjamin anafurahia kuchunguza asili kupitia upigaji picha, akikamata ugumu na uzuri wa dunia ya asili. Ni mchangiaji hai katika Jumba la Makumbusho la Historia Asilia, akichangia muda wake na utaalamu kusonga mbele elimu ya umma na thamani ya biolojia. Benjamin ni msomaji mkubwa wa sayansi ya kubuni, akipata mifano na msukumo kwa kazi yake katika uchunguzi wa kispekulativi wa sayansi na teknolojia. Zaidi ya hayo, anajihusisha na ufugaji nyuki mijini, mwendelezo wa kujitolea kwake kwa biolojia na juhudi za uhifadhi, zikisisitiza umuhimu wa bioanuai na ulezi wa mazingira. Mtazamo wa Benjamin kwa kufundisha ni binafsi na maalum, ukijidhihirisha katika mafanikio ya zaidi ya wanafunzi 5,000 chini ya mwongozo wake. Kazi yake ya kina, mtandaoni na nje ya mtandao, katika uwanja wa elimu ya biolojia, inamweka kama mtu muhimu katika uwanja, akisonga mbele uelewa na thamani ya biolojia miongoni mwa wanafunzi na wapenzi sawa. Jamii:wanabiolojia wa Uingereza
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Benjamin_Margate
| null | 46,119
|
Kikwama
|
'''Kikwama''' ni lugha ya Kinilo-Sahara nchini Ethiopia inayozungumzwa na Wakwama. Mwaka wa 1982 idadi ya wasemaji wa Kikwama imehesabiwa kuwa watu 15,000. Pia kuna kijiji kimoja nchini Sudan cha wasemaji wa Kikwama. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kikwama iko katika kundi la Kikomuz. *[http://multitree.org/codes/kmq lugha ya Kikwama kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/kmq makala za OLAC kuhusu Kikwama] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/kwam1249 lugha ya Kikwama katika Glottolog] *http://www.ethnologue.com/language/kmq Jamii:Lugha za Ethiopia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kikwama
| null | 16,510
|
Tuzo za Muziki za Kisima
|
'''Tuzo za Muziki za Kisima''' ni programu ya kila mwaka ya tuzo inayotambua vipaji vya muziki katika Afrika Mashariki.Licha ya kuwa na msingi wa Kenya, mpango huu huwatunuku wasanii kutoka nchi mbalimbali, hasa Kenya, Uganda na Tanzania, na hushirikisha aina mbalimbali za muziki. '''Tuzo za Kisima''' zilizopewa jina la Kiswahili la "vizuri" zilianzishwa na '''Pete Odera''' na Tedd Josiah mnamo []. Mpango huu hapo awali ulilenga kutambua mafanikio bora katika sanaa ya uigizaji na nyanja zinazohusiana kama vile elimu na biashara, na ulifanyika kenya katika ukumbi wa michezo wa Braeburn wa Nairobi. Mchakato huu uliendelea kila mwaka huku tuzo zikifanyika katika Mkahawa wa Carnivore, hata hivyo mwaka wa [] mpango huo ulikomeshwa. Jamii:Mbegu za muziki wa Afrika Jamii:Arusha Editathon Muziki
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tuzo_za_Muziki_za_Kisima
| null | 40,131
|
Ziwa Magadi (Kenya)
|
| type = | inflow = | outflow = | catchment = | basin_countries = Kenya | length = | width = | area = 100 km² | depth = | max-depth = | volume = | residence_time = | shore = | elevation = | islands = | cities = | frozen = }} '''Ziwa Magadi''' lipo kusini mwa Kenya katika eneo la Bonde la Ufa, kaskazini mashariki kwa Ziwa Eyasi. Ni ziwa la chumvi na kiwango chake cha uchumvi kinazidi asilimia 30[https://www.semanticscholar.org/paper/Microbial-Diversity-of-Soda-Lake-Habitats-Baumgarte/d20a852bd0867382e65376beeaea115aee60acf4 Susanne Baumgarte: Microbial Diversity of Soda Lake Habitats (2003)], tasnifu ya umahiri, Chuo Kikuu cha Braunschweig / Ujerumani. Limepokea jina lake kutokana kiasi kikubwa cha magadi (kabonati ya sodiamu) ndani ya maji yake; wakati wa kiangazi maji ya ziwa hupungua na % 80 ya eneo lake hufunikwa na chumvi hii. Wakati wa msimu wa mvua chumvi huwa inafunikwa tena kwa maji, kisha uzidi tena maji yanapokauka na kuacha chumvi nyeupe. Ni maarufu kwa aina mbalimbali za ndege wanaoishi kandokando ya ziwa hilo, kwa mfano flamingo. Ziwa Magadi lina ukubwa wa kilomita mraba 100 na huwa limejaa maji iliyokolea kabonati ya sodiamu ambayo huwa na kiasi kikubwa cha madini ya trona. Asili ya chumvi hii ni chemchemi moto zinazopatikana katika bonde la Ufa. Chemchemi hizo huwa kaskazini magharibi na kusini mwa ziwa hili. Kuna aina moja tu ya samaki kwenye ziwa hili: cichlid Alcolapia grahami. Samaki huyu anaishi kwenye chemchemi moto zilizo kwenye ufukwe wa ziwa hili. Ziwa Magadi hapo awali halikuwa na kiwango kikubwa cha chumvi. Miaka elfu kadhaa iliyopita (kipindi cha Pleistocene) na katikati ya kipindi cha Holocene lilikuwa na samaki wengi na kiwango cha chumvi kilikuwa cha chini. Kuna muda wa kihistoria ambamo Ziwa Magadi na Ziwa Natron yalikuwa yameshikamana kuwa ziwa moja kubwa. thumb|250px|Ziwa Magadi kutoka anga za mbali. Mji wa Magadi upo kwenye pwani ya mashariki ya ziwa hili. Kiwanda cha soda Magadi kinapatikana kwenye mji huu. * Kisiwa Kirefu (kaunti ya Kajiado) * Kisiwa cha Mwamba (kaunti ya Kajiado) * Orodha ya maziwa ya Kenya * Baker, B.H. 1958. Geology of the Magadi area. Report of the Geological Survey of Kenya, 42, 81 pp. * Behr, H.J. 2002. Magadiite and Magadi chert: a critical analysis of the silica sediments in the Lake Magadi Basin, Kenya. SEPM Special Publication 73, p. 257-273. * Eugster, H.P. 1970. Chemistry and origin of the brines from Lake Magadi, Kenya. Mineralogical Society of America Special Paper, No. 3, p. 215-235. * Eugster, H.P. 1980. Lake Magadi, Kenya, and its Pleistocene precursors. In Nissenbaum, A. (Editor) Hypersaline brines and evaporitic environments. Elsevier, Amsterdam, pp. 195–232. * Jones, B.F., Eugster, H.P., and Rettig, S.L. 1977. Hydrochemistry of the Lake Magadi basin, Kenya. Geochimica et Cosmochimica Acta, v. 41, p. 53-72. Jamii:Bonde la Ufa la Afrika Mashariki Jamii:Maziwa ya Kenya Jamii:Maziwa ya chumvi Jamii:Kaunti ya Kajiado
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ziwa_Magadi_(Kenya)
| null | 12,231
|
Mapishi ya Sierra Leone
|
'''Mapishi ya Sierra Leone''' yana mchanganyiko wa vyakula vya jadi vya makabila mbalimbali kama Wamende, Watemne, na ushawishi wa Wakristo wa Kiingereza na Waislamu. Chakula cha Sierra Leone hutegemea nafaka, maharagwe, samaki, na mboga mbalimbali, pamoja na viungo vya asili kama pilipili na tangawizi. Lugha rasmi ni Kiingereza, lakini Kisierra Leone pia kinazungumzwa katika muktadha wa chakula na mila. Mchuzi wa kisamvu ni mchuzi mzito unaotengenezwa kwa majani ya muhogo, samaki, na viungo mbalimbali, ni chakula cha asili kinachopendwa sana. Wali wa Jollof ni wali mwekundu uliopikwa kwa mchuzi wa nyanya, pilipili, na viungo vingine, maarufu katika nchi nyingi za Afrika Magharibi. Mchuzi wa karanga ni kitoweo chenye mchuzi wa karanga, nyama, na mboga, kinachopikwa kwa muda mrefu kwa ladha tamu na ya kipekee. Fufu ni mkate wa nafaka kama mtama au mahindi, unaoliwa kama kamba ya chakula cha mchuzi. Supu ya pilipili ni supu yenye pilipili nyingi na viungo vingine vya asili, hutumiwa kama dawa na chakula cha kuamsha hamu ya kula. Jamii:Utamaduni wa Sierra Leone Jamii:Chakula cha Kiafrika Jamii:Afrocrowd 2025
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mapishi_ya_Sierra_Leone
| null | 57,209
|
Unyanyasaji wa watoto mtandaoni
|
'''Unyanyasaji wa watoto mtandaoni''' ni aina mpya ya unyanyasaji wa watoto ambao pia hujulikana hivyo kwa sababu ya asili yake, hata kutoka kwa watu wa mbali na wasiojulikana. Unyanyasaji huo unatumia intaneti au simu za mkononi. Ingawa hautokei ana kwa ana, wala hauhitaji kukutana kimwili, unyanyasaji mtandaoni unaweza kusababisha hata athari mbaya za ana kwa ana kwa njia ya ubakaji, unyanyasaji wa kingono n.k. Nchini Marekani, unyanyasaji wa watoto mtandaoni unatambuliwa kama aina ya unyanyasaji wa watoto na Jumuiya ya Kitaifa ya Kuzuia Ukatili kwa Watoto. Ripoti ya Data & Society Research Institute na ya Center for Innovative Public Health Research imeonyesha kwamba 72% za watumiaji wa intaneti wameshuhudia aina mojawapo ya unyanyasaji, na 47% wamepatwa wenyewe. *Janis Wolak, David Finkelhor, Kimberly J. Mitchell, Michele L. Ybarra (February–March 2008). Online "Predators" and Their Victims (PDF) (Vol 63 ed.). American Psychological Association. pp. 111–128. Retrieved 2 March 2018. *Child abuse and neglect". NSPCC.'' Jamii:makosa ya jinai Jamii:Jinsia Jamii:Intaneti Jamii:Editathon 2021-06 Morogor
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Unyanyasaji_wa_watoto_mtandaoni
| null | 36,289
|
4 Novemba
|
Tarehe '''4 Novemba''' ni siku ya 308 ya mwaka (ya 309 katika miaka mirefu). Mpaka uishe zinabaki siku 57. * [] - Cleopa David Msuya, Waziri Mkuu wa Tanzania ([]-[] na []-[]) * [] - Emeka Ojukwu, mwanasiasa Mnigeria * [] - C. K. Williams, mshairi kutoka Marekani * [] - Laura Bush, mke wa George W. Bush, Rais wa Marekani ([]-[]) * [] - Sean Combs, mwanamuziki kutoka Marekani * [] - Felix Mendelssohn, mtunzi wa muziki kutoka Ujerumani * [] - Charles Richet, mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba mwaka wa [] Wakristo wengi, wakifuata mapokeo ya Roma, huadhimisha kumbukumbu za watakatifu Karolo Borromeo, Vitali na Agrikola, Nikandro na Herme, Pierio, Amansi wa Rodez, Perpetui wa Maastricht, Modesta wa Trier, Emeriko wa Hungaria, Felisi wa Valois n.k. Jamii:Novemba
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/4_Novemba
| null | 1,495
|
Sherman Landers
|
'''Sherman George Landers''' (Oregon, Illinois, Machi 24, [] - Springfield,Delaware,Pennsylvania, 15 Mei []) alikuwa mwanariadha kutoka Marekani ambaye alishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya joto ya mwaka []. Mwaka 1920 alimaliza wa tano katika shindano la kuruka mara tatu. Landers-Loomis Field katika Shule ya Upili ya Oregon huko Oregon, Illinois, imetajwa kwa sehemu yake, na kwa mwenzake wa Oregon na Olimpiki Frank Loomis. Jamii:Waliozaliwa 1898 Jamii:Waliofariki 1994 Jamii:Wanariadha wa Marekani
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sherman_Landers
| null | 51,361
|
Kiyangum-Mon
|
'''Kiyangum-Mon''' ni lugha ya Kitorricelli nchini Papua Guinea Mpya inayozungumzwa na Wayangum. Mwaka wa 2000 idadi ya wasemaji wa Kiyangum-Mon imehesabiwa kuwa watu 730. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiyangum-Mon iko katika kundi la Kipalei. *[http://multitree.org/codes/ymo lugha ya Kiyangum-Mon kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/ymo makala za OLAC kuhusu Kiyangum-Mon] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/yang1296 lugha ya Kiyangum-Mon katika Glottolog] *[http://www.ethnologue.com/language/ymo lugha ya Kiyangum-Mon kwenye Ethnologue] Jamii:Lugha za Papua Guinea Mpya
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiyangum-Mon
| null | 18,768
|
Mlembule
|
'''Mlembule''' ni kata ya Wilaya ya Mpwapwa katika Mkoa wa Dodoma, nchini Tanzania, yenye msimbo wa posta 41631. Katika sensa ya mwaka [] wakazi walihesabiwa 11,335 https://www.nbs.go.tz. Wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, idadi ya wakazi ilikadiriwa kuwa 9,458[https://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/majimbo/MAJIMBOApril_Kisw.pdf Makadirio ya Idadi ya Watu katika Majimbo ya Uchaguzi kwa Mwaka 2016, Tanzania Bara], tovuti ya TBS, iliangaliwa Septemba 2020. Jamii:kata za Mkoa wa Dodoma Jamii:Wilaya ya Mpwapwa
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mlembule
| null | 33,542
|
Trakai
|
thumb|250px|Boma la Trakai thumb '''Trakai''' ni mji wa kihistoriai nchini Lituanya. Kuna wakazi 5,357 (mwaka 2009). Mji ulianzishwa []. Kuna boma katika kisiwa: '' Trakų salos pilis'' (Boma la kisima cha Trakai) Iko kando ya Galvė. thumb|right|180px| Picha:Trakai Kenesa.JPG|''Karaite Kenesa'' (sunagogi) Picha:Trakai wooden houses.jpg|''Afisi ya posta'' * [http://www.trakai.lt/index.php?583953362 www.trakai.lt] Jamii:Lituanya Jamii:Miji ya Lituanya
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Trakai
| null | 12,345
|
Bikira Maria
|
right|thumb|Ukuu wa Bikira Maria unamtegemea Mwanae, Yesu. thumb|200px|''[[Stabat Mater'', yaani picha ya Bikira Maria chini ya msalaba wa Yesu, kadiri ya Gentile wa Fabriano, []-[] hivi.]] '''Maria''' alikuwa mwanamke Myahudi aliyeishi kati ya karne ya 1 KK na karne ya 1 BK. Mke wa Yosefu, alimzaa Yesu Kristo. Kwa sababu hiyo na kwa utakatifu wake anapewa heshima ya pekee katika madhehebu mengi ya Ukristo, lakini pia katika Uislamu. Jina asili kwa Kiaramu ni מרים, ''Maryām'' lenye maana ya "Bibi"; watafsiri wa kwanza wa Biblia ya Kiebrania wanaojulikana kama Septuaginta (LXX) waliliacha kama lilivyo wakiandika kwa Kigiriki Μαρίαμ, ''Mariam'', au walilifupisha wakiandika Μαρία, ''Maria''. Katika Kurani jina hilo kwa Kiarabu ni مريم, ''Maryam''. Jina hilo limeenea sana duniani kote, hasa kwa heshima ya mama wa Yesu. Mwenyewe anatajwa kwa kawaida kwa kutanguliza sifa yake mojawapo, hasa ''Bikira''. Mapokeo ya karne ya 2 (Injili ya Yakobo) kuhusu Bikira Maria yanasema alikuwa binti pekee wa Yohakimu na Ana. Lakini habari muhimu zaidi ni zile zinazopatikana katika Biblia ya Kikristo. Maandiko matakatifu yanawasifu watu mbalimbali kutokana na jinsi walivyomuamini Mungu na kutenda makuu kwa ajili ya taifa lake. Abrahamu alimuamini Mungu akawa tayari kumtolea sadaka mwanae Isaka, tukio lililomfanya apate baraka ya pekee ya kuwa baba wa waamini (Mwa 22:15-18). Yosefu, mwana mpenzi wa Yakobo-Israeli, alikuwa mwaminifu hata akaliokoa taifa lisiangamie kwa njaa (Mwa 50:20). Musa ndiye mkombozi wa taifa la Mungu katika Agano la Kale: aliongoza Israeli kutoka utumwani Misri akalipatia sheria kutoka kwa Mungu katika mlima Sinai. Maandiko ya Agano la Kale yanakiri, "Wala hajainuka kiongozi kama alivyokuwa Musa" (Kumb 34:10-12). Waliofuata ni Yoshua, Debora, Gideoni, Ruthu, Samweli, wafalme Daudi na Solomoni, manabii Eliya, Isaya, Yeremia, Ezekieli na wengineo. Mwishoni Yesu Kristo akamsifu Yohane Mbatizaji akisema, "Ni mkuu kati ya uzao wa wanawake" (Lk 7:24-28). Elizabeti, mama wa Yohane, alijiona hastahili kutembelewa na Bikira Maria, Mama wa Yesu, akamuita, "Mama wa Bwana wangu" (Lk 1:43). Bikira Maria si mtu wa ziada katika mpango wa Mungu bali ni mshiriki mkuu wa ukombozi wa binadamu. Maria amechangia wokovu kwa kukubali mpango wote wa Mungu aliyetaka amzae Mwanae, amlee na kumfuata kiaminifu hadi msalabani, aliposhiriki kumtoa kama sadaka ya kutuokoa. Msimamo wake ulikuwa mmoja tu: "Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema" (Lk 1:38). Tukichunguza nafasi yake katika fumbo hilo, tunaweza kukiri pamoja naye kuwa ni Mwenyezi Mungu aliyemtendea makuu (Lk 1:49), kwa kuwa, "Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu" (Yoh 3:27). Yale yote ambayo Wakristo wengi wanayasadiki kuhusu Bikira Maria, hakujipatia bali alijaliwa na Mwenyezi Mungu huku akiitikia kwa hiari fumbo la mpango wake. Biblia inatupatia utabiri uliotolewa na Mungu mwanzoni mwa historia kuhusu mwanamke atakayemshinda nyoka wa kale (Shetani): "Nitaweka uadui kati yako na huyu mwanamke, kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa chako" (Mwa 3:15). Juu ya Eva wa kale, ambaye alidanganywa na kuangushwa na Shetani atende [[dhambi, imesemwa: "Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa, kwa kuwa ndiye aliye Mama wa walio hai" (Mwa 3:20). Hata hivyo Adamu na Eva wa kale wametuletea kifo (Rom 5:12). Mababu wa Kanisa wanamtazama Bikira Maria kama Eva mpya aliyemshinda Ibilisi na kuwa mama wa wote walio hai. Yesu, aliye Adamu mpya, alipokuwa anakamilisha sadaka ya ukombozi pale msalabani alimfanya Mama yake awe Mama wa waliokombolewa kwa kumkabidhi mwanafunzi, tena yule aliyempenda zaidi. "Penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, Mariamu wa Kleopa, na Mariamu Magdalene. Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, "Mama, tazama, mwanao". Kisha akamwambia yule mwanafunzi, "Tazama, mama yako". Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake. (Yoh 19:26-27). Utabiri mwingine ulisema, "Tazama Bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamuita jina lake Emanueli, yaani Mungu pamoja nasi" (Isa 7:14). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:34-35, "Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu akakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli. Kwa sababu hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu". "Imba, ee binti Sion, piga kelele, ee Israeli, furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, ee binti Yerusalemu. Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana yu katikati yako" (Sef 3:14-15). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:28: "Malaika akaingia nyumbani mwake akamwambia, 'Furahi Maria, umejaliwa neema kubwa, Bwana yu pamoja nawe'". "Umebarikiwa wewe katika kila hema la Yuda na katika kila taifa, nao wanaposikia jina lako watafadhaika. Imani yako haitatoka mioyoni mwa watu wanaoukumbuka uweza wa Mungu milele" (Yudithi 14:7; 15:9). Dondoo hilo linalinganishwa na Lk 1:42, "Akapaza sauti kwa nguvu akasema, 'Umebarikiwa wewe kuliko wanawake wote, na yeye utakayemzaa amebarikiwa'". Bikira Maria ni fumbo la ajabu alilolifanya Mungu katika mpango wa wokovu kwa ajili yake na kwa ajili yetu. Jamaa yake Elizabeti alimpongeza tena akiongozwa na Roho Mtakatifu, "Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale uliyoambiwa na Bwana" (Lk 1:45). Hivyo manabii mbalimbali kwa mwanga wa Roho Mtakatifu walimuagua Maria kwa heshima. Mambo yaliyotabiriwa katika Agano la Kale yalitimia katika Agano Jipya: ukombozi ulianza Bikira Maria alipokubali kwa imani fumbo la umwilisho wa Mwana wa Mungu. Bikira Maria hakuwa "chombo" tu kilichotumika bila ya kuelewa, bali alikuwa mshiriki huru wa kazi ya ukombozi ya Mwanae, kwa kuwa alipopashwa habari na malaika alikubali kwa hiari mpango wa Mungu akisema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, na iwe kwangu kama ulivyonena" (Lk 1:38). Yesu, kama mtu yeyote mcha Mungu, aliwaheshimu na kuwatii wazee wake: "Basi, akarudi pamoja nao Nazareti, akawa anawatii" (Lk 2:51). Ishara ya kwanza kwenye maisha ya hadhara ya Yesu iliongozwa na Bikira Maria katika arusi ya Kana ya Galilaya, akisukumwa na huruma kwa wenye shida: kwa ombi lake Yesu aligeuza maji kuwa divai, na wanafunzi wake wakamwamini. Yohane alisimulia hivi, "Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, 'Hawana divai'. Yesu akamwambia, 'Mama tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia'. Mamaye akawaambia watumishi, 'Lo lote atakalowaambia, fanyeni'. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. Yesu akawaambia, 'Jalizeni mabalasi maji'. Nao wakayajaliza hata juu. Akawaambia, 'Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza'. Wakapelekea. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maj), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, akamwambia, 'Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa'. Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini. (Yoh 2:1-12). Bikira Maria anasifiwa kwanza kwa imani yake kuu kabisa, kuliko kwa kumchukua Yesu tumboni tu. Yesu alitaka kuwainua wasikilizaji wake wafuate mambo ya roho kuliko ya mwili. "Basi, mtu mmoja akamwambia, 'Mama yako na ndugu zako wako nje, wataka kusema nawe'. Lakini Yesu akamjibu huyo mtu aliyemwambia hivyo, 'Mama yangu ni nani, na ndugu zangu ni akina nani?' Kisha akanyosha mkono wake juu ya wanafunzi wake akasema, 'Hawa ndio Mama yangu na ndugu zangu, maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye kaka yangu na dada yangu na mama yangu'" (Math 12:46-50). Vilevile, wakati wa utume wake, alimsikia "mwanamke mmoja katika lile kundi la watu akisema, 'Hongera kwa mwanamke aliyekuzaa na kukunyonyesha'. Yesu akamjibu, 'Barabara, lakini heri yake zaidi yule anayelisikia Neno la Mungu na kulishika'" (Mk 11:27-28). Katika kumfuata Mwanae Bikira Maria alitabiriwa wazi na mzee Simeoni uchungu kama upanga utakaopenya moyo wake, "Tazama huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. Nawe mwenyewe uchungu ulio kama upanga utauchoma moyo wako" (Lk 2:34-35). Bikira Maria alishiriki kwanza mateso ya ukimbizi huko Misri kwa lengo la kumficha Mwanae asiuawe na Herode Mkuu, "Hivyo Yosefu aliamka akamchukua mtoto pamoja na Mama yake akaondoka usiku akaenda Misri akakaa huko mpaka Herode alipokufa" (Math 2:14-15). Bikira Maria alishuhudia hatua kwa hatua kuteswa kwa Yesu; wanafunzi walipokimbia au kumtazama kwa mbali, yeye alikuwa karibu akaona vema kila teso lililompata Mwanae. Kutokana na fungamano la upendo wa ajabu lililokuwepo kati ya Yesu na Mamaye, alipoyashuhudia yote aliteseka sana katika moyo wake safi, kiasi kwamba Bernardo wa Klervoo akasema, "Msalaba wa Yesu uliwasulubisha wote wawili, Yesu mwilini na Mama yake moyoni". Uaguzi wa mzee Simeoni ulitimia hivyo. Kadiri ya mtume Paulo kuteseka ni kutimiliza yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya Kanisa, "Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo" (Kol 1:24). "... maana tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake" (Rom 8:17b). Pale msalabani Bikira Maria, kwa njia ya mtume Yohane alifanywa Mama wa wote wanaompenda Mwanae; kisha kumzaa pasipo uchungu Bwana wa uzima, pale alituzaa sisi kwa uchungu wa kutisha uliotokana na kumuona Mwanae akifa msalabani. Hata hivyo Bikira Maria aliendelea kumuamini Mwanae aliyeonekana ameshindwa. Bikira Maria alikuwepo hapo mwanzo wa Kanisa, akilivutia zaidi Roho Mtakatifu kwa sala yake. "Hao wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria Mama yake Yesu na ndugu zake" (Mdo 1:14). Yesu alisema, "Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili, lakini atakapokuja huyo Roho wa ukweli atawaongoza kwenye ukweli wote" (Yoh 16:12-13). Kwa msaada wa Roho Mtakatifu heshima kwa Bikira Maria ilienea katika Kanisa lote tangu zamani kabisa kadiri ya utabiri wake kuwa ataheshimiwa na vizazi vyote, "Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mdogo, hivyo tangu sasa vizazi vyote wataniita mwenye heri" (Lk 1:48). Kuna mafundisho makuu manne kumhusu Bikira Maria ambayo ni lazima kila Mkatoliki ayasadiki kutokana na ufunuo wa Mungu: # B. Maria mkingiwa dhambi ya asili # B. Maria Mama wa Mungu # B. Maria Bikira daima # B. Maria kupalizwa mbinguni mwili na roho Malaika alimsalimia Maria "umejaa neema" (Lk 1:28) maana ndiye tunda bora la ukombozi ulioletwa na Yesu. Ni imani ya Wakatoliki kwamba kwa stahili za Mwanae alikingiwa asirithi kwa wazazi dhambi ya asili na madonda yanayotokana nayo, wala asitende dhambi maisha yake yote. Kwa maneno mengine, Bikira Maria tangu atungwe mimba Mungu alimkinga na kila doa la dhambi kwa kutazamia stahili za Yesu Kristo aliye Mkombozi wa binadamu wote. Maria ndiye aliyekombolewa kwa namna bora kushinda viungo vyote vya Kanisa. Maisha yake yote hakutenda dhambi hata moja. Mapokeo ya mashariki yanamuita "A Panagia" = "Mtakatifu tu". Dogma hiyo ilitangazwa na papa Pius IX mwaka [], halafu mwaka [] Bikira Maria alijitambulisha kama Mkingiwa kwa Bernadeta Soubirous huko Lurdi (Ufaransa) kadiri ya njozi zilizokubaliwa na Kanisa hilo. Tena waumini wake wanaelekezwa kuamini kwamba mwaka [] huko Fatima (Ureno) aliwafunulia Lusia, Fransisko na Yasinta Marto moyo wake safi usio na doa. Injili ya Yohane inaanza kwa kishindo, "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu" (Yoh 1:1). Huyo Mungu Mwana alitwaa ubinadamu katika Bikira Maria akazaliwa mtoto, jina lake Yesu, maana yake Mungu Mwokozi. Huyo ni binadamu kama sisi katika yote isipokuwa dhambi. Ubinadamu wa Yesu unategemea Nafsi yake ya Kimungu: akisema, 'Mimi', ni kwa Nafsi yake hiyo. Ndiyo maana aliwaambia Wayahudi, "Kweli nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, nalikuwepo" (Yoh 8:50). "Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo alivyomjalia Mwanae kuwa asili ya uhai" (Yoh 5:26). Mtume Paulo akaeleza, "Wakati maalumu ulipotimia Mungu alimtuma Mwanae aliyezaliwa na mwanamke" (Gal 4:4). Bikira Maria ni Mama wa Mungu kwanzia wakati huo: tangu Bikira Maria alipojaliwa kumchukua mimba, kumzaa, kumnyonyesha na kumlea mtu ambaye kwa asili ni Mungu. Cheo hicho kimemuinua juu kuliko hata malaika. "Malaika alimwambia, 'Hicho kitakachozaliwa kitaitwa Kitakatifu, Mwana wa Mungu'" (Lk 1:35). Dogma ilitangazwa mwaka [] kwenye Mtaguso wa Efeso uliomuita "Mzazi wa Mungu", ukisema Maria anastahili kuitwa hivyo kwa sababu Mwana wa milele wa Mungu, ambaye ni Mungu sawa na Baba, alifanyika mtu toka kwake. Akiwa mja mzito alishangiliwa: "Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?" (Lk 1:42-43). Ungamo hilo la Elizabeti likakamilishwa na Mtume Thoma aliyemuambia Yesu mfufuka: "Bwana wangu na Mungu wangu!" (Yoh 20:28). Wakristo na Waislamu wote wanakiri kuwa Yesu alitungwa bila ya mchango wa mwanamume. La ajabu zaidi katika imani hiyo ni kwamba hata uzazi wenyewe haukuondoa ubikira wake, bali uliutakasa: ni Bikira daima. Ingawa akili inasita, ni lazima kukiri na malaika, "Hakuna lisilowezekana kwa Mungu" (Lk 1:38). Yosefu, ingawa kisheria alikuwa mume wake, hakutenda naye tendo la ndoa. Ni imani ya Wakatoliki na Waorthodoksi kuwa Mama wa Yesu anastahili kuitwa "Bikira daima" kwa sababu alimchukua mimba akiwa bikira, akamzaa bila ya kupotewa na ubikira, akabaki bikira hadi mwisho wa maisha yake. Hamu yake ya kuwa bikira hata kisha kuchumbiwa inajitokeza katika jibu alilompa malaika aliyemtabiria mimba: "Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?" (Lk 1:35). Ni kielelezo cha Wakristo ambao Mtume Paulo aliwaandikia: "Nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi" (2Kor 11:2), "mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine" (1Kor 7:35). Wanaosemwa katika Injili "ndugu zake Yesu" si watoto wa Bikira Maria, bali ndugu wa ukoo waliokuwa jirani sana na familia hiyo takatifu. Kama Bikira Maria angekuwa na watoto wengine, Yesu angekuwa amefanya kosa la kuwanyang'anya Mama yao na kumfanya awe Mama wa mtume Yohane alipomkabidhi msalabani, "'Mwana, tazama Mama yako'. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake" (Yoh 19:27). Katika Agano Jipya yupo Yakobo anayeitwa na mtume Paulo "ndugu yake Bwana" (Gal 1:19): Yakobo huyo alikuwa maarufu katika Kanisa la Yerusalemu (Mdo 12:7; 15:13-21; 21:18-20; Gal 2:9). Yakobo huyo si mtume Yakobo kaka yake Yohane (Lk 6:12-16), bali ni Yakobo ndugu yake Yose na mama yao kwenye Injili anaitwa "Maria mwingine", si Maria Mama wa Yesu. "Walikuwepo pia wanawake waliotazama kwa mbali. Miongoni mwao akiwa Maria Magdalena, Salome na Maria mama wa akina Yakobo mdogo na Yose" (Mk 15:40). Maria lilikuwa jina la kawaida kwa Wayahudi: akina Maria wakiwa wengi hivyo, tujue kuwatofautisha kwenye Injili, ambazo zinamtaja Bikira Maria kama "Mama wa Yesu". Baada ya maisha haya ya duniani Bikira Maria alipalizwa mbinguni mwili na roho, ishara ya mwanamke mshindi. "Ishara kubwa ikaonekana mbinguni, ambapo mwanamke aliyevikwa jua, pia na mwezi chini ya miguu yake, na taji la nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake" (Ufu 12:1). Maneno ya shangilio lake yametimia: Mungu "amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; na wanyonge amewakweza" (Lk 1:52). Imani hiyo ya mapokeo ya kale, yanavyoshuhudiwa na Mababu wa Kanisa, ilitangazwa rasmi na Papa Pius XII kwa niaba ya maaskofu wote mwaka []. Katika liturujia ya Roma, mbali ya kumtaja Mama Bikira Maria katika kila Misa wakati wa sala ya ekaristi, kuna maadhimisho kwa heshima yake. Hapa yamepangwa kulingana na kiwango cha heshima hiyo: *8 Desemba – Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili *1 Januari – Bikira Maria Mama wa Mungu *25 Machi – Bikira Maria Kupashwa Habari *15 Agosti – Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni *31 Mei – Ziara ya Bikira Maria *8 Septemba – Kuzaliwa kwa Bikira Maria *Mei-Juni - Mama wa Kanisa *Juni – Moyo Safi wa Maria *15 Septemba – Bikira Maria wa Mateso *22 Agosti – Bikira Maria Malkia *7 Oktoba – Bikira Maria wa Rozari *21 Novemba – Bikira Maria Kutolewa Hekaluni *11 Februari – Bikira Maria wa Lurdi *13 Mei – Bikira Maria wa Fatima *16 Julai – Bikira Maria wa Mlima Karmeli *5 Agosti – Kutabaruku Kanisa la Bikira Maria *12 Septemba – Jina takatifu la Maria *10 Desemba – Bikira Maria wa Loreto *12 Desemba – Bikira Maria wa Guadalupe Tena kila Jumamosi isiyo na adhimisho maalumu, Kanisa huadhimisha kumbukumbu ya hiari ya Mama wa Mungu. Pia zipo heshima za binafsi kwa Bikira Maria: mashariki zinatumika tenzi na nyimbo mbalimbali, k.mf. Akatistos inayomuita "daraja linalounganisha dunia na mbingu", "ngazi aliyoiona Yakobo" "kina kisichochunguzika kwa macho ya malaika" (Mwa 28:12); magharibi anaheshimiwa kwa rozari. Wakristo wanaomheshimu Bikira Maria hawamuabudu hata kidogo, lakini wanamtolea heshima ya juu kuliko watakatifu wengine. Tofauti ni kwamba Mungu tu anastahili kuabudiwa (kwa Kigiriki, 'latria') watakatifu wanapewa heshima ('dulia') na Bikira Maria heshima zaidi ('yuper-dulia'). Kanisa Katoliki linakiri neema zote za Mungu zinampitia Maria. left|thumb|300px|[[Panagia kutoka Yaroslavl, karne ya 13.]] Kwa kiasi kikubwa imani ya Waorthodoksi kuhusu Maria inalingana na ile ya Wakatoliki, ingawa hawakubali jinsi baadhi ya dogma hizo zilivyotangazwa na pengine hata jinsi zinavyofafanuliwa. Martin Luther alipoanza Matengenezo ya Kiprotestanti aliandika kwa heshima juu ya Bikira Maria, lakini kadiri mabishano yalivyozidi kati ya madhehebu ya Kikristo, Waprotestanti walizidi kupinga mafundisho ya Kanisa Katoliki juu ya Mama wa Yesu. Siku hizi baadhi yake, hasa Waanglikana na Wamethodisti wanamrudishia Maria nafasi yake kama kielelezo cha imani na cha kupokea neema ya Mungu. Kurani inamtaja mwanamke mmoja tu, tena mara 34: ni Mariamu, mama wa nabii Isa. Akichanganywa na dada wa Haruni na Musa, aliyekuwa na jina hilohilo, anatajwa kama binti Imrani. Pia habari nyingine kadhaa zinapishana na zile za Injili. Hata hivyo anapewa heshima ya pekee, kama inavyoonekana katika sura ya 3:43: "Na kumbukeni malaika waliposema, 'Ewe Mariamu, kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuchagua na kukutakasa na kukutukuza kuliko wanawake wa walimwengu". Tena katika aya 3:46: "Na kumbukeni waliposema malaika: 'Ewe Mariamu, bila shaka Mwenyezi Mungu anakupa habari njema za Neno litokalo kwake, jina lake Masihi Isa mwana wa Mariamu, mwenye heshima katika dunia na ahera, na yu miongoni mwa waliokaribishwa'". Aliambiwa amefanywa "ishara" pamoja na mwanae, ingawa haisemwi ni ishara ya nini. Sura ya 19, yenye jina lake, inaeleza kwamba Malaika Jibrili (Gabrieli) akimpasha habari ya mimba alisema, 'Hakika mimi ni mjumbe wa Mola wako ili nikupe mwana mtakatifu'. Akasema, 'Ninawezaje kupata mtoto hali hajanigusa mwanamume yeyote, wala mimi si mwasherati?' Akasema, 'Ni kama hivyo; Mola wako amesema: Haya ni rahisi kwangu, na ili tukufanya ishara kwa mwanadamu na rehema itokayo kwetu, na ni jambo lililokwisha hukumiwa' " (19:19-21). "Na mwanamke yule aliyejilinda tupu yake na tukampulizia roho yetu na tukamfanya yeye na mwanawe ishara kwa walimwengu" (21:91). Pamoja na kusifiwa kwa usafi wake, anaongezewa sifa za imani na unyenyekevu: "Na Mariamu binti Imrani aliyejilinda uchi wake, na tukampulizia humo Roho yetu na kayasadikisha maneno ya Mola wake, na vitabu vyake; na alikuwa miongoni mwa wanyenyekevu" (66:12). * Das Mirakel (as a statue which comes to life) * Saint Mary (Iranian film) * Mary Mother of Christ * Mary, Mother of Jesus * Jesus of Nazareth * Color of the Cross * Ben-Hur (1959 film) * The Greatest Story Ever Told * The Living Christ Series * The Nativity Story * The Miracle (a remake of ''Das Mirakel'', as a statue which comes to life) * The Miracle of Our Lady of Fatima * The Song of Bernadette * The Passion of the Christ * The Passion (TV serial)http://www.guardian.co.uk/media/2007/aug/18/religion.news featured in ITV documentary * King of Kings (1961 film) File:Madonna catacomb.jpg|Picha ya zamani zaidi kumuonyesha Maria akimnyonyesha mtoto Yesu, Catacomb of Priscilla, Roma (karne ya 2) File:Panachranta.jpg|''Theotokos Panachranta'', Gertrude Psalter, (karne ya 11) File:Kings College Chapel-IMG 3962.jpg|''Heshima ya Mamajusi'', mchoro wa Rubens ([]) File:Ethiopia-Axum Cathedral-fresco-Black Madonna.JPG|Black Madonna na Mtoto, Axum, Ethiopia File:Angelico, madonna col bambino, pinacoteca sabauda.jpg|''Madonna of humility'', mchoro wa Fra Angelico, ([] hivi). File:Flight into Egypt - Capella dei Scrovegni - Padua 2016.jpg|''Kukimbilia Misri'', mchoro wa Giotto ([]) hivi. Image:Pietro lorenzetti, compianto (dettaglio) basilica inferiore di assisi (1310-1329).jpg|''Kumuomboleza Yesu'', mchoro wa Pietro Lorenzetti, Basilika la Mt. Fransisko, Assisi, ([]–[]) File:saintmaryghaxaq.JPG|Sanamu ya Kupalizwa Mbinguni, Ghaxaq, Malta ([]) File:Tomb of the Virgin Mary. Altar.jpg|Undani wa Kaburi la Maria, kwenye Mlima wa Mizeituni, Yerusalemu * Claudio Monteverdi: Vespro della Beata Vergine (1610) * J.S. Bach, Magnificat: Ave Maria Prelude (1722) * Franz Schubert: Ave Maria (1835) * Charles Gounod: Ave Maria (1859) *Watakatifu wa Agano la Kale *Orodha ya Watakatifu Wakristo *Orodha ya Watakatifu wa Afrika *Orodha ya Watakatifu Wafransisko * Brown, Raymond E.; Donfried, Karl P.; Fitzmyer, Joseph A.; & Reumann, John, (eds.),''Mary in the New Testament'', Fortress/Paulist Press, 1978, ISBN 0-8006-1345-7 * Brownson, Orestes, ''Saint Worship and the Worship of Mary'', [http://www.sophiainstitute.com/ Sophia Institute Press], 2003, ISBN 1-928832-88-1 * Corner, Dan. ''Is This The Mary Of The Bible?'', Evangelical Outreach, 2004, 249 pages ISBN 0-9639076-7-0 * Cronin, Vincent, ''Mary Portrayed'', London: Darton, Longman & Todd, Ltd., 1968, ISBN 0-87505-213-4 * Epie, Chantal. ''The Scriptural Roots of Catholic Teaching'', [http://www.sophiainstitute.com/ Sophia Institute Press], 2002, ISBN 1-928832-53-9 * Fox, Fr. Robert J., '' Catechism on Mary'', '' Immaculate Heart of Mary'', ''Mary Through the Ages'' [http://fatimafamily.org/ Fatima Family Apostolate] * Glavich, Mary Kathleen, ACTA Publications, 2007 * Graef, Hilda. ''Mary: A History of Doctrine and Devotion'', London: Sheed & Ward, 1985, ISBN 0-7220-5221-9 * Groeschel, Benedict, ''A Still, Small Voice: A Practical Guide on Reported Revelations'', San Francisco: Ignatius Press, 1993 ISBN 0-89870-436-7 * Hahn, Scott, ''Hail, Holy Queen: The Mother of God in the Word of God'', Doubleday, 2001, ISBN 0-385-50168-4 * Marley, Stephen, ''The Life of the Virgin Mary'', Lennard Publishing, 1990, ISBN 1-85291-024-0 * Maunder, Chris (ed.), ''The Origins of the Cult of the Virgin Mary'', Burns&Oates/Continuum, 2008, ISBN 978-0-86012-456-6 * Mills, David. ''Discovering Mary: Answers to Questions About the Mother of God'', 2009, ISBN 0-86716-927-3 * Miravalle, Mark. '' Introduction to Mary'', [http://www.queenship.org/ Queenship Publishing], 1993, Second Edition 2006, soft, 220 pages ISBN 1-882972-06-6 * Newman, Barbara. ''God and the Goddesses'', Philadelphia: University of Pennsylvania Press, 2003, ISBN 0-8122-1911-2 * Pelikan, Jaroslav. ''Mary Through the Centuries: Her Place in the History of Culture'', [http://www.yale.edu/yup/ Yale University Press], 1998, hardcover, 240 pages ISBN 0-300-06951-0; trade paperback, 1998, 240 pages, ISBN 0-300-07661-4 *Shoemaker, Stephen J. (2002, 2006). [http://www.oup.com/uk/catalogue/?ci=9780199210749 ''Ancient Traditions of the Virgin Mary's Dormition and Assumption''] . Oxford University Press, Oxford. ISBN 0-19-925075-8 (Hardcover 2004, Reprint), ISBN 0-19-921074-8 (Paperback 2006) * Gambero, Luigi (1999) ''Mary and the fathers of the church'' ISBN 0-89870-686-6 * Josemaria, Anthony (2008) ''The Blessed Virgin Mary in England'' ISBN 0-595-50074-9 * Maximus the Confessor, [http://yalepress.yale.edu/YupBooks/book.asp?isbn=9780300175042 ''The Life of the Virgin: Translated, with an Introduction and Notes''] , Stephen J. Shoemaker, trans. (New Haven: Yale University Press, 2012) (ISBN 0-300-17504-3) * * [http://www.mariologicalsociety.com/ Marilogical Society of America] * [http://campus.udayton.edu/mary/aboutmary2.html University of Dayton─The Mary Page] * * [http://www.churchfathers.org/category/mary-and-the-saints/mary-without-sin/ Church Fathers on the Sinless Nature of Mary] * [http://www.churchfathers.org/category/mary-and-the-saints/mary-ever-virgin/ Church Fathers on the Perpetual Virginity of Mary] Jamii:Ukristo Jamii:Bikira Maria Jamii:Wafuasi wa Yesu Jamii:Watakatifu wa Israeli Jamii:Manabii wa Agano Jipya Jamii:Watu wa Biblia Jamii:Watu wa Kurani Jamii:Waliozaliwa karne ya 1 KK Jamii:Waliofariki karne ya 1 Jamii:Yesu Kristo Jamii:Wayahudi
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bikira_Maria
| null | 4,926
|
Uwanja wa ndege wa Uíge/Carmona
|
'''Uwanja wa ndege wa Uíge/Carmona''' ni uwanja wa ndege unaotumiwa na umma upande wa magharibi wa Uíge, mji mkuu wa Mkoa wa Uíge nchini Angola . Njia ya ndege pia ina mita 65 kizingiti kilichohamishwa kwa kila ncha. Nuru ya Uíge isiyo ya mwelekeo (Kitambulisho: '''UG''' ) iko maili 2.2 kusini mwa njia ya kurukia ndege. Jamii:Viwanja vya ndege nchini Angola Jamii:Africa Wiki Challenge Arusha 2022 Jamii:Uige (mkoa)
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Uwanja_wa_ndege_wa_Uíge/Carmona
| null | 41,817
|
Girolamo Boncompagni
|
'''Girolamo Boncompagni''' (23 Machi [] – 24 Januari []) alikuwa kardinali wa Kanisa Katoliki. Alizaliwa Isola del Liri akiwa mwana wa Don Gregorio I Boncompagni, Duke wa Pili wa Sora, Aquino, Arce na Arpino, Marquess wa Tatu wa Vignola, na mke wake Eleonora Zapata anayeitwa Zappi na mjukuu wa mjukuu wa Papa Gregori XIII. Wikipedia:SPS| Jamii:Waliozaliwa 1622 Jamii:Waliofariki 1684 Jamii:maaskofu Wakatoliki Jamii:makardinali Jamii:Watu wa Italia
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Girolamo_Boncompagni
| null | 55,469
|
Orodha ya mito ya wilaya ya Pallisa
|
'''Orodha ya mito ya wilaya ya Pallisa''' inataja kwa mpangilio wa alfabeti baadhi tu ya mito ya eneo hilo la Uganda mashariki kabla ya kumegwa ili kuunda wilaya mpya ya Butebo. * Mto Kakoro * Mto Nabwali * Orodha ya mito ya Uganda Jamii:Orodha za kijiografia Jamii:Wilaya ya Pallisa Jamii:Mito ya Uganda Jamii:Mkoa wa Mashariki (Uganda)
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Orodha_ya_mito_ya_wilaya_ya_Pallisa
| null | 28,025
|
Kiwogamusin
|
'''Kiwogamusin''' ni lugha ya Kisepik nchini Papua Guinea Mpya inayozungumzwa na Wawogamusin. Mwaka wa 1998 idadi ya wasemaji wa Kiwogamusin imehesabiwa kuwa watu 700. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiwogamusin iko katika kundi la Kiwogamusin-Chenapian. *[http://multitree.org/codes/wog lugha ya Kiwogamusin kwenye Multitree] *[http://www.language-archives.org/language/wog makala za OLAC kuhusu Kiwogamusin] *[http://glottolog.org/resource/languoid/id/woga1249 lugha ya Kiwogamusin katika Glottolog] *[http://www.ethnologue.com/language/wog lugha ya Kiwogamusin kwenye Ethnologue] Jamii:Lugha za Papua Guinea Mpya
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiwogamusin
| null | 18,827
|
When You're Mad
|
'''"When You're Mad"''' ni wimbo wa tatu kutoka katika albamu ya kwanza ya mwimbaji-mtunzi wa muziki wa R&B-pop wa Kimarekani Ne-Yo. Wimbo unatoka katika albamu ya In My Own Words. Wimbo ulipata kushika nafasi ya 15 katika chati za Billboard Hot 100 bora na kufikia hadi katika tano bora ya chati ya muziki wa R&B. Wimbo huu ni wa pili katika moja kati ya nyimbo za Ne-Yo ambazo hazikutolewa katika Uingereza. Wimbo unazungumzia jinsi Ne-Yo anavyoweza kuongea sana na wasichana wengine, kitendo ambacho kinamtia wazimu mno mpenzi aliyenaye. Ne-Yo aligundua pale mpenzi wake akiwa amekasirika anakuwa na mvuto wa ajabu, na anafanya vyovyote awezavyo ili aweze kumkera mpenzi wake huyo. Pale wale wote wakiwa na wazimu, halafu baadaye wanaonekana wakiwa wamelala pamoja, huku wakiwa wamesahau kile kilichowafanya wawe na wazimu. * [http://ne-yofan.com/lyrics/in-my-own-words/when-youre-mad/ Mistari ya When You're Mad] Category:Nyimbo za 2006 Category:Nyimbo za Ne-Yo
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/When_You're_Mad
| null | 4,988
|
Toi
|
300px|thumbnail|[[Gololi (hapa za kioo) ni vichezeo vinavyopendwa kote duniani]] '''Toi'''"toi" ni jaribio la kutumia neno la Kiingereza jinsi linavyoweza kusikika mjini Dar es Salaam kwa jambo ingawa haionekani katika maandishi ya Kiswahili, ''(ing. toy)'', pia '''kichezeo'''Kichezeo si neno la kawaida kwa Kiswahili; hadi sasa hakuna nomino moja kwa "kitu cha kuchezea" lililo kawaida kwa Kiswahili. "Kichezeo" imewahi kutumiwa mara chache kwenye blogu kadhaa na kurasa nyingine. Inapatikana pia katika kamusi ya Legere, Kijerumani-Kiswahili ni kitu cha kuchezea, hasa kwa watoto. Mifano yake ni mwanasesere, mpira au gololi. Lakini si watoto pekee wanaotumia toi hutumiwa pia na watu wazima au wanyama. Kwa mfano paka hupenda kucheza kwa mpira. Katika mazingira ya kijadi watoto wanatumia vitu vinavyopatikana kiasili kama mawe na mafimbo. Halafu wanatumia udongo wa kushikana (kama udongo wa mfinyazi) na kufinyanga vidoli. Mahali pengi wazazi waliwatengenezea watoto toi za aina mbalimbali. Watoto walipewa pia au kujitengenezea vifaa vidogo vya kufanana na vifaa vya wtu wazima. Mifano ni pinde na mishale midogo, au sufuria za kuiga shughuli za wakubwa. Katika mazingira ya mjini watu walianza kutengeneza toi na kuziuza. Katika utamaduni wa Ugiriki ya Kale ilikuwa kawaida ya kwamba watoto walitoa vichezeo kama sadaka kwa miungu kwenye hekalu wakati wa kubalehe kama ishara ya kwamba wamekuwa wakubwa sasa.Powell, Barry B. (2001). Classical Myth; Third Edition. Upper Saddle River, NJ: Prentice Hall. pp. 33–34. ISBN 0-13-088442-1 . Katika mazingira ya kisasa toi zimekuwa biashara kubwa. Hutengenezwa viwandani na kupelekwa kote duniani. Kwa mfano huko Marekani biashara ya vitu vya kuchezea ilikuwa na thamani ya bilioni 22.9 za dolar za Marekani. Asilimia 88 za biashara hii ilikuwa kwa watoto wenye umri wa miaka 0–11. Asilimia 75% za vichezeo vyote vilivyouzwa Marekani vilitengenezwa huko China. File:Little horse on wheels (Ancient greek child's Toy).jpg|Doli ya farasi mwenye magurudumu, kichezeo cha Ugiriki ya Kale File:COLLECTIE_TROPENMUSEUM_Houten_autobus_kinderspeelgoed_TMnr_4444-1.jpg|Basi ya ubao kwa kuchezea file:Poupée Turkana-Kenya.jpg|Doli kutoka Turkana, Kenya File:LEGO-01.jpg|Matofali ya plastiki ya Lego Jamii:Burudani Jamii:Uchumi
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Toi
| null | 19,014
|
James Watt
|
thumb|right|James Watt thumb|right|Sampuli ya injini ya mvuke ya James Watt '''James Watt''' (19 Januari [] - 19 Agosti []) alikuwa mhandisi kutoka Uskoti. Amekuwa maarufu kwa kuboresha injini ya mvuke kufikia kiwango kilichowezesha matumizi ya mashine hii kwa viwanda. Kwa njia hiyo alikuwa katiy a watu waliweka msingi kwa mapinduzi ya viwanda wa karne ya 18 na karne ya 19. Alizaliwa Uskoti katika familia ya kipresbiteri kama mtoto wa mjenzi wa meli. Shuleni alipenda hisabati na kusoma mengi lakini lugha na historia aliacha kando. Angependa kuwa daktari lakini wazazi walishindwa kumgharamia masomo ya chhuoni. Alipofikia umri wa miaka 17 aliingia katika mafunzo ya fundi makanika huko London. Aliamwacha fundi mwalimu alipoona hajifunzi kitu kipya tena bila kusubiri kutimiza miaka saba ya kawaida na kwa sababu hiyo hakutambuliwa kama fundi kamili. Watt alibahatika alipopata kazi ya fundi kwa vifaa vya upimaji kwenye chuo kikuu cha Glasgow. Alipendwa na walimu na wanafunzi waliokutana katika karakana ndogo ya Watt kwa majadiliano. Profesa wa fizikia Joseph Black na mwanauchumi Adam Smith wakawa marafiki zake. Mwaka 1760 Watt alimwoa Margaret Miller. Kati ya watoto wao ni mwanawe James pekee aliyeishi kufikia umri mkubwa. Mwaka 1764 rafiki mwingine Profesa John Robison alimwonyesha injini ya mvuke. Watt alianza kusoma yote juu ya teknolojia hii yaliyopatikana kwake. Chuo kikuu kilikuwa na injini moja iliyoharibika na Watt alipewa kazi ya kuitengeneza. Alifaulu lakini aliona ya kwamba injini ilikuwa na tatizo la muundo wake kwa sababu kiasi kikubwa cha nishati kilipotea badala ya kufanya kazi. Watt alitengeneza sampuli ndogo ya injini bora. Marafiki kwenye chuo kikuu walimsaidia kwa kumpa pesa alipotengeneza injini kubwa. Utengenezaji wa mashine hizi ulikuwa na matatizo makubwa. Wafanyakazi wa wakati ule hawakuzoea kutekjeleza shughuli kwa umakinifu uliohitajika kwa mashine hii. Mtajiri aliyomsaidia kwa pesa alishindwa kuendelea na mwenye kiwanda mwingine aliingia akiamini ubora wa muundo wa Watt. Ilichukua miaka kadhaa na msaada wa watu mbalimbali hadi injini ya mvuke iliyoboreshwa ilikuwa tayari kwa uzalishaji na matumizi. Tangu 1785 kiwanda cha Watt na mwenzake kilianza kuleta faida ya kifedha na hali yake ya kiuchumi kilikuwa nzuri. Watt aliendelea kutengezea aina mpya za gia kwa mashine yake iliyowezesha matumizi yake kwa shughuli nyingi. Alibuni pia kizio cha kupima nguvu akaiita "nguvu ya farasi" (horsepower) kinachoendelea kutumiwa duniani kama kipimo kwa nguvu ya injini hata kama kipimo kipya cha SI kinachoitwa "Watt" (wati) kimechukua nafasi yake kitaalamu. Jamii:Waliozaliwa 1736 Jamii:Waliofariki 1819 Jamii:Wahandisi wa Uskoti Jamii:Wavumbuzi
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/James_Watt
| null | 4,282
|
Camillo Astalli
|
'''Camillo Astalli''' (21 Oktoba [] – 21 Desemba []) alikuwa Kardinali wa Kanisa Katoliki wa Italia na Kardinali-Mpwa wa Papa Innocent X ambaye alihudumu kama Kardinali-padri wa San Pietro in Montorio ([]–[]), Camerlengo wa Urika wa Makardinali ([]–[]), na Askofu Mkuu (cheo binafsi) wa Catania ([]–[]).[http://www.catholic-hierarchy.org/bishop/bastpam.html "Camillo Cardinal Astalli-Pamphilj"] ''Catholic-Hierarchy.org''. David M. Cheney. Retrieved September 19, 2016 Jamii:Waliozaliwa 1616 Jamii:Waliofariki 1663 Jamii:Watu wa Italia Jamii:Maaskofu Wakatoliki Jamii:makardinali
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Camillo_Astalli
| null | 55,462
|
Pijini na krioli
|
'''Pijini na Krioli''' ni aina za lugha mpya ambazo zinajitokeza katika mazingira ya pekee. Yafuatayo ni maelezo juu ya tofauti na mahusiano kati ya aina hizo mbili katika asili na matumizi. Lugha zote mbili, Pijini na Krioli, ni lingua franka. Pijini ni lugha ambayo hutokea pale ambapo wazungumzaji wa lugha tofauti hukutana; hapo, ili kukidhi haja yao ya kuwasiliana, inawalazimu kuibua au kutumia lugha moja ambayo itawawezesha kuelewana katika nyanja za mawasiliano. Pijini huzuka mara nyingi kwa ajili ya biashara hasa. Pijini kadhaa zinazoonekana leo zilianza wakati wa ukoloni ambako watu waliotawaliwa na mataifa ya Ulaya kwa hiari yao au kwa kulazimishwa walianza kutumia lugha za Kizungu katika maisha ya kila siku. Pijini ni lugha ya kijuujuu ambapo jamii mbili au zaidi za waongeaji wa lugha tofauti zinazirahisisha ili kuungana katika lugha yenye maneno pamoja na sheria za 'moja kwa moja' kisarufi. Yaani pijini ni matokeo ya mchanganyiko wa lugha ambao muundo na msamiati wake umerahisishwa sana. Lugha ya aina hii basi huwa haizungumzwi na mtu yeyote kama lugha ya kwanza. Izingatiwe pia kuwa kwa kawaida sehemu kubwa ya msamiati pamoja na muundo wa pijini huwa na misingi katika lugha moja tu kati ya lugha zilizoizaa. Mfano wa Pijini ni ule wa Pijini ya Kiingereza au Kiingereza cha Kipijini kinachotumiwa sana Afrika Magharibi. Wakati unapofika wa watu kujifunza pijini kama lugha mama, 1ugha hiyo wanayojifunza na kuiongea kienyeji hujulikana kama Krioli. Hiyo inatokea wakati jamii ya wazungumzaji inapoanza kutegemea Pijini kwa kila hali na kuipokeza kwa watoto wao. Kwa hiyo Pijini ni lugha ya kijuujuu inayotokana na kuengaengwa na lugha zinazojitegemea baada ya kuazimwa msamiati na miundo rahisi ya msamiati. Lugha ya aina hiyo inapoanza kuimarika na kupata waongeaji wake yenyewe, inakuwa Krio1i. Ingawa lugha za Pijini huzitangulia lugha za Krioli katika kuzuka, lugha hizo zote hutokea katika jamii kwa sababu ya mawasiliano ambapo watu wanaozungumza lugha mbalimbali wamekutana na hapana lugha ambayo wanaelewa wote, yaani pale amabapo kila mmoja huzungumza lugha yake ya kipekee. Lugha za Pijini na Krioli huzuka ili kuwaunganisha watu wanaozungumza lugha mbalimbali ili waweze kuelewana. Lugha kama hizo, ambazo huwaunganisha watu wa makabila au mataifa mbalimbali, huitwa lugha franka, lugha sambazi, lugha za mawasiliano mapana, lugha za mahusiano na maingiliano, lugha unganishi na hata lugha za biashara. Kwa misingi hii basi, lugha za Pijini na Kirioli kadri muda unapozonga hukua na huenda ukawa lingua franka ambazo hutokana na watu wa lugha mbalimbali kukutana na kuwepo kwa hitaji la mawasiliano baina yao. Hata hivyo, hii itatokea tu pale lugha hiyo itapata wazungumzaji wengi na pia msamiati uliokomaa. Katika lugha hizo mbili, Pijini hupatikana au kuzalika kwanza. Pijini ikiendelea kuwepo na kutumika kama chombo cha mawasiliano huzalisha Krioli. Kwa hiyo, Pijini ndiyo inayokua na kuzaa Krioli. Hivyo basi lugha hizo mbili zina msingi mmoja, ingawa Krioli huwa imekolea na kupiga hatua zaidi kama lugha kamili. Kwa kifupi, Krioli hutokana na Pijini na hapawezi kamwe kuwepo lugha ya Krioli bila kutanguliwa na lugha ya Pijini. Kwa msingi huo, lugha ya Pijini na ile ya Krioli ni kama pande mbili za shilingi moja. Pijini na Krioli zina uhusiano mkubwa kwa kuwa zote ni lugha kama zilivyo lugha nyingine zozote zile, kwa sababu hutumika katika mawasiliano na pia bila kujali zinapopatikana ulimwenguni. Pijini na Krioli zinazo sifa na sura za kilimwengu ambazo huzifananisha na kuzitofautisha na lugha nyinginezo. Sarufi za lugha hizo mbili zinafanana kote ulimwenguni zinapoongelewa. Msamiati wa lugha za Pijini na Krioli huwa sawa na hufanana kote zinapoongewa. Pijini hutumika katika shughuli za kijamii kana kwamba ni lugha ya kwanza (asili), msamiati wake huongezeka kwa kiasi kikubwa ili kuweza kutosheleza mahitaji ya kila siku ya mawasiliano ya watumizi wake. Katika hali kama hizo, lugha hizi huwa si Pijini hasa, bali hugeuka na kuwa Pijini pana. Kama lugha, Pijini pana huendelea kupanuka kwa kubadilika kimuundo kiasi cha kufikia hatua inayoipa hadhi ya kuwa lugha ya Krioli. Ile hatua ya kubadilika Pijini pana hadi kuwa Krioli hutokana na kupatikana kwa kizazi kinachozungumza lugha hiyo kama lugha asili. Mbali na kupata wazungumzaji asilia, Krioli huwa na msamiati wake mpana na miundo changamano ya kisarufi na maana. Ingawa Krioli ina msamiati mpana kuliko Pijini, la msingi ni kuwa Pijini ndiyo huzaa Krioli. Lugha za Pijini na Krioli huangaliwa na baadhi ya watu kama zisizo muhimu kutokana na asili zake na pia hali za umaskini ambazo wengi wa wale wanaozizungumza hujikita kwamo. Lugha za Pijini na Krioli zinapatikana hasa katika mataifa ya Ulimwengu wa Tatu. Kihistoria, lugha za Pijini na Krioli zimekuwa zikibezwa kwa muda mrefu kutokana na ukweli kuwa lugha hizo zimezuka hivi karibuni tu. Kwa hiyo lugha za Pijini na Krioli hazina historia ndefu kwa sababu zilijitokeza kama zao la ukoloni pamoja na watawala na wafanyabiashara walioingiliana na wenyeji. Pia, msingi wa lugha zote huathiriwa na msamiati kutoka lugha anzishi husika japokuwa huwepo lugha moja inayojitokeza kama msingi wa Pijini husika. Madhara hayo ya Pijini kutawaliwa na lugha moja baina ya lugha iliyokopa msamiati kutoka kwake, hukopwa pia na Krioli inayokuzwa. Ikiwa msingi wa Pijini husika utajikita sana katika lugha moja, kwa mfano lugha ya Kifaransa, Krioli itakayozalika nayo vilevile itakuwa na misingi katika hicho Kifaransa, si katika Kiingereza au Kijerumani. Ingawa Pijini ndiyo huizaa Krioli, pana tofauti za kutosha zinazopinga hoja kuwa pana mahusiano baina ya lugha ya Pijini na Krioli. Japo lugha za Pijini na Krioli zinao uingiliano mwingi, zipo tofauti za hapa na pale. Tofauti hizo ni kama zifuatavyo: Lugha ya Pijini huwa haina wazungumzaji asilia na kwa hali hii, Pijini haiwezi kudaiwa na yeyote yule kuwa ni lugha yake ya kwanza ilhali Krioli hupatikana kutokana na kuwepo kwa kizazi kinachozungumza Pijini kama lugha asilia na Pijini hiyo huwa pana kutokana na kuwa na msamiati mpana. Lugha za Pijini huwa hazina wazawa wanaoweza kuzidai kuwa ni lugha za waliowazaa na kuwalea; kinyume na lugha za Krioli zilizo na wazawa asili. Kiulinganishi, muundo wa lugha za Krioli huwa imara kuliko lugha za Pijini. Hii ni kwa sababu lugha za Krioli huangaliwa kama lugha za kawaida na kwa hivyo zaweza kufanyiwa juhudi za kupangwa. Juhudi hizo za kupangwa kwa lugha za Krioli huzifanya kupewa hadhi ya kutumiwa kama lugha za taifa au hata lugha rasmi. Pijini huwa ni zao la maingiliano ya watu walio na lugha tofauti lakini ambao wanapenda kuwasiliana. Kutokana na hali hiyo, Pijini huwa na muundo sahili kusudi mawasiliano yaweze kusahilishwa bila ugumu mkubwa. Hivyo basi, lugha za Pijini huwa na muundo wa vokali ulio na vokali tano za msingi ambazo ni a, e, i, o, u. Maumbo ya maneno mara nyingi hujikita katika yale ya lugha-msingi ya Pijini husika. Pijini huwa na msamiati finyu. Muundo wa sentensi za lugha za Pijini huwa sahili na wakati mwingine usio wa sentensi zilizokamilika kisarufi. Lugha za Pijini huwa na mawanda finyu ya matumizi kwa sababu mara nyingi hujikita katika shughuli iliyosababisha kuzuka kwake. Yaani, Pijini ikiwa imezuka kwa sababu za biashara au za vita, msamiati wake utajikita katika sajili hiyo fulani. Krioli hujitokeza kuwa tofauti kabisa na Pijini katika kitengo cha msamiati na miundo wa kisarufi. Krioli huwa na msamiati mpana na miundo changamano ya kisarufi na maana. Lugha ya Pijini hutokana na maingiliano ya watu. Hivi ni kusema kuwa Pijini ni zao la hali ya wingilugha katika jamii. Huzuka tu baina ya wazungumzaji wa lugha tofauti wanaohitaji lugha moja ya dharura ya mawasiliano. Krioli ni lugha ambayo wazungumzaji wake hujifunza kama lugha yao ya kwanza tangu wanapozaliwa. Hadhi ya Krioli huwa juu kuliko ya Pijini ambayo hadhi yake huwa ya kiwango cha chini. Hali hiyo hutokea pale ambapo lugha za Krioli hupangwa na muundo wake wa kisarufi kuimarishwa na kubainishwa. Jambo hilo huchangia hadhi ya lugha za Krioli kupanda na kuwa tofauti na ile ipewayo lugha za Pijini na mawanda ya matumizi ya lugha za Krioli hupanuka ili kukidhi mahitaji ya mawasiliano ya watumiaji wake wote. Tofauti nyingine baina ya lugha ya Pijini na Krioli ni kuwa, wakati mwingine Pijini hukosa kukua na kuimarika hadi kufikia kiwango cha Krioli. Jambo hilo hutokana na kuwa shughuli iliyopelekea kuzuka kwa Pijini fulani kukosa umuhimu na hivyo kupelekea Pijini husika kudidimia na kujifia mbali. Jambo hilo huwa halitokei katika lugha ya Krioli. * Pijini * Krioli Jamii:Isimujamii Jamii:Lugha
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Pijini_na_krioli
| null | 17,487
|
Abdullah Al Noman
|
thumb|Abdullah Al Noman]] '''Abdullah Al Noman''' (2 Julai [] – 25 Februari []) alikuwa mwanasiasa wa Bangladesh ambaye aliwahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Taifa cha Bangladesh (BNP). Alikuwa mbunge wa Jatiya Sangsad kwa vipindi vitatu, akiwakilisha jimbo la Chittagong-9.Pia aliwahi kuwa waziri wa Uvuvi na Chakula katika baraza la mawaziri la pili la Khaleda Zia. Jamii:Waliozaliwa 1942 Jamii:Waliofariki 2025 Jamii:Wanasiasa wa Bangladesh
|
swahili_wikipedia
|
https://sw.wikipedia.org/wiki/Abdullah_Al_Noman
| null | 55,213
|
End of preview. Expand
in Data Studio
Swahili Small Clean Corpus (Demo)
One-line summary
A small high-quality Swahili text corpus (≈58k documents, ~52.8 MB) extracted from Swahili Wikipedia and public news sources, cleaned, deduplicated, and split into train / validation / test. Suitable for fine-tuning and small-scale experiments.
Dataset composition
- Languages: Swahili (
sw) - Total rows: ≈58,386
- Size: ≈52.8 MB (parquet)
- Splits: train (≈46.7k rows), validation (≈5.84k rows), test (≈5.84k rows)
- Fields:
titlearticletext— cleaned article text (UTF-8)source— source identifier (swahili_wikipedia,bbc_swahili)url— URL
How the dataset was created
- Downloaded Swahili Wikipedia dump and scraped selected public Swahili news pages.
- Extracted text from XML/HTML; cleaned wiki markup and HTML using regex-based cleaning.
- Performed language filtering (kept Swahili), basic quality filtering (min length, special-char heuristics), and exact deduplication.
- Sampled and saved top-quality documents; created train/validation/test splits.
- Saved in Hugging Face
datasetsformat (Parquet/Arrow) and uploaded to the Hub.
Provenance & license
- Primary source: Swahili Wikipedia (CC BY-SA). If any other sources were included (news sites), please check their terms for redistribution.
- License: CC-BY-SA-4.0 (confirm this is compatible with all included sources; if you included non-free sources, change this field accordingly).
Limitations & safety
- The dataset may contain bias inherent to source texts. Evaluate for harmful content before deploying.
- PII redaction was performed with simple regex heuristics; manual audit is recommended for production use.
Example: Loading the dataset
from datasets import load_dataset
ds = load_dataset("marcoharuni95/swahili-text-corpus")
print(ds)
print(ds['train'][0]['text'][:400])
Example: Minimal fine-tuning snippet (illustrative only)
This is a short example showing how you might begin fine-tuning a causal model (adapt to your environment; use appropriate compute and licenses):
# Example only — adapt model, tokenizer and training loop to your infra.
from transformers import AutoTokenizer, AutoModelForCausalLM
from datasets import load_dataset
ds = load_dataset("maroharuni95/swahili-text-corpus")
train_ds = ds['train']
tokenizer = AutoTokenizer.from_pretrained("meta-llama/Llama-2-7b-hf", use_fast=False)
model = AutoModelForCausalLM.from_pretrained("meta-llama/Llama-2-7b-hf", trust_remote_code=True)
# tokenization & training steps omitted for brevity — see transformers + PEFT docs
Citation
If you use this dataset in research, please cite it as:
@misc{swahili_small_demo_2025,
title = {Swahili Small Clean Corpus (Demo)},
author = {Your Name},
year = {2025},
howpublished = {Hugging Face Dataset},
note = {https://huggingface.co/datasets/YOUR_USERNAME/YOUR_REPO_NAME}
}
Contact
If you have questions or find issues, contact: [email protected].
- Downloads last month
- 59